Prospérité et victoires de David
 1 Naye Hiramu, mfalme wa Tiro, akatuma wajumbe kwa Daudi, akampelekea na mierezi, na waashi, na maseremala, ili wamjengee nyumba.
Esdras 3.7  2 Chroniques 2.3  2 Samuel 5.11-5.16  1 Rois 5.18  2 Chroniques 2.8-2.12  
 2 Daudi akajua ya kwamba Bwana amemweka imara ili amiliki juu ya Israeli, kwa kuwa milki yake imeinuka kwa ajili ya watu wake Israeli.
Nombres 24.7  2 Samuel 7.8  Esaïe 1.25-1.27  1 Rois 10.9  Psaumes 89.20-89.37  
 3 Tena Daudi akazidi kuoa wake huko Yerusalemu; akazidi Daudi kuzaa wana na binti.
Deutéronome 17.17  1 Chroniques 3.1-3.4  Ecclésiaste 9.9  Proverbes 5.18-5.19  2 Samuel 5.13  
 4 Na haya ndiyo majina ya watoto aliozaliwa huko Yerusalemu; Shamua, na Shobabu, na Nathani, na Sulemani;
1 Chroniques 3.5-3.9  2 Samuel 12.1  1 Chroniques 22.9-22.12  2 Samuel 5.14  1 Chroniques 28.5-28.6  
 5 na Ibhari, na Elishua, na Elpeleti;
1 Chroniques 3.6  2 Samuel 5.15  
 6 na Noga, na Nefegi, na Yafia; 
7 na Elishama, na Eliada, na Elifeleti.
2 Samuel 5.16  1 Chroniques 3.8  
 8 Na waliposikia hao Wafilisti ya kwamba Daudi ametiwa mafuta ili awe mfalme juu ya Israeli wote, Wafilisti wote wakapanda kumtafuta Daudi; naye Daudi akasikia, akatoka nje kupigana nao.
2 Samuel 5.3  Apocalypse 11.15-11.18  2 Samuel 5.17-5.25  Psaumes 2.1-2.6  1 Chroniques 11.3  
 9 Basi hao Wafilisti walikuwa wamekuja na kuteka nyara katika bonde la Warefai.
1 Chroniques 11.15  1 Chroniques 14.13  2 Samuel 5.18  2 Samuel 23.13  Esaïe 17.5  
 10 Daudi akamwuliza Mungu, kusema, Je! Nipande juu ya Wafilisti! Utawatia mikononi mwangu? Naye Bwana akamwambia, Panda; kwa kuwa nitawatia mikononi mwako.
Proverbes 3.6  1 Rois 22.15-22.17  Juges 4.6-4.7  1 Chroniques 13.3  1 Chroniques 14.14  
 11 Basi wakapanda mpaka Baal-perasimu, Daudi naye akawapiga huko; Daudi akasema, Bwana amewafurikia adui zangu kwa mkono wangu, kama mafuriko ya maji. Basi wakapaita mahali pale jina lake Baal-perasimu.
Esaïe 28.21  2 Samuel 5.20  Psaumes 144.1  Exode 14.28  Psaumes 18.13-18.15  
 12 Nao wakaiacha miungu yao huko; naye Daudi akaamuru, ikateketezwa kwa moto.
Exode 32.20  Exode 12.12  Deutéronome 7.5  Deutéronome 7.25  1 Samuel 5.2-5.6  
 13 Lakini hao Wafilisti wakateka nyara tena mara ya pili bondeni.
1 Chroniques 14.9  2 Samuel 5.22-5.25  1 Rois 20.22  
 14 Na Daudi akamwuliza Mungu tena; naye Mungu akamwambia, Hutapanda kuwafuata; uwageukie mbali, ukawajie huko kuielekea miforsadi.Psaumes 27.4  Jean 9.6-9.7  1 Chroniques 14.10  Josué 8.2-8.7  
 15 Kisha itakuwa utakapoisikia sauti ya kwenda katika vilele vya miforsadi, ndipo utakapokwenda nje vitani; kwa maana ndipo Mungu ametoka mbele yako, awapige jeshi la Wafilisti.
Lévitique 26.36  2 Rois 19.7  Juges 7.9  Michée 2.12-2.13  Philippiens 2.12-2.13  
 16 Daudi akafanya kama vile Mungu alivyomwamuru; wakawapiga jeshi la Wafilisti toka Geba mpaka Gezeri.
Jean 2.5  Exode 39.42-39.43  Jean 13.17  2 Samuel 5.25  Jean 15.14  
 17 Sifa za Daudi zikafika nchi zote; naye Bwana akawaletea mataifa yote hofu yake.
Deutéronome 2.25  Exode 15.14-15.16  2 Chroniques 26.8  Josué 6.27  Josué 2.9-2.11