Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 18.6
Bible en Swahili de l’est


Prospérité de David

1 Ikawa baadaye, Daudi akawapiga Wafilisti, akawashinda, akautwaa Gathi na vijiji vyake mikononi mwa Wafilisti.
2 Samuel 8.1-8.18 1 Samuel 27.4 2 Samuel 1.20 1 Samuel 5.8
2 Akapiga Moabu; na hao Wamoabi wakawa watumwa wa Daudi wakaleta zawadi.
1 Rois 10.25 Esaïe 16.1 2 Rois 3.4-3.5 1 Rois 10.2 Psaumes 72.8-72.10
3 Tena Daudi akampiga Hadadezeri, mfalme wa Soba, mpaka Hamathi, alipokwenda kujisimamishia mamlaka yake kwenye mto wa Frati.
Psaumes 60.1 2 Samuel 8.3 Genèse 15.18 2 Samuel 10.6 1 Samuel 14.47
4 Daudi akampokonya magari elfu, na wapanda farasi saba elfu, na askari waendao kwa miguu ishirini elfu; Daudi akawakata mshipa farasi wote wa magari, ila wa magari mia akawaweka.
2 Samuel 8.4 1 Rois 4.2 Psaumes 33.16-33.17 Josué 11.6 Josué 11.9
5 Na Washami wa Dameski walipokuja wamsaidie Hadadezeri, mfalme wa Soba, Daudi akapiga katika hao Washami watu ishirini na mbili elfu.
1 Chroniques 19.6 1 Samuel 14.47 2 Samuel 8.5-8.6 1 Rois 11.23-11.24 1 Chroniques 18.3
6 Ndipo Daudi akaweka ngome katika Shamu ya Dameski; nao Washami wakawa watumwa wa Daudi, wakaleta zawadi. Naye Bwana akampa Daudi kushinda kila alikokwenda.
Proverbes 21.31 1 Chroniques 18.2 1 Chroniques 17.8 Psaumes 121.8 Psaumes 18.43-18.44
7 Tena Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizovaliwa na watumishi wa Hadadezeri akazileta Yerusalemu.
1 Rois 14.26-14.28 2 Chroniques 12.9-12.10 2 Chroniques 9.15-9.16 1 Rois 10.16-10.17
8 Tena toka Tibhathi, na toka Berothai, miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi mno, aliyofanyizia Sulemani ile bahari ya shaba, na zile nguzo, na vile vyombo vya shaba.
2 Samuel 8.8 2 Chroniques 4.12-4.18 1 Chroniques 22.14 1 Rois 7.15-7.47 2 Chroniques 4.2-4.6
9 Hata aliposikia Tou, mfalme wa Hamathi, ya kuwa Daudi amewapiga jeshi lote la Hadadezeri, mfalme wa Soba,
2 Samuel 8.9
10 akampeleka mwanawe Hadoramu kwa mfalme Daudi, ili kumsalimia, na kumbarikia, kwa sababu alikuwa amepigana na Hadadezeri, na kumpiga; kwa maana Hadadezeri alikuwa amepigana vita juu ya Tou; naye akaleta vyombo vya dhahabu, na fedha, na shaba, vya namna zote.
2 Samuel 8.10 2 Chroniques 9.1 Esaïe 39.1 2 Chroniques 9.23-9.24
11 Hivi pia mfalme Daudi akavifanya wakfu kwa Bwana, pamoja na hiyo fedha na dhahabu, aliyoteka nyara kwa mataifa yote; kwa Edomu, na kwa Moabu, na kwa wana wa Amoni, na kwa Wafilisti, na kwa Amaleki.
Michée 4.13 2 Samuel 8.11-8.12 1 Chroniques 26.26-26.27 Exode 35.5 1 Samuel 30.20
12 Tena Abishai, mwana wa Seruya, akawapiga wa Waedomi katika Bonde la Chumvi watu kumi na nane elfu.
1 Samuel 26.6 1 Chroniques 11.20 2 Rois 14.7 2 Samuel 8.13-8.14 2 Samuel 7.13
13 Akaweka ngome katika Edomu; na Waedomi wote wakawa watumwa wa Daudi. Naye Bwana akampa Daudi kushinda, kila alikokwenda.
1 Chroniques 18.6 Nombres 24.18 Psaumes 18.48-18.50 1 Samuel 13.3 Genèse 25.23
14 Basi Daudi akatawala juu ya Israeli wote; akawafanyia hukumu na haki watu wake wote.
Jérémie 22.15 Jérémie 23.5-23.6 Psaumes 78.71-78.72 2 Samuel 8.15 Jérémie 33.15
15 Na Yoabu mwana wa Seruya akawa juu ya jeshi; na Yehoshafati mwana wa Ahiludi mwenye kuandika tarehe.
1 Chroniques 11.6 2 Samuel 8.16 1 Rois 4.3
16 Na Sadoki mwana wa Ahitubu, na Ahimeleki mwana wa Abiathari, walikuwa makuhani; na Shausha mwandishi;
2 Samuel 8.17 2 Samuel 20.25 1 Rois 4.3 1 Rois 2.35 1 Chroniques 24.6
17 na Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi; na wana wa Daudi walikuwa wakuu kumzunguka mfalme.
2 Samuel 8.18 2 Samuel 15.18 1 Rois 1.38 1 Rois 2.34-2.35 2 Samuel 20.23

Cette Bible est dans le domaine public.