Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 17
Bible en Swahili de l’est


Une maison pour Dieu et pour David

1 Ikawa, Daudi alipokuwa akikaa nyumbani mwake, Daudi akamwambia nabii Nathani, Angalia, mimi ninakaa katika nyumba ya mwerezi, bali sanduku la agano la Bwana linakaa chini ya mapazia.
1 Chroniques 15.1 1 Chroniques 17.5 Exode 40.19-40.21 1 Chroniques 29.29 1 Rois 1.23
2 Naye Nathani akamwambia Daudi, Haya, fanya yote yaliyomo moyoni mwako; kwa maana Mungu yu pamoja nawe.
1 Corinthiens 13.9 1 Chroniques 22.7 1 Samuel 16.7 Zacharie 8.23 1 Samuel 10.7
3 Ikawa usiku uo huo, neno la Mungu likamjia Nathani, kusema,
2 Rois 20.1-20.5 Amos 3.7 Esaïe 30.21 Nombres 12.6
4 Nenda, kamwambie mtumishi wangu, Daudi, Bwana asema hivi, Wewe hutanijengea nyumba ya kukaa;
1 Chroniques 28.2-28.3 2 Chroniques 6.8-6.9 2 Samuel 7.4-7.5 Esaïe 55.8-55.9 Romains 11.33-11.34
5 kwa maana sikukaa ndani ya nyumba tangu siku ile nilipowaleta Israeli huku hata leo; lakini hema kwa hema nimehamia, na maskani kwa maskani.
2 Samuel 7.6 Exode 40.2-40.3 2 Chroniques 6.18 Actes 7.44-7.50 1 Rois 8.27
6 Katika mahali mwote nilimokwenda na Israeli wote, je! Nimesema neno lo lote na mtu ye yote wa waamuzi wa Israeli, niliowaagiza kuwalisha watu wangu, nikisema, Mbona hamkunijengea nyumba ya mwerezi?
2 Samuel 7.7 Psaumes 78.71-78.72 Lévitique 26.11-26.12 Jérémie 23.4 Juges 2.16-2.18
7 Basi sasa ndivyo utakavyomwambia mtumishi wangu Daudi, Bwana wa majeshi asema hivi, Nalikutwaa katika zizi la kondoo, katika kuwaandama kondoo ili uwe mkuu juu ya watu wangu Israeli;
2 Samuel 6.21 1 Samuel 17.15 Matthieu 2.6 2 Samuel 7.8 Amos 7.14-7.15
8 nami nimekuwa pamoja nawe kila ulikokwenda, na kuwakatilia mbali adui zako wote mbele yako; nami nitakufanyia jina, kama jina la hao wakuu walioko duniani.
Esdras 4.20 1 Chroniques 17.2 1 Samuel 18.28 1 Samuel 26.10 Genèse 28.15
9 Tena nitawaagizia watu wangu Israeli mahali, nami nitawapanda, wapate kukaa mahali pao wenyewe, wasiondolewe tena; wala wana wa uovu hawatawatesa tena kama hapo kwanza,
Psaumes 92.13 Amos 9.15 Ephésiens 5.6 Jérémie 31.3-31.12 Esaïe 61.3
10 na tangu siku ile nilipowaamuru waamuzi wawe juu ya watu wangu Israeli, nami nitawashinda adui zako wote. Pamoja na hayo nakuambia, ya kwamba Bwana atakujengea nyumba.
2 Samuel 7.11 Juges 2.14-2.18 Psaumes 89.23 Psaumes 18.40-18.50 1 Corinthiens 15.25
11 Hata itakuwa, siku zako zitakapotimia, uende na babazo, nitainua mzao wako nyuma yako, atakayekuwa wa wana wako; nami nitaufanya imara ufalme wake.
Psaumes 132.11 Actes 13.36 2 Samuel 12.24-12.25 1 Chroniques 29.15 1 Chroniques 28.5
12 Yeye ndiye atakayenijengea nyumba, nami nitakifanya imara kiti cha enzi cha ufalme wake milele.
Daniel 2.44 Esaïe 9.7 1 Rois 5.5 Psaumes 89.29 Psaumes 89.4
13 Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu; wala sitamwondolea fadhili zangu, kama nilivyomwondolea yeye aliyekuwa kabla yako;
Hébreux 1.5 Esaïe 55.3 1 Chroniques 17.12 1 Chroniques 10.14 1 Samuel 15.28
14 ila nitamstarehesha katika nyumba yangu na katika ufalme wangu milele; na kiti chake cha enzi kitathibitishwa milele.
Psaumes 72.17 Psaumes 2.6 Luc 1.32-1.33 Hébreux 3.6 Psaumes 89.36
15 Kwa maneno hayo yote, na kwa maono hayo yote, ndivyo Nathani alivyonena na Daudi.
Actes 20.27 Jérémie 23.28 2 Samuel 7.17
16 Ndipo akaingia Daudi mfalme, akaketi mbele za Bwana; akasema Mimi ni nani, Ee Bwana Mungu, na nyumba yangu ni nini, hata umenileta hata hapa?
2 Samuel 7.18 Genèse 32.10 2 Corinthiens 1.10 Ephésiens 3.8 1 Samuel 9.21
17 Tena jambo hili lilikuwa dogo machoni pako, Ee Mungu; hata umeleta habari ya nyumba yangu mimi, mtumwa wako, kwa miaka mingi inayokuja, nawe umeniangalia sawasawa na hali ya mtu mwenye cheo, Ee Bwana Mungu.
2 Samuel 12.8 1 Chroniques 17.11-17.15 Ephésiens 3.20 1 Rois 3.13 Philippiens 2.8-2.11
18 Na Daudi akuambie nini tena zaidi kwa habari ya heshima aliyotendewa mtumwa wako? Kwa maana wewe umemjua mtumwa wako.
Psaumes 139.1 Apocalypse 2.23 1 Samuel 16.7 Jean 21.17 1 Samuel 2.30
19 Ee Bwana, kwa ajili ya mtumwa wako, na kwa moyo wako mwenyewe, umeyatenda hayo makuu yote, ili yajulikane hayo matendo makuu yote.
Esaïe 37.35 Esaïe 42.1 Psaumes 111.3 1 Chroniques 29.11-29.12 Esaïe 49.5-49.6
20 Ee Bwana, hakuna mwingine kama wewe, wala hakuna Mungu mwingine ila wewe, kwa kadiri tulivyosikia kwa masikio yetu.
Exode 15.11 Esaïe 44.6 Psaumes 89.6 Exode 18.11 Esaïe 43.10
21 Tena ni taifa lipi duniani lililo kama watu wako Israeli, ambalo Mungu alikwenda kuwakomboa kwa ajili yake mwenyewe, ili wawe watu wake, na kujifanyia jina kwa njia ya mambo makuu, yenye kuogofya, kwa kufukuza mataifa mbele ya watu wako, uliowakomboa kutoka Misri?
Ezéchiel 20.9-20.10 Josué 21.43-21.45 Deutéronome 15.15 Psaumes 65.5 Deutéronome 4.7
22 Kwa maana watu wako Israeli ndio uliowafanya kuwa watu wako wa milele; nawe, Bwana, umekuwa Mungu wao.
Exode 19.5-19.6 Romains 11.1-11.12 Jérémie 31.31-31.34 Romains 9.4-9.6 Zacharie 13.9
23 Basi sasa, Ee Bwana, neno lile ulilolinena katika habari za mtumwa wako, na katika habari za nyumba yake, na lifanywe imara milele, ukafanye kama ulivyosema.
Psaumes 119.49 Jérémie 11.5 Luc 1.38 Genèse 32.12 2 Samuel 7.25-7.29
24 Jina lako na liwe imara, likatukuzwe milele, kusema, Bwana wa majeshi ndiye Mungu wa Israeli, naam, Mungu juu ya Israeli; na hiyo nyumba ya Daudi mtumwa wako imefanywa imara mbele zako.
Psaumes 21.13 Matthieu 6.13 Jérémie 31.1 Apocalypse 21.3 Hébreux 11.16
25 Kwa kuwa wewe, Ee Mungu wangu, umenifunulia mimi mtumwa wako ya kuwa utanijengea nyumba; kwa hiyo mimi mtumwa wako nimeona vema moyoni mwangu kuomba mbele yako.
Psaumes 10.17 1 Samuel 9.15 Ezéchiel 36.37 1 Jean 5.14-5.15
26 Na sasa, Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu, nawe umemwahidia mtumwa wako jambo hili jema;
Hébreux 6.18 Tite 1.2 Exode 34.6-34.7
27 nawe sasa umekuwa radhi kuibarikia nyumba ya mtumwa wako, ipate kudumu milele mbele zako; kwa maana wewe, Bwana, umebarikia, nayo imebarikiwa milele.
Ephésiens 1.3 Genèse 27.33 Romains 11.29 Psaumes 72.17

Cette Bible est dans le domaine public.