Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 16.9
Bible en Swahili de l’est


Règne d’Achaz sur Juda

1 Katika mwaka wa kumi na saba wa Peka mwana wa Remalia Ahazi mwana wa Yothamu mfalme wa Yuda alianza kutawala.
Esaïe 1.1 2 Rois 15.32-15.33 2 Chroniques 28.1-28.4 Esaïe 7.1 Michée 1.1
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini alipoanza kutawala; akatawala miaka kumi na sita katika Yerusalemu; wala hakufanya mema machoni pa Bwana Mungu wake, kama Daudi babaye.
2 Chroniques 17.3 2 Rois 22.2 1 Rois 9.4 2 Rois 14.3 2 Rois 15.3
3 Lakini aliiendea njia ya wafalme wa Israeli, hata akampitisha mwanawe motoni, sawasawa na machukizo ya mataifa Bwana aliowafukuza mbele ya wana wa Israeli.
Deutéronome 12.31 Lévitique 18.21 2 Rois 21.2 2 Rois 21.11 Psaumes 106.37-106.38
4 Kisha akatoa sadaka na kufukiza uvumba katika mahali pa juu, na juu ya vilima, na chini ya kila mti mbichi.
Deutéronome 12.2 1 Rois 14.23 Esaïe 65.4 Esaïe 66.17 2 Rois 14.4
5 Hapo ndipo akakwea Resini mfalme wa Shamu pamoja na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli juu ya Yerusalemu ili wapigane; wakamhusuru Ahazi, ila hawakuweza kumshinda.
2 Rois 15.37 Esaïe 7.1-7.9 Esaïe 8.9-8.10 2 Chroniques 28.5-28.15 1 Rois 15.4
6 Wakati huo Resini mfalme wa Shamu akawarudishia Washami Elathi, akawafukuza Wayahudi kutoka Elathi; nao Washami wakaja Elathi, wakakaa humo hata leo.
2 Rois 14.22 2 Chroniques 26.2 Deutéronome 2.8 1 Rois 9.26
7 Basi Ahazi akatuma wajumbe kwa Tiglath-pileseri mfalme wa Ashuru, akasema, Mimi ni mtumishi, tena mwana wako; kwea, ukaniokoe mkononi mwa mfalme wa Shamu, na mkononi mwa mfalme wa Israeli, walioniinukia.
2 Rois 15.29 Lamentations 4.17 1 Chroniques 5.26 2 Chroniques 28.20 Osée 14.3
8 Ahazi akatwaa fedha na dhahabu iliyoonekana katika nyumba ya Bwana, na katika hazina za nyumba ya mfalme, akazipeleka kwa mfalme wa Ashuru kuwa zawadi.
2 Rois 12.17-12.18 2 Rois 16.17-16.18 2 Chroniques 16.2 Esaïe 7.17 Esaïe 8.7-8.8
9 Na huyo mfalme wa Ashuru akamsikia; mfalme wa Ashuru akapanda juu ya Dameski, akautwaa, akawahamisha watu wake mateka mpaka Kiri, akamwua Resini.
Esaïe 22.6 Amos 9.7 Amos 1.3-1.5 2 Chroniques 28.21 2 Chroniques 28.5
10 Naye mfalme Ahazi akaenda Dameski ili aonane na Tiglath-pileseri mfalme wa Ashuru, akaiona ile madhabahu iliyokuwako Dameski. Mfalme Ahazi akamletea Uria kuhani namna yake ile madhabahu, na cheo chake, kama ilivyokuwa kazi yake yote.
Esaïe 8.2 Romains 12.2 2 Chroniques 28.23-28.25 Ezéchiel 43.8 Ezéchiel 43.11
11 Naye Uria kuhani akajenga madhabahu; sawasawa na yote aliyomletea mfalme Ahazi kutoka Dameski; ndivyo alivyoifanya Uria kuhani iwe tayari atakaporudi mfalme Ahazi kutoka Dameski.
Esaïe 8.2 Galates 1.10 Malachie 2.7-2.9 Ezéchiel 22.26 Osée 5.11
12 Na mfalme aliporudi kutoka Dameski, mfalme akaiona ile madhabahu; mfalme akakaribia madhabahuni, na kutoa sadaka juu yake.
2 Chroniques 26.16-26.19 Nombres 18.4-18.7 2 Chroniques 28.23 2 Chroniques 28.25 1 Rois 13.1
13 Akaiteketeza sadaka yake ya kuteketezwa, na sadaka yake ya unga, akamimina sadaka yake ya kinywaji, akanyunyiza damu ya sadaka zake za amani, juu ya madhabahu.
Lévitique 1.1-1.3
14 Na ile madhabahu ya shaba iliyokuwako mbele za Bwana, akaileta kutoka mbele ya nyumba, kutoka kati ya madhabahu yake mwenyewe na nyumba ya Bwana, akaiweka upande wa kaskazini wa madhabahu yake.
2 Chroniques 4.1 Exode 40.6 Exode 40.29 2 Rois 16.11 2 Chroniques 1.5
15 Mfalme Ahazi akamwamuru Uria kuhani, akisema, Juu ya madhabahu hiyo kubwa uiteketeze sadaka ya kuteketezwa ya asubuhi, na sadaka ya unga ya jioni, na sadaka ya mfalme ya kuteketezwa, na sadaka yake ya unga, pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya watu wote wa nchi, na sadaka yao ya unga, na sadaka zao za kinywaji; ukanyunyize juu yake damu yote ya sadaka ya kuteketezwa, na damu yote ya dhabihu; bali madhabahu ya shaba itakuwa kwangu mimi ili niiulizie.
Exode 29.39-29.41 1 Rois 8.64 2 Rois 18.4 2 Chroniques 29.21-29.24 Ezéchiel 46.12-46.14
16 Akafanya hivyo Uria kuhani, sawasawa na yote aliyoyaamuru mfalme Ahazi.
Actes 5.29 Actes 4.19 1 Thessaloniciens 2.4 Jude 1.11 2 Rois 16.11
17 Mfalme Ahazi akakata papi za matako, akaliondoa lile birika juu yake; akaitelemsha ile bahari itoke juu ya ng’ombe za shaba zilizokuwa chini yake, akaiweka juu ya sakafu ya mawe.
1 Rois 7.23-7.39 Jérémie 52.20 2 Chroniques 29.19 2 Rois 25.13-25.16 2 Chroniques 4.14-4.15
18 Na ukumbi wa sabato walioujenga katika hiyo nyumba, na mahali pa kuingia pake mfalme palipokuwapo nje, akavigeuza kuikabili nyumba ya Bwana, kwa sababu ya mfalme wa Ashuru.
Ezéchiel 46.2 1 Rois 10.5 2 Rois 11.5
19 Basi mambo yote ya Ahazi yaliyosalia, aliyoyafanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Yuda?
2 Rois 20.20-20.21 2 Chroniques 28.26 2 Rois 15.6-15.7 2 Rois 15.38 2 Rois 15.36
20 Ahazi akalala na babaze, akazikwa pamoja na babaze katika mji wa Daudi; na Hezekia mwanawe akatawala mahali pake.
Esaïe 1.1 Matthieu 1.9 2 Rois 18.1 2 Chroniques 28.27-29.1 2 Rois 21.18

Cette Bible est dans le domaine public.