Prospérité de David
 1 Ikawa baadaye, Daudi akawapiga Wafilisti, akawashinda, akautwaa Gathi na vijiji vyake mikononi mwa Wafilisti.
2 Samuel 8.1-8.18  1 Samuel 27.4  2 Samuel 1.20  1 Samuel 5.8  
 2 Akapiga Moabu; na hao Wamoabi wakawa watumwa wa Daudi wakaleta zawadi.
Esaïe 16.1  2 Rois 3.4-3.5  1 Rois 10.2  Psaumes 72.8-72.10  Esaïe 11.14  
 3 Tena Daudi akampiga Hadadezeri, mfalme wa Soba, mpaka Hamathi, alipokwenda kujisimamishia mamlaka yake kwenye mto wa Frati.
Psaumes 60.1  2 Samuel 8.3  Genèse 15.18  2 Samuel 10.6  1 Samuel 14.47  
 4 Daudi akampokonya magari elfu, na wapanda farasi saba elfu, na askari waendao kwa miguu ishirini elfu; Daudi akawakata mshipa farasi wote wa magari, ila wa magari mia akawaweka.
2 Samuel 8.4  1 Rois 4.2  Psaumes 33.16-33.17  Josué 11.6  Josué 11.9  
 5 Na Washami wa Dameski walipokuja wamsaidie Hadadezeri, mfalme wa Soba, Daudi akapiga katika hao Washami watu ishirini na mbili elfu.
1 Chroniques 19.6  1 Samuel 14.47  2 Samuel 8.5-8.6  1 Rois 11.23-11.24  1 Chroniques 18.3  
 6 Ndipo Daudi akaweka ngome katika Shamu ya Dameski; nao Washami wakawa watumwa wa Daudi, wakaleta zawadi. Naye Bwana akampa Daudi kushinda kila alikokwenda.
Proverbes 21.31  1 Chroniques 18.2  1 Chroniques 17.8  Psaumes 121.8  Psaumes 18.43-18.44  
 7 Tena Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizovaliwa na watumishi wa Hadadezeri akazileta Yerusalemu.
1 Rois 14.26-14.28  2 Chroniques 12.9-12.10  2 Chroniques 9.15-9.16  1 Rois 10.16-10.17  
 8 Tena toka Tibhathi, na toka Berothai, miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi mno, aliyofanyizia Sulemani ile bahari ya shaba, na zile nguzo, na vile vyombo vya shaba.
2 Samuel 8.8  2 Chroniques 4.12-4.18  1 Chroniques 22.14  1 Rois 7.15-7.47  2 Chroniques 4.2-4.6  
 9 Hata aliposikia Tou, mfalme wa Hamathi, ya kuwa Daudi amewapiga jeshi lote la Hadadezeri, mfalme wa Soba,
2 Samuel 8.9  
 10 akampeleka mwanawe Hadoramu kwa mfalme Daudi, ili kumsalimia, na kumbarikia, kwa sababu alikuwa amepigana na Hadadezeri, na kumpiga; kwa maana Hadadezeri alikuwa amepigana vita juu ya Tou; naye akaleta vyombo vya dhahabu, na fedha, na shaba, vya namna zote.
2 Samuel 8.10  2 Chroniques 9.1  Esaïe 39.1  2 Chroniques 9.23-9.24  
 11 Hivi pia mfalme Daudi akavifanya wakfu kwa Bwana, pamoja na hiyo fedha na dhahabu, aliyoteka nyara kwa mataifa yote; kwa Edomu, na kwa Moabu, na kwa wana wa Amoni, na kwa Wafilisti, na kwa Amaleki.
1 Chroniques 26.26-26.27  Exode 35.5  1 Samuel 30.20  1 Chroniques 20.1-20.2  Josué 6.19  
 12 Tena Abishai, mwana wa Seruya, akawapiga wa Waedomi katika Bonde la Chumvi watu kumi na nane elfu.
1 Samuel 26.6  2 Samuel 8.13-8.14  2 Samuel 7.13  1 Samuel 26.8  2 Samuel 23.18  
 13 Akaweka ngome katika Edomu; na Waedomi wote wakawa watumwa wa Daudi. Naye Bwana akampa Daudi kushinda, kila alikokwenda.
1 Chroniques 18.6  1 Samuel 13.3  Genèse 25.23  2 Samuel 7.14-7.17  Genèse 27.37  
 14 Basi Daudi akatawala juu ya Israeli wote; akawafanyia hukumu na haki watu wake wote.Jérémie 22.15  Jérémie 23.5-23.6  Psaumes 78.71-78.72  2 Samuel 8.15  Jérémie 33.15  
 15 Na Yoabu mwana wa Seruya akawa juu ya jeshi; na Yehoshafati mwana wa Ahiludi mwenye kuandika tarehe.
1 Chroniques 11.6  2 Samuel 8.16  1 Rois 4.3  
 16 Na Sadoki mwana wa Ahitubu, na Ahimeleki mwana wa Abiathari, walikuwa makuhani; na Shausha mwandishi;
2 Samuel 8.17  2 Samuel 20.25  1 Rois 4.3  1 Rois 2.35  1 Chroniques 24.6  
 17 na Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi; na wana wa Daudi walikuwa wakuu kumzunguka mfalme.
2 Samuel 8.18  2 Samuel 15.18  1 Rois 1.38  1 Rois 2.34-2.35  2 Samuel 20.23