Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 8.3
Bible en Swahili de l’est


Demande d’un roi par Israël

1 Hata Samweli alipokuwa mzee, aliwafanya wanawe wawe waamuzi juu ya Israeli.
Deutéronome 16.18-16.19 1 Timothée 5.21 2 Chroniques 19.5-19.6 Juges 10.4 Néhémie 7.2
2 Na jina la mwanawe mzaliwa wa kwanza aliitwa Yoeli; na jina la wa pili Abiya; walikuwa waamuzi katika Beer-sheba.
Amos 5.5 Genèse 22.19 1 Chroniques 6.38 1 Rois 19.3 1 Chroniques 6.28
3 Ila wanawe hawakuenda katika njia zake, bali waliziacha, ili wapate faida; wakapokea rushwa, na kupotosha hukumu.
Deutéronome 16.19 Psaumes 15.5 Exode 18.21 Exode 23.8 1 Timothée 6.10
4 Ndipo wazee wote wa Israeli wakakutana pamoja, wakamwendea Samweli huko Rama;
1 Samuel 7.17 2 Samuel 5.3 Exode 3.16 Exode 24.1
5 wakamwambia, Angalia, wewe umekuwa mzee, na wanao hawaendi katika njia zako; basi, tufanyie mfalme atuamue, mfano wa mataifa yote.
Deutéronome 17.14-17.15 1 Samuel 8.19-8.20 Actes 13.21 1 Samuel 8.6-8.8 Nombres 23.9
6 Lakini neno hilo likawa baya machoni pa Samweli, waliposema, Tupe mfalme atuamue. Naye Samweli akamwomba Bwana.
1 Samuel 15.11 1 Samuel 12.17 Luc 6.11-6.12 Nombres 16.22 Jacques 1.5
7 Bwana akamwambia Samweli, Isikilize sauti ya watu hawa katika kila neno watakalokuambia; kwa maana hawakukukataa wewe, bali wamenikataa mimi, ili nisiwe mfalme juu yao.
Exode 16.8 1 Samuel 10.19 Psaumes 81.11-81.12 Luc 10.16 Matthieu 10.40
8 Kwa kadiri ya matendo yote waliyonitenda tokea siku ile nilipowatoa katika Misri hata leo, kwa kuniacha mimi, na kwa kutumikia miungu mingine, ndivyo wanavyokutenda wewe.
Deutéronome 9.24 Juges 4.1 Juges 2.2-2.3 Psaumes 78.56-78.59 Psaumes 106.34-106.40
9 Basi sasa, isikilize sauti yao; walakini, uwaonye sana, na kuwaonyesha desturi ya mfalme atakayewamiliki.
1 Samuel 8.11-8.18 1 Samuel 10.25 Ezéchiel 3.18 Ezéchiel 46.18 1 Samuel 2.13
10 Naye Samweli akawaambia wale watu waliotaka mfalme maneno yote ya Bwana.
11 Akasema, Mfalme atakayewamiliki ninyi atakuwa na desturi hii; atatwaa wana wenu na kuwaweka kwake, kwa magari yake, na kuwa wapanda farasi wake; nao watapiga mbio mbele ya magari yake.
1 Samuel 14.52 1 Samuel 10.25 2 Samuel 15.1 Deutéronome 17.14-17.20 1 Rois 18.46
12 Naye atawaweka kwake kuwa maakida juu ya elfu, na maakida juu ya hamsini; na wengine atawaweka walime shamba lake, na kuvuna mavuno yake, na kufanyiza zana zake za vita, na vyombo vya magari yake.
1 Rois 4.7 1 Rois 4.22-4.23 2 Chroniques 32.28-32.29 1 Chroniques 27.1-27.22 1 Rois 4.27-4.28
13 Na binti zenu atawatwaa kuwa wafanyaji wa marhamu, na wapishi, na waokaji.
14 Atatwaa makonde yenu, na mashamba yenu ya mizabibu, na ya mizeituni, yale yaliyo mazuri sana, ili awape watumishi wake.
Ezéchiel 46.18 1 Rois 21.7 1 Rois 21.19 1 Samuel 22.7
15 Naye atawatoza ushuru wa mbegu zenu na wa mizabibu yenu, awape maakida wake, na watumishi Wake.
Daniel 1.18 Daniel 1.3 Esaïe 39.7 Daniel 1.7-1.10 Genèse 37.36
16 Atawatwaa watumishi wenu na wajakazi wenu, na ng’ombe zenu walio wazuri sana, na punda zenu, naye atawatia katika kazi zake mwenyewe.
17 Atawatoza fungu la kumi la makundi yenu; nanyi mtakuwa watumwa wake.
18 Nanyi mtalia siku ile kwa sababu ya mfalme wenu mliyejichagulia; Bwana asiwajibu siku ile.
Michée 3.4 Esaïe 1.15 Esaïe 8.21 Proverbes 1.25-1.28 Luc 13.25
19 Walakini hao watu wakakataa kuisikiliza sauti ya Samweli; wakasema, Sivyo hivyo; lakini tunataka kuwa na mfalme juu yetu;
Jérémie 44.16 Jérémie 7.13 Esaïe 66.4 Ezéchiel 33.31 Psaumes 81.11
20 ili sisi nasi tufanane na mataifa yote; tena ili mfalme wetu atuamue, tena atoke mbele yetu na kutupigia vita vyetu.
1 Samuel 8.5 Philippiens 3.20 Nombres 23.9 Deutéronome 7.6 2 Corinthiens 6.17
21 Samweli akayasikia maneno yote ya watu, akayanena masikioni mwa Bwana.
Juges 11.11
22 Bwana akamwambia Samweli, Isikilize sauti yao, ukawafanyie mfalme. Kisha Samweli akawaambia watu wa Israeli, Enendeni kila mtu mjini kwake.
1 Samuel 8.7 Osée 13.11

Cette Bible est dans le domaine public.