Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 12.8
Bible en Swahili de l’est


Le schisme et ses suites

Accession au trône de Roboam et Jéroboam

1 Rehoboamu akaenda Shekemu; maana Israeli wote walikuwa wamekwenda Shekemu, ili kumfanya mfalme.
2 Chroniques 10.1-10.19 Josué 24.1 Actes 7.16 1 Rois 11.43 Juges 9.6
2 Ikawa Yeroboamu mwana wa Nebati alipopata habari (maana alikuwa akaliko Misri, huko alikokimbilia awe mbali na mfalme Sulemani; Yeroboamu akakaa huko Misri,
1 Rois 11.40 1 Rois 11.26-11.31 2 Chroniques 10.2-10.3
3 wakapeleka watu kwenda kumwita); basi Yeroboamu na jamii yote ya Israeli wakaenda, wakamwambia Rehoboamu, wakasema,
4 Baba yako alilifanya zito kongwa letu; basi sasa utupunguzie utumwa mzito tuliotumikishwa na baba yako, na lile kongwa zito alilotutwika, nasi tutakutumikia.
1 Samuel 8.11-8.18 1 Rois 9.15 1 Rois 4.7 1 Jean 5.3 Matthieu 23.4
5 Akawaambia, Enendeni zenu hata siku ya tatu, kisha mnirudie tena. Watu wakaenda zao.
1 Rois 12.12
6 Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee waliokuwa wakisimama mbele ya Sulemani, baba yake, alipokuwa hai, akasema, Mwanipa shauri gani ili niwajibu watu hawa?
Job 12.12 Job 32.7 2 Samuel 16.20 Proverbes 27.10 2 Samuel 17.5
7 Wakamwambia wakasema, Ukikubali kuwa mtumishi wa watu hawa leo, na kuwatumikia, na kuwajibu, na kuwapa maneno mazuri, basi watakuwa watumishi wako daima.
Proverbes 15.1 2 Chroniques 10.6-10.7 Zacharie 1.13 Ecclésiaste 10.4 Philippiens 2.7-2.11
8 Lakini akaliacha shauri lile la wazee, walilompa, akataka shauri kwa wale vijana waliokua pamoja naye, na kusimama mbele yake.
Proverbes 1.2-1.5 Proverbes 25.12 Proverbes 1.25 Proverbes 1.30 2 Chroniques 25.15-25.16
9 Akawaambia, Mwanipa shauri gani ili tuwajibu watu hawa, waliosema nami, wakinena Utufanyie jepesi kongwa lile alilotutwika baba yako?
2 Chroniques 10.9 2 Samuel 17.5-17.6 1 Rois 22.6-22.8 2 Chroniques 18.5-18.7
10 Na wale vijana waliokua pamoja naye wakamwambia, wakasema, Uwaambie hivi watu wale waliokuambia, wakisema, Baba yako alilifanya zito kongwa letu, bali wewe utufanyie jepesi, uwaambie hivi, Kidole changu cha mwisho ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
Proverbes 18.6-18.7 Proverbes 29.23 Proverbes 10.14 2 Samuel 17.7-17.13 Proverbes 28.25
11 Basi kama vile baba yangu alivyowatwika kongwa zito, mimi nitaongeza kongwa lenu; baba yangu aliwapiga kwa mijeledi, bali mimi nitawapigeni kwa nge.
Jérémie 27.11 Ezéchiel 2.6 Jérémie 28.13-28.14 1 Samuel 8.18 Exode 5.18
12 Basi, Yeroboamu na watu wote wakamfikia Rehoboamu siku ya tatu, kama mfalme alivyoamuru, akisema, Mnirudie siku ya tatu.
1 Rois 12.5 2 Chroniques 10.12-10.14
13 Mfalme akawajibu watu wale kwa ukali, akaliacha shauri lile wazee walilompa;
Jacques 3.17 Genèse 42.30 Proverbes 15.1 1 Samuel 20.30-20.31 1 Samuel 20.10
14 akawajibu kama vile walivyomshauri vijana, akasema, Baba yangu alilifanya zito kongwa lenu, bali mimi nitaongeza kongwa lenu; baba yangu aliwapiga kwa mijeledi, bali mimi nitawapigeni kwa nge.
Exode 5.5-5.9 1 Rois 12.10-12.11 Exode 5.16-5.18 Esther 2.2-2.4 Proverbes 12.5
15 Basi mfalme hakuwasikia wale watu; maana jambo hili lilitoka kwa Bwana, ili alitimize neno lake, Bwana alilomwambia Yeroboamu mwana wa Nebati kwa kinywa cha Ahiya Mshiloni.
1 Rois 12.24 Juges 14.4 Deutéronome 2.30 1 Rois 11.11 2 Chroniques 10.15
16 Basi Israeli wote walipoona ya kuwa mfalme hakuwasikia, hao watu walimjibu mfalme, wakasema, Tuna sehemu gani katika Daudi? Wala hatuna urithi katika mwana wa Yese. Haya! Nendeni zenu hemani kwenu, enyi Israeli; sasa itunze nyumba yako mwenyewe, Ee Daudi. Hivyo Israeli wakaenda zao hemani kwao.
2 Samuel 20.1 1 Rois 11.34 1 Rois 11.13 Psaumes 132.17 2 Chroniques 10.16
17 Lakini kwa habari za wana wa Israeli waliokaa katika miji ya Yuda, Rehoboamu aliwatawala wao.
1 Rois 11.36 1 Rois 11.13 2 Chroniques 11.13-11.17 2 Chroniques 10.17
18 Ndipo mfalme Rehoboamu akampeleka Adoramu, aliyekuwa juu ya shokoa, nao Israeli wote wakampiga kwa mawe hata akafa. Mfalme Rehoboamu akafanya haraka kupanda katika gari, ili akimbilie Yerusalemu.
1 Rois 4.6 1 Rois 5.14 2 Samuel 20.24 1 Rois 20.18-20.20 Amos 2.16
19 Hivyo Israeli wakaasi juu ya nyumba ya Daudi hata leo.
2 Rois 17.21 1 Samuel 10.19 2 Chroniques 13.17 2 Chroniques 10.19 Esaïe 7.17
20 Ikawa, Israeli wote waliposikia ya kwamba Yeroboamu amerudi, wakapeleka watu wakamwita aje mkutanoni, wakamfanya mfalme juu ya Israeli wote; wala hapakuwa na mtu aliyeshikamana na nyumba ya Daudi, ila kabila ya Yuda peke yake.
1 Rois 11.13 1 Rois 11.32 1 Rois 12.17 1 Rois 11.36 1 Samuel 10.24
21 Hata Rehoboamu alipofika Yerusalemu, akakusanya nyumba yote ya Yuda, pamoja na kabila ya Benyamini, watu wateule mia na themanini elfu, waliokuwa watu wa vita, ili wapigane na nyumba ya Israeli, waurudishe ufalme tena kwa Rehoboamu mwana wa Sulemani.
2 Chroniques 11.1-11.3 2 Chroniques 14.8 1 Chroniques 21.5 2 Chroniques 17.14-17.19 Proverbes 21.30-21.31
22 Lakini likaja neno la Mungu kwa Shemaya mtu wa Mungu, kusema,
2 Chroniques 11.2 Deutéronome 33.1 1 Rois 13.11 2 Chroniques 12.5-12.7 1 Rois 17.18
23 Mwambie Rehoboamu mwana wa Sulemani, mfalme wa Yuda, na jamaa yote ya Yuda na Benyamini, na watu waliosalia, ukisema,
1 Rois 12.17
24 Bwana asema hivi, Msiende, wala msipigane na ndugu zenu wana wa Israeli; rudini kila mtu nyumbani kwake; kwa kuwa jambo hili limetoka kwangu. Basi, wakalisikiliza neno la Bwana, wakarudi, wakaenda zao, sawasawa na neno la Bwana.
1 Rois 12.15 2 Chroniques 11.4 Osée 8.4 Nombres 14.42 2 Chroniques 28.9-28.15

Règne de Jéroboam sur Israël

25 Ndipo Yeroboamu akajenga Shekemu katika milima ya Efraimu, akakaa huko. Akatoka huko akajenga Penueli.
Juges 8.17 Juges 8.8 Juges 9.45-9.49 Genèse 32.30-32.31 Juges 9.1
26 Yeroboamu akasema moyoni mwake, Basi ufalme utairudia nyumba ya Daudi.
1 Rois 11.38 Jean 12.10-12.11 Psaumes 14.1 Jean 12.19 1 Samuel 27.1
27 Kama watu hawa wakipanda kwenda kutoa dhabihu katika nyumba ya Bwana huko Yerusalemu, ndipo mioyo ya watu hawa itamrudia bwana wao, yaani Rehoboamu, mfalme wa Yuda; nao wataniua mimi, na kumrudia Rehoboamu, mfalme wa Yuda.
Deutéronome 12.14 Deutéronome 12.5-12.7 1 Rois 11.32 Genèse 26.7 Deutéronome 16.6
28 Kwa hiyo mfalme akafanya shauri, akafanyiza ng’ombe wawili wa dhahabu, akawaambia watu, Ni vigumu kwenu kupanda kwenda Yerusalemu; tazama, hii ndiyo miungu yenu, enyi Israeli, iliyowapandisha kutoka nchi ya Misri.
Exode 32.4 Exode 32.8 2 Rois 17.16 2 Rois 10.29 2 Chroniques 11.15
29 Akamweka mmoja katika Betheli, na wa pili akamweka katika Dani.
Genèse 28.19 Deutéronome 34.1 Osée 4.15 2 Rois 10.29 Genèse 14.14
30 Jambo hili likawa dhambi, maana watu walikwenda kuabudu mbele ya kila mmoja, hata huko Dani.
2 Rois 17.21 1 Rois 13.34 2 Rois 10.31
31 Tena akafanya nyumba za mahali pa juu, akafanya na watu wo wote, watu wasio wa wana wa Lawi, kuwa makuhani.
2 Rois 17.32 2 Chroniques 13.9 1 Rois 13.32-13.33 2 Chroniques 11.14-11.15 Nombres 3.10
32 Yeroboamu akaamuru kushika sikukuu katika mwezi wa nane, siku ya kumi na tano ya mwezi, mfano wa sikukuu iliyokuwa katika Yuda, akapanda juu ili kuiendea madhabahu. Akafanya vivyo katika Betheli akiwatolea dhabihu wale ng’ombe aliowafanya; akawaweka katika Betheli wale makuhani wa mahali pa juu alipokuwa amepafanya.
1 Rois 8.2 1 Rois 8.5 Amos 7.10-7.13 Matthieu 15.8-15.9 Nombres 29.12-29.40
33 Akatoa dhabihu juu ya ile madhabahu aliyoifanya katika Betheli, siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, mwezi aliouwaza moyoni mwake mwenyewe; akawaamuru wana wa Israeli waishike sikukuu hiyo, akapanda kuiendea madhabahu, ili kufukiza uvumba.
1 Rois 13.1 Nombres 15.39 2 Chroniques 26.6 Marc 7.13 Matthieu 15.6

Cette Bible est dans le domaine public.