Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 8.18
Bible en Swahili de l’est


Famine annoncée par Élisée

1 Basi Elisha alikuwa amemwambia yule mwanamke, ambaye alimfufulia mwanawe, akasema, Ondoka, ukaende wewe na jamaa yako, ukae hali ya kigeni utakakoweza kukaa; kwa sababu Bwana ameiita njaa; nayo itakuja juu ya nchi hii muda wa miaka saba.
2 Rois 4.31-4.35 Psaumes 105.16 Aggée 1.11 2 Rois 4.18 Genèse 12.10
2 Akaondoka yule mwanamke, akafanya kama alivyosema mtu wa Mungu; akaenda, yeye na jamaa yake, akakaa katika nchi ya Wafilisti miaka saba.
1 Timothée 5.8 Juges 3.3 1 Samuel 27.1-27.3
3 Ikawa miaka saba ilipoisha, yule mwanamke akarudi kutoka nchi ya Wafilisti; akatokea amlilie mfalme kwa ajili ya nyumba yake na shamba lake.
2 Rois 6.26 Psaumes 82.3-82.4 Jérémie 22.16 2 Rois 4.13 2 Rois 8.6
4 Basi mfalme alikuwa akizungumza na Gehazi, mtumishi wa mtu wa Mungu, akinena, Uniambie, nakusihi, mambo makuu yote aliyoyafanya Elisha.
2 Rois 5.20-5.27 2 Rois 6.17-6.20 2 Rois 7.16-7.20 Jean 9.27 2 Rois 4.16-4.17
5 Ikawa, alipokuwa katika kumwambia mfalme jinsi alivyomfufua mtu aliyekufa, tazama, huyo mwanamke aliyemfufulia mwanawe, alimlilia mfalme kwa ajili ya nyumba yake na shamba lake. Gehazi akasema, Bwana wangu mfalme, huyu ndiye mwanamke, na huyu ndiye mwanawe, ambaye Elisha alimfufua.
2 Rois 4.35 Esther 5.14 Psaumes 145.1 2 Rois 6.12 1 Samuel 26.17
6 Na mfalme alipomwuliza yule mwanamke, yeye akamweleza. Basi mfalme akamtolea akida, akasema, Mrudishie yote aliyokuwa nayo, na mapato yote ya shamba lake tangu siku aliposafiri, hata leo.
Proverbes 16.7 Genèse 37.36 2 Rois 9.32 Juges 11.13 Deutéronome 22.2

Annonce du règne d’Hazaël sur la Syrie

7 Kisha, Elisha akaenda Dameski; na Ben-hadadi, mfalme wa Shamu, alikuwa hawezi; akaambiwa ya kwamba, Yule mtu wa Mungu amefika hapa.
1 Rois 11.24 2 Rois 6.24 1 Rois 20.1 Deutéronome 33.1 Genèse 14.15
8 Mfalme akamwambia Hazaeli, Chukua zawadi mkononi mwako, ukaende ili kumlaki yule mtu wa Mungu, ukamwulize Bwana kwa kinywa chake, kusema, Je! Nitapona ugonjwa huu?
1 Rois 19.15 2 Rois 1.2 1 Samuel 9.7 2 Rois 1.6 2 Rois 3.11-3.13
9 Basi Hazaeli akaenda kumlaki, akachukua zawadi mkononi mwake, za kila kitu chema kilichopatikana Dameski, kiasi cha mizigo ya ngamia arobaini, akaenda, akasimama mbele yake akasema, Mwana wako Ben-hadadi, mfalme wa Shamu, amenituma kwako, kusema, Je nitapona ugonjwa huu?
1 Rois 19.15 2 Rois 5.13 2 Rois 13.14 2 Rois 5.5 2 Rois 6.21
10 Elisha akamwambia, Enenda, ukamwambie, Bila shaka utapona; lakini Bwana amenionyesha ya kwamba bila shaka atakufa.
Amos 8.1 Apocalypse 22.1 Jérémie 38.21 Genèse 2.17 1 Rois 22.15
11 Akamkazia macho hata akatahayari; na yule mtu wa Mungu akalia machozi.
Luc 19.41 Actes 20.19 Psaumes 119.136 Romains 9.2 Actes 20.31
12 Hazaeli akasema, Bwana wangu analilia nini? Akajibu, Kwa sababu nayajua mabaya utakayowatenda wana wa Israeli; utazichoma moto ngome zao, utawaua vijana wao kwa upanga, utawaseta-seta watoto wao wachanga na wanawake wao wenye mimba utawapasua.
Osée 13.16 Nahum 3.10 2 Rois 12.17 2 Rois 13.3 2 Rois 15.16
13 Hazaeli akasema, Lakini mimi mtumwa wako ni nani, mimi niliye mbwa tu, hata nifanye jambo hili kubwa? Elisha akajibu, Bwana amenionyesha ya kwamba wewe utakuwa mfalme juu ya Shamu.
1 Rois 19.15 1 Samuel 17.43 2 Samuel 9.8 2 Rois 8.10 Michée 2.1
14 Ndipo akamwacha Elisha, akarudi kwa bwana wake; naye akamwambia, Elisha alikuambiaje? Akajibu, Aliniambia ya kuwa bila shaka utapona.
2 Rois 8.10 Matthieu 26.16 2 Rois 5.25
15 Ikawa siku ya pili yake, akatwaa tandiko la kitanda, akalichovya katika maji, akalitandaza juu ya uso wake, hata akafa. Na Hazaeli akatawala badala yake.
2 Rois 8.13 Psaumes 36.4 2 Rois 15.25 1 Samuel 26.9-26.11 2 Rois 15.30

Règne de Joram sur Juda

16 Katika mwaka wa tano wa Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, [Yehoshafati alipokuwa mfalme wa Yuda], alianza kutawala Yehoramu mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda.
2 Rois 1.17 2 Rois 3.1 1 Rois 22.50 2 Chroniques 21.1-21.20
17 Alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipoanza kutawala, akatawala miaka minane huko Yerusalemu.
2 Chroniques 21.5-21.10
18 Akaiendea njia ya wafalme wa Israeli kama walivyofanya nyumba ya Ahabu; kwa kuwa alikuwa amemwoa binti Ahabu; akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana.
2 Rois 8.26 2 Chroniques 21.6 Michée 6.16 2 Rois 9.7-9.8 Néhémie 13.25-13.26
19 Walakini Bwana hakupenda kuiharibu Yuda, kwa ajili ya Daudi mtumishi wake, kama alivyomwahidia akasema, kuwa atampa taa, yeye na wazao wake siku zote.
1 Rois 11.36 2 Samuel 7.12-7.13 2 Samuel 7.15 Luc 1.32-1.33 1 Rois 15.4-15.5
20 Zamani zake, Edomu wakaasi mkononi mwa Yuda, wakajifanyia mfalme.
1 Rois 22.47 2 Rois 3.9 2 Rois 8.22 2 Rois 3.27 2 Samuel 8.14
21 Basi akaenda Yehoramu mpaka Sairi, na magari yake yote pamoja naye. Akaondoka usiku, akawapiga Waedomi waliomzunguka yeye na maakida wa magari; na watu wakakimbilia hemani kwao.
2 Samuel 18.17
22 Hivyo Edomu wakaasi mkononi mwa Yuda hata leo. Na Libna wakaasi zamani zizo hizo.
Josué 21.13 2 Rois 19.8 Genèse 27.40 2 Chroniques 21.10
23 Na mambo yote ya Yehoramu yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Yuda?
1 Rois 14.29 1 Rois 11.41 2 Rois 15.6 2 Chroniques 21.11-21.20 1 Rois 15.23
24 Akalala Yehoramu na baba zake, akazikwa pamoja na baba zake mjini mwa Daudi; na Ahazia mwanawe akatawala mahali pake.
2 Chroniques 21.1 2 Chroniques 21.17 2 Chroniques 22.6 2 Chroniques 25.23 1 Rois 11.43

Règne d’Achazia sur Juda

25 Katika mwaka wa kumi na mbili wa Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda alianza kutawala.
2 Rois 9.29 2 Rois 8.16-8.17 2 Chroniques 21.20-22.6
26 Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala; akatawala mwaka mmoja huko Yerusalemu. Na jina la mamaye aliitwa Athalia binti Omri mfalme wa Israeli.
2 Chroniques 22.2 2 Chroniques 22.5-22.8 2 Rois 9.21-9.27 2 Rois 11.13-11.16 2 Rois 11.1
27 Akaiendea njia ya nyumba ya Ahabu, akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, kama walivyofanya nyumba ya Ahabu, kwa kuwa alikuwa mkwe wa jamaa ya Ahabu.
2 Rois 8.18 2 Corinthiens 6.14-6.17 Ecclésiaste 7.26 2 Chroniques 22.3-22.4
28 Akaenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu ili kupigana na Hazaeli mfalme wa Shamu, huko Ramoth-gileadi; nao Washami wakamtia Yoramu jeraha.
2 Chroniques 22.5 2 Rois 8.15 2 Chroniques 18.31 2 Rois 9.15 1 Rois 22.3-22.4
29 Akarudi Yoramu mfalme, auguzwe katika Yezreeli jeraha walizotia Washami huko Rama alipopigana na Hazaeli mfalme wa Shamu. Naye Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akashuka amtazame Yoramu mwana wa Ahabu huko Yezreeli, kwa sababu alikuwa hawezi.
2 Rois 9.15-9.16 1 Rois 22.34 2 Rois 8.28 2 Chroniques 22.5-22.7

Cette Bible est dans le domaine public.