Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 17.14
Bible en Swahili de l’est


Une maison pour Dieu et pour David

1 Ikawa, Daudi alipokuwa akikaa nyumbani mwake, Daudi akamwambia nabii Nathani, Angalia, mimi ninakaa katika nyumba ya mwerezi, bali sanduku la agano la Bwana linakaa chini ya mapazia.
1 Chroniques 15.1 1 Chroniques 17.5 2 Chroniques 1.4 Daniel 4.4 2 Chroniques 6.7-6.9
2 Naye Nathani akamwambia Daudi, Haya, fanya yote yaliyomo moyoni mwako; kwa maana Mungu yu pamoja nawe.
2 Samuel 7.3 Luc 1.28 Josué 9.14 1 Chroniques 28.2 1 Corinthiens 13.9
3 Ikawa usiku uo huo, neno la Mungu likamjia Nathani, kusema,
Esaïe 30.21 Nombres 12.6 2 Rois 20.1-20.5 Amos 3.7
4 Nenda, kamwambie mtumishi wangu, Daudi, Bwana asema hivi, Wewe hutanijengea nyumba ya kukaa;
1 Chroniques 28.2-28.3 Esaïe 55.8-55.9 Romains 11.33-11.34 1 Rois 8.19 1 Chroniques 22.7-22.8
5 kwa maana sikukaa ndani ya nyumba tangu siku ile nilipowaleta Israeli huku hata leo; lakini hema kwa hema nimehamia, na maskani kwa maskani.
2 Samuel 7.6 Exode 40.2-40.3 1 Rois 8.16 2 Samuel 6.17 2 Chroniques 2.6
6 Katika mahali mwote nilimokwenda na Israeli wote, je! Nimesema neno lo lote na mtu ye yote wa waamuzi wa Israeli, niliowaagiza kuwalisha watu wangu, nikisema, Mbona hamkunijengea nyumba ya mwerezi?
2 Samuel 7.7 Michée 5.4 Exode 33.14-33.15 Nombres 10.33-10.36 1 Samuel 12.11
7 Basi sasa ndivyo utakavyomwambia mtumishi wangu Daudi, Bwana wa majeshi asema hivi, Nalikutwaa katika zizi la kondoo, katika kuwaandama kondoo ili uwe mkuu juu ya watu wangu Israeli;
2 Samuel 6.21 Exode 3.1-3.10 1 Samuel 16.11-16.12 Luc 5.10 Matthieu 4.18-4.22
8 nami nimekuwa pamoja nawe kila ulikokwenda, na kuwakatilia mbali adui zako wote mbele yako; nami nitakufanyia jina, kama jina la hao wakuu walioko duniani.
2 Samuel 22.38-22.41 1 Samuel 18.14 2 Samuel 8.13-8.14 2 Samuel 22.1 2 Samuel 8.6
9 Tena nitawaagizia watu wangu Israeli mahali, nami nitawapanda, wapate kukaa mahali pao wenyewe, wasiondolewe tena; wala wana wa uovu hawatawatesa tena kama hapo kwanza,
Ephésiens 2.2-2.3 Jérémie 32.41 Ezéchiel 28.4 Exode 2.23 Apocalypse 21.4
10 na tangu siku ile nilipowaamuru waamuzi wawe juu ya watu wangu Israeli, nami nitawashinda adui zako wote. Pamoja na hayo nakuambia, ya kwamba Bwana atakujengea nyumba.
2 Samuel 7.11 Juges 2.14-2.18 Juges 4.3 Psaumes 21.8-21.9 Juges 3.8
11 Hata itakuwa, siku zako zitakapotimia, uende na babazo, nitainua mzao wako nyuma yako, atakayekuwa wa wana wako; nami nitaufanya imara ufalme wake.
Psaumes 132.11 1 Chroniques 29.28 Actes 2.29 Deutéronome 31.16 1 Rois 8.20
12 Yeye ndiye atakayenijengea nyumba, nami nitakifanya imara kiti cha enzi cha ufalme wake milele.
1 Rois 5.5 Daniel 2.44 Esaïe 9.7 Colossiens 2.9 Jean 2.19-2.21
13 Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu; wala sitamwondolea fadhili zangu, kama nilivyomwondolea yeye aliyekuwa kabla yako;
Hébreux 1.5 Psaumes 2.7 Esaïe 55.3 1 Chroniques 17.12 1 Chroniques 10.14
14 ila nitamstarehesha katika nyumba yangu na katika ufalme wangu milele; na kiti chake cha enzi kitathibitishwa milele.
Luc 1.32-1.33 Hébreux 3.6 Psaumes 89.36 Psaumes 72.17 Psaumes 2.6
15 Kwa maneno hayo yote, na kwa maono hayo yote, ndivyo Nathani alivyonena na Daudi.
2 Samuel 7.17 Actes 20.27 Jérémie 23.28
16 Ndipo akaingia Daudi mfalme, akaketi mbele za Bwana; akasema Mimi ni nani, Ee Bwana Mungu, na nyumba yangu ni nini, hata umenileta hata hapa?
Genèse 32.10 2 Samuel 7.18 1 Samuel 7.12 Genèse 48.15-48.16 Actes 26.22
17 Tena jambo hili lilikuwa dogo machoni pako, Ee Mungu; hata umeleta habari ya nyumba yangu mimi, mtumwa wako, kwa miaka mingi inayokuja, nawe umeniangalia sawasawa na hali ya mtu mwenye cheo, Ee Bwana Mungu.
2 Samuel 7.19 1 Chroniques 17.7-17.8 Psaumes 78.70-78.72 Esaïe 49.6 2 Samuel 12.8
18 Na Daudi akuambie nini tena zaidi kwa habari ya heshima aliyotendewa mtumwa wako? Kwa maana wewe umemjua mtumwa wako.
1 Samuel 16.7 Jean 21.17 1 Samuel 2.30 2 Samuel 7.20-7.24 Psaumes 139.1
19 Ee Bwana, kwa ajili ya mtumwa wako, na kwa moyo wako mwenyewe, umeyatenda hayo makuu yote, ili yajulikane hayo matendo makuu yote.
Esaïe 37.35 Psaumes 111.6 Esaïe 49.3 Daniel 9.17 Esaïe 42.1
20 Ee Bwana, hakuna mwingine kama wewe, wala hakuna Mungu mwingine ila wewe, kwa kadiri tulivyosikia kwa masikio yetu.
Exode 15.11 Esaïe 44.6 Ephésiens 3.20 Esaïe 40.25 Deutéronome 3.24
21 Tena ni taifa lipi duniani lililo kama watu wako Israeli, ambalo Mungu alikwenda kuwakomboa kwa ajili yake mwenyewe, ili wawe watu wake, na kujifanyia jina kwa njia ya mambo makuu, yenye kuogofya, kwa kufukuza mataifa mbele ya watu wako, uliowakomboa kutoka Misri?
Ezéchiel 20.9-20.10 Deutéronome 33.26-33.29 Josué 24.11-24.12 Psaumes 44.2-44.3 Psaumes 114.3-114.8
22 Kwa maana watu wako Israeli ndio uliowafanya kuwa watu wako wa milele; nawe, Bwana, umekuwa Mungu wao.
Exode 19.5-19.6 Romains 9.25-9.26 1 Pierre 2.9 Deutéronome 7.6-7.8 1 Samuel 12.22
23 Basi sasa, Ee Bwana, neno lile ulilolinena katika habari za mtumwa wako, na katika habari za nyumba yake, na lifanywe imara milele, ukafanye kama ulivyosema.
Jérémie 11.5 Luc 1.38 Psaumes 119.49 2 Samuel 7.25-7.29 Genèse 32.12
24 Jina lako na liwe imara, likatukuzwe milele, kusema, Bwana wa majeshi ndiye Mungu wa Israeli, naam, Mungu juu ya Israeli; na hiyo nyumba ya Daudi mtumwa wako imefanywa imara mbele zako.
Hébreux 8.10 Jean 12.28 1 Pierre 4.11 Matthieu 6.9 Psaumes 21.13
25 Kwa kuwa wewe, Ee Mungu wangu, umenifunulia mimi mtumwa wako ya kuwa utanijengea nyumba; kwa hiyo mimi mtumwa wako nimeona vema moyoni mwangu kuomba mbele yako.
Ezéchiel 36.37 1 Jean 5.14-5.15 Psaumes 10.17 1 Samuel 9.15
26 Na sasa, Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu, nawe umemwahidia mtumwa wako jambo hili jema;
Exode 34.6-34.7 Hébreux 6.18 Tite 1.2
27 nawe sasa umekuwa radhi kuibarikia nyumba ya mtumwa wako, ipate kudumu milele mbele zako; kwa maana wewe, Bwana, umebarikia, nayo imebarikiwa milele.
Romains 11.29 Psaumes 72.17 Ephésiens 1.3 Genèse 27.33

Cette Bible est dans le domaine public.