Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 3.18
Bible en Swahili de l’est


La tentation et la chute

1 Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani?
2 Corinthiens 11.3 Apocalypse 12.9 Apocalypse 20.2 2 Corinthiens 11.14 Matthieu 4.3
2 Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula;
Psaumes 58.4
3 lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa.
Genèse 2.16-2.17 Job 1.11 Job 2.5 Exode 19.12-19.13 Genèse 20.6
4 Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa,
Jean 8.44 2 Corinthiens 11.3 Genèse 3.13 Deutéronome 29.19 2 Corinthiens 2.11
5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.
Ezéchiel 28.2 Genèse 2.17 Psaumes 12.4 Ezéchiel 13.22 Jérémie 14.13-14.14
6 Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala.
1 Jean 2.16 1 Timothée 2.14 Jacques 1.14-1.15 2 Samuel 11.2 Josué 7.21
7 Wakafumbuliwa macho wote wawili wakajijua kuwa wa uchi, wakashona majani ya mtini, wakajifanyia nguo.
Genèse 2.25 Genèse 3.5 Job 9.29-9.31 Esaïe 59.6 Esaïe 28.20
8 Kisha wakasikia sauti ya Bwana Mungu, akitembea bustanini wakati wa jua kupunga; Adamu na mkewe wakajificha kati ya miti ya bustani, Bwana Mungu asiwaone.
Jérémie 23.24 Psaumes 139.1-139.12 Job 22.14 Job 31.33 Romains 2.15
9 Bwana Mungu akamwita Adamu, akamwambia, Uko wapi?
Genèse 4.9 Genèse 16.8 Josué 7.17-7.19 Apocalypse 20.12-20.13 Genèse 18.20-18.21
10 Akasema, Nalisikia sauti yako bustanini, nikaogopa kwa kuwa mimi ni uchi; nikajificha.
Genèse 2.25 Genèse 3.7 Esaïe 57.11 Exode 32.25 1 Jean 3.20
11 Akasema, Ni nani aliyekuambia ya kuwa u uchi? Je! Umekula wewe matunda ya mti niliyokuagiza usiyale?
Romains 3.20 Genèse 4.10 Psaumes 50.21
12 Adamu akasema, Huyo mwanamke uliyenipa awe pamoja nami ndiye aliyenipa matunda ya mti huo, nikala.
Job 31.33 Jacques 1.13-1.15 Genèse 2.18 Proverbes 28.13 1 Samuel 15.20-15.24
13 Bwana Mungu akamwambia mwanamke, Nini hili ulilolifanya? Mwanamke akasema, Nyoka alinidanganya, nikala.
2 Corinthiens 11.3 1 Timothée 2.14 2 Samuel 12.9-12.12 Jean 18.35 Genèse 3.4-3.6
14 Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako;
Esaïe 65.25 Michée 7.17 Psaumes 72.9 Esaïe 29.4 Genèse 3.1
15 nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.
Romains 16.20 1 Jean 3.8 Apocalypse 12.17 Galates 4.4 Esaïe 7.14
16 Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala.
1 Corinthiens 14.34 1 Timothée 2.15 1 Corinthiens 11.3 1 Timothée 2.11-2.12 Genèse 4.7
17 Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako;
Romains 8.20-8.22 Genèse 5.29 Ecclésiaste 2.22-2.23 Job 14.1 Matthieu 25.26-25.27
18 michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni;
Job 5.5 Esaïe 7.23 Josué 23.13 Psaumes 104.2 Psaumes 104.14-104.15
19 kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.
Ecclésiaste 12.7 Psaumes 104.29 Genèse 2.7 Psaumes 90.3 Job 34.15
20 Adamu akamwita mkewe jina lake Hawa; kwa kuwa yeye ndiye aliye mama yao wote walio hai.
Genèse 2.20 Actes 17.26 Genèse 2.23 1 Samuel 1.20 Matthieu 1.21
21 Bwana Mungu akawafanyia Adamu na mkewe mavazi ya ngozi, akawavika.
Esaïe 61.10 2 Corinthiens 5.2-5.3 2 Corinthiens 5.21 Romains 3.22 Genèse 3.7
22 Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele;
Genèse 1.26 Genèse 2.9 Genèse 3.5 Apocalypse 22.2 Jean 6.48-6.58
23 kwa hiyo Bwana Mungu akamtoa katika bustani ya Edeni, ailime ardhi ambayo katika hiyo alitwaliwa.
Genèse 4.2 Genèse 2.5 Genèse 9.20 Genèse 3.19 Ecclésiaste 5.9
24 Basi akamfukuza huyo mtu, akaweka Makerubi, upande wa mashariki wa bustani ya Edeni, na upanga wa moto uliogeuka huko na huko, kuilinda njia ya mti wa uzima.
Hébreux 1.7 Psaumes 104.4 Exode 25.18-25.22 Hébreux 10.18-10.22 1 Chroniques 21.16-21.17

Cette Bible est dans le domaine public.