Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 23.18
Bible en Swahili de l’est


Recensement et fonctions des Lévites

1 Basi Daudi alikuwa mzee, ameshiba siku; akamtawaza mwanawe Sulemani awe mfalme juu ya Israeli.
1 Chroniques 29.28 1 Chroniques 28.5 1 Rois 1.33-1.39 1 Rois 1.1 1 Rois 1.30
2 Akawakusanya wakuu wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi.
Josué 24.1 1 Chroniques 13.1 2 Chroniques 34.29-34.30 1 Chroniques 28.1 Josué 23.2
3 Nao wakahesabiwa Walawi wenye miaka thelathini na zaidi; na jumla yao kwa vichwa, mtu kwa mtu, ikapata thelathini na nane elfu.
1 Chroniques 23.24 Nombres 4.2-4.49
4 Katika hao ishirini na nne elfu walikuwa wa kusimamia kazi ya nyumba ya Bwana; na sita elfu walikuwa maakida na makadhi;
2 Chroniques 19.8 Deutéronome 16.18 Esdras 3.8-3.9 1 Chroniques 26.29-26.31 Malachie 2.7
5 na elfu nne walikuwa mabawabu; na elfu nne walimsifu Bwana kwa vinanda, nilivyovifanya, alisema Daudi, vya kumsifia.
2 Chroniques 29.25-29.26 Amos 6.5 1 Rois 10.12 Esdras 7.7 1 Chroniques 26.1-26.12
6 Basi Daudi akawagawanya kuwa zamu zao sawasawa na wana wa Lawi; Gershoni, Kohathi, na Merari.
1 Chroniques 6.1 2 Chroniques 8.14 Esdras 6.18 2 Chroniques 29.25 1 Chroniques 6.16
7 Wa Wagershoni; Ladani, na Shimei.
1 Chroniques 26.21 Exode 6.17 1 Chroniques 15.7 1 Chroniques 6.17-6.20
8 Wana wa Ladani; Yehieli mkuu wao, na Zethamu, na Yoeli, watu watatu.
1 Chroniques 15.17-15.18 1 Chroniques 15.11 1 Chroniques 6.33-6.34 1 Chroniques 15.7 1 Chroniques 15.20-15.21
9 Wana wa Shimei; Shelomothi, na Hazieli, na Harani, watatu. Hao walikuwa vichwa vya mbari za baba za Ladani.
10 Na wana wa Shimei; Yahathi, na Zina, na Yeushi, na Beria. Hao wanne walikuwa wana wa Shimei.
11 Naye Yahathi alikuwa mkubwa wao, na Zina alikuwa wa pili; lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; basi wakawa mbari ya baba kwa kuhesabiwa pamoja.
12 Wana wa Kohathi; Amramu, Ishari, Hebroni, na Uzieli, watu wanne.
Exode 6.18 Nombres 3.27 1 Chroniques 6.2 Nombres 26.58
13 Wana wa Amramu; Haruni na Musa; naye Haruni akatengwa, ili ayatakase yaliyo matakatifu sana, yeye na wanawe milele, ili kufukiza uvumba mbele za Bwana, kumtumikia, na kubariki kwa jina lake, milele.
Exode 6.20 Deutéronome 21.5 Exode 30.6-30.10 1 Samuel 2.28 Hébreux 5.4
14 Lakini kwa habari za Musa, mtu wa Mungu, wanawe hutajwa miongoni mwa kabila ya Lawi.
Deutéronome 33.1 1 Chroniques 26.23-26.25 Psaumes 90.1
15 Wana wa Musa; Gershomu na Eliezeri.
Exode 18.3-18.4 Exode 2.22 Exode 4.20
16 Wana wa Gershomu; Shebueli mkuu wao.
1 Chroniques 26.24 1 Chroniques 25.20 1 Chroniques 24.20
17 Na wana wa Eliezeri; Rehabia mkuu wao. Yeye Eliezeri hakuwa na wana wengine; lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.
1 Chroniques 26.25
18 Wana wa Ishari; Shelomithi mkuu wao.
1 Chroniques 24.22 1 Chroniques 26.26
19 Wana wa Hebroni; Yeria mkuu wao, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
1 Chroniques 24.23 1 Chroniques 23.12 1 Chroniques 15.9
20 Wana wa Uzieli; Mika mkuu wao, na Ishia wa pili.
21 Wana wa Merari; Mali na Mushi. Wana wa Mali; Eleazari, na Kishi.
Exode 6.19 1 Chroniques 23.6 1 Chroniques 24.26-24.30 1 Chroniques 6.30 1 Chroniques 6.20
22 Akafa Eleazari, wala hakuwa na wana, ila binti tu; na ndugu zao, wana wa Kishi, wakawaoa.
1 Chroniques 24.28 Nombres 36.6-36.8
23 Wana wa Mushi; Mali, na Ederi, na Yeremothi, watu watatu.
1 Chroniques 24.30
24 Hao walikuwa wana wa Lawi, kwa kufuata mbari za baba zao, yaani, vichwa vya mbari za baba zao waliohesabiwa, kwa hiyo hesabu ya majina yao kwa vichwa, hao walioifanya kazi ya utumishi wa nyumba ya Bwana, wenye miaka ishirini na zaidi.
Nombres 10.17 Nombres 10.21 1 Chroniques 23.3 Nombres 4.3 Esdras 3.8
25 Kwa kuwa Daudi alisema, Bwana, Mungu wa Israeli, amewastarehesha watu wake; naye hukaa Yerusalemu milele;
1 Chroniques 22.18 2 Samuel 7.11 2 Samuel 7.1 Psaumes 68.18 Joël 3.21
26 wala Walawi hawahitaji tena kuichukua maskani, na vyombo vyake vyote kwa utumishi wake.
Nombres 4.5 Nombres 7.9 Nombres 4.15 Nombres 4.49 Deutéronome 10.8
27 Maana kwa maneno ya mwisho ya Daudi, hao wana wa Lawi walihesabiwa, wenye miaka ishirini na zaidi.
1 Chroniques 23.24 Psaumes 72.20 2 Samuel 23.1 1 Chroniques 23.3
28 Kwani kazi yao ilikuwa kuwangojea wana wa Haruni katika utumishi wa nyumba ya Bwana, nyuani, na vyumbani, na kwa kuvisafisha vitakatifu vyote, ndiyo kazi ya utumishi wa nyumba ya Mungu;
Néhémie 13.9 2 Chroniques 29.5 Esdras 8.29 1 Chroniques 18.17 1 Rois 6.5
29 tena kazi ya mikate ya wonyesho, na ya unga mwembamba wa sadaka ya unga; ikiwa ni wa maandazi yasiyochachwa, au wa yale yaliyotokoswa, au wa yale yaliyookwa; na kazi ya kila namna ya kipimo na cheo;
Lévitique 19.35-19.36 Lévitique 2.4-2.7 Lévitique 6.20-6.23 Lévitique 24.5-24.9 Exode 25.30
30 nao wasimame kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana, na jioni vivyo hivyo;
1 Chroniques 9.33 2 Chroniques 29.25-29.28 Apocalypse 14.3 2 Chroniques 31.2 Esdras 3.10-3.11
31 na kumtolea Bwana sadaka zote za kuteketezwa, katika siku za sabato, za mwezi mpya, na za sikukuu zilizoagizwa, kwa hesabu kadiri ya agizo lake, daima mbele za Bwana;
Esaïe 1.13-1.14 Psaumes 81.1-81.4 Lévitique 23.39 Nombres 10.10 Nombres 28.1-28.29
32 tena walinde ulinzi wa hema ya kukutania, na ulinzi wa patakatifu, na ulinzi wa wana wa Haruni, ndugu zao, katika utumishi wa nyumba ya Bwana.
Nombres 1.53 Nombres 3.38 Nombres 3.6-3.9 1 Chroniques 9.27 1 Rois 8.4

Cette Bible est dans le domaine public.