Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 24.15
Bible en Swahili de l’est


1 Katika siku zake akakwea Nebukadreza, mfalme wa Babeli na Yehoyakimu akawa mtumishi wake muda wa miaka mitatu;kisha ,akageuka,akamwasi.
Jérémie 25.1 Daniel 1.1 Jérémie 25.9 2 Chroniques 36.6-36.21 Jérémie 46.2
2 Naye Bwana akatuma juu yake vikosi vya Wakaldayo, na vikosi vya Washami, na vikosi vya Wamoabi, na vikosi vya wana wa Amoni, akawatuma juu ya Yuda ili kuiharibu, sawasawa na neno la Bwana alilolinena kwa mkono wa watumishi wake manabii.
Jérémie 35.11 2 Rois 23.27 Jérémie 25.9 2 Rois 6.23 Ezéchiel 19.8
3 Hakika kwa amri ya Bwana mambo hayo yalimpata Yuda, ili waondoshwe kutoka machoni pake, kwa sababu ya dhambi zake Manase, kadiri ya yote aliyoyafanya;
2 Rois 18.25 Jérémie 15.1-15.4 Deutéronome 28.63 Esaïe 45.7 Amos 3.6
4 tena kwa ajili ya damu zisizo na hatia alizozimwaga; kwani aliujaza Yerusalemu damu zisizo na hatia; wala Bwana hakukubali kusamehe.
2 Rois 21.16 Psaumes 106.38 Jérémie 19.4 Deutéronome 19.10 Nombres 35.33
5 Basi mambo yote ya Yehoyakimu yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Yuda?
2 Chroniques 36.8 Jérémie 26.1-26.24 Jérémie 22.13-22.17
6 Yehoyakimu akalala na babaze; na mwanawe Yekonia akatawala mahali pake.
Jérémie 22.18-22.19 2 Chroniques 36.6 Jérémie 36.30 2 Chroniques 36.8
7 Basi mfalme wa Misri hakuja tena kutoka nchi yake; kwa kuwa mfalme wa Babeli alikuwa amemnyang’anya nchi, tangu kijito cha Misri mpaka mto wa Frati, yote aliyokuwa nayo mfalme wa Misri.
Jérémie 37.5-37.7 Jérémie 46.2 Genèse 15.18 Nombres 34.5 1 Rois 4.21

Règne de Jojakin sur Juda

8 Yekonia alikuwa na umri wa miaka kumi na minane alipoanza kutawala; akatawala miezi mitatu katika Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Nehushta binti Elnathani wa Yerusalemu.
2 Chroniques 36.9 1 Chroniques 3.16 Jérémie 24.1 Jérémie 22.28 Jérémie 37.1
9 Akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, mfano wa yote aliyoyafanya baba yake.
10 Wakati ule watumishi wa Nebukadreza mfalme wa Babeli wakakwea kwenda Yerusalemu, na mji ukahusuriwa.
2 Rois 25.2 Daniel 1.1-1.2
11 Na Nebukadreza, mfalme wa Babeli, akaufikilia huo mji, hapo watumishi wake walipokuwa wakiuhusuru.
12 Na Yekonia, mfalme wa Yuda, akatoka akamwendea mfalme wa Babeli, yeye na mama yake, na watumishi wake, na wakuu wa watu wake, na maakida wake; mfalme wa Babeli akamchukua mateka katika mwaka wa nane wa kutawala kwake.
Jérémie 52.28 Jérémie 24.1 2 Chroniques 36.10 Jérémie 29.1-29.2 2 Rois 25.27
13 Akatoa huko hazina zote za nyumba ya Bwana, na hazina za nyumba ya mfalme, akavikata-kata vyombo vyote vya dhahabu ambavyo Sulemani, mfalme wa Israeli, alivifanya katika hekalu la Bwana, kama Bwana alivyosema.
2 Rois 20.17 Esaïe 39.6 1 Rois 7.48-7.50 Jérémie 20.5 Daniel 5.2-5.3
14 Akawachukua mateka watu wa Yerusalemu wote pia, na wakuu wote, na mashujaa wote, watu elfu kumi; na mafundi wote, na wafua chuma wote; hapana mtu aliyebaki, ila waliokuwa wanyonge wa watu wa nchi.
2 Rois 25.12 Jérémie 52.28 Jérémie 40.7 Ezéchiel 1.1-1.2 Ezéchiel 17.14
15 Akamchukua Yekonia mpaka Babeli; na mama yake mfalme, na wake zake mfalme, na maakida wake, na wakuu wa nchi, aliwachukua mateka toka Yerusalemu mpaka Babeli.
2 Chroniques 36.10 Jérémie 22.24-22.28 Esther 2.6 Ezéchiel 17.12 2 Rois 24.8
16 Na mashujaa wote, watu elfu saba, na mafundi na wafua chuma elfu moja, wote pia wenye nguvu, tayari kwa vita, hao wote mfalme wa Babeli aliwachukua mateka mpaka Babeli.
Jérémie 52.28 2 Rois 24.14 Jérémie 29.2
17 Mfalme wa Babeli akamtawaza Matania, ndugu ya baba yake, awe mfalme badala yake, akalibadili jina lake, akamwita Sedekia.
Jérémie 37.1 2 Chroniques 36.4 2 Rois 23.34 1 Chroniques 3.15-3.16 Jérémie 52.1

Règne de Sédécias sur Juda

18 Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala; akatawala miaka kumi na mmoja katika Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Hamutali, binti Yeremia wa Libna.
2 Rois 23.31 Jérémie 52.1-52.11 2 Chroniques 36.11 Jérémie 37.1
19 Akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, sawasawa na yote aliyoyafanya Yehoyakimu.
2 Rois 23.37 2 Chroniques 36.12 Jérémie 37.1-37.21 Jérémie 24.8 Ezéchiel 21.25
20 Maana kwa sababu ya hasira ya Bwana mambo hayo yalitokea katika Yerusalemu na katika Yuda, hata alipokuwa amewaondosha wasiwe mbele ya uso wake; naye Sedekia akamwasi mfalme wa Babeli.
2 Chroniques 36.13 Jérémie 27.12-27.15 Deutéronome 2.30 Deutéronome 29.27 1 Corinthiens 1.20

Cette Bible est dans le domaine public.