Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 3.18
Bible en Swahili de l’est


Appel de Samuel

1 Basi, mtoto Samweli akamtumikia Bwana mbele ya Eli. Na neno la Bwana lilikuwa adimu siku zile; hapakuwa na mafunuo dhahiri.
Psaumes 74.9 1 Samuel 2.11 Amos 8.11-8.12 1 Samuel 2.18 1 Samuel 3.21
2 Ikawa wakati huo, Eli alipokuwa amelala mahali pake (tena macho yake yalikuwa yameanza kupofuka, hata asiweze kuona),
1 Samuel 4.15 Genèse 27.1 1 Samuel 2.22 Genèse 48.19 Ecclésiaste 12.3
3 na taa ya Mungu ilikuwa haijazimika bado, na Samweli alikuwa amelala katika hekalu la Bwana, palipokuwa na sanduku la Mungu;
2 Chroniques 13.11 Exode 27.20-27.21 Lévitique 24.2-24.4 Psaumes 29.9 Psaumes 5.7
4 basi, wakati huo Bwana akamwita Samweli; naye akasema, Mimi hapa.
Genèse 22.1 1 Corinthiens 12.6-12.11 Psaumes 99.6 Galates 1.15-1.16 Esaïe 6.8
5 Akamwendea Eli kwa haraka, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akasema, Sikukuita; kalale tena. Naye akaenda, akalala tena.
6 Bwana akaita mara ya pili, Samweli! Samweli! Akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akajibu, Sikukuita, mwanangu; kalale tena.
Matthieu 9.2 2 Samuel 18.22 1 Samuel 4.16 Genèse 43.29
7 Basi Samweli alikuwa hamjui Bwana bado, na neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake.
Actes 19.2 Jérémie 9.24
8 Bwana akamwita Samweli mara ya tatu. Naye akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Ndipo Eli akatambua ya kuwa Bwana ndiye aliyemwita yule mtoto.
1 Corinthiens 13.11-13.12 Job 33.14-33.15
9 Kwa hivyo Eli akamwambia Samweli, Enenda, kalale; itakuwa, akikuita, utasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. Basi Samweli akaenda akalala mahali pake.
Exode 20.19 Daniel 10.19 Esaïe 6.8 Psaumes 85.8 Actes 9.6
10 Bwana akaja, akasimama, akaita vile vile kama kwanza, Samweli! Samweli! Ndipo Samweli akasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia.
11 Bwana akamwambia Samweli, Angalia, nitatenda tendo katika Israeli, ambalo kila atakayelisikia masikio yake yatamwasha.
Jérémie 19.3 2 Rois 21.12 Habakuk 1.5 Luc 21.26 Actes 13.41
12 Siku hiyo nitayatimiza maneno yale yote niliyoyasema juu ya Eli katika habari za nyumba yake, tangu mwanzo hata mwisho.
1 Samuel 2.27-2.36 Josué 23.15 Nombres 23.19 Zacharie 1.6 Luc 21.33
13 Kwa maana nimemwambia ya kwamba nitaihukumu nyumba yake milele, kwa ajili ya ule uovu alioujua; kwa kuwa wanawe walijiletea laana, wala yeye hakuwazuia.
1 Samuel 2.12 1 Samuel 2.17 Proverbes 29.15 Proverbes 23.13-23.14 1 Samuel 2.22-2.36
14 Na kwa hiyo nimeapa juu ya nyumba ya Eli, ya kwamba uovu wa nyumba ya Eli hautasafika kwa dhabihu wala kwa sadaka hata milele.
Esaïe 22.14 1 Samuel 2.25 Hébreux 10.26-10.31 Psaumes 51.16 Jérémie 15.1
15 Naye Samweli akalala hata asubuhi, akaifungua milango ya nyumba ya Bwana. Samweli akaogopa kumjulisha Eli maono hayo.
Jérémie 1.6-1.8 1 Samuel 1.9 1 Corinthiens 16.10-16.11 Malachie 1.10
16 Basi Eli akamwita Samweli, akasema, Samweli, mwanangu. Naye akajibu, Mimi hapa.
17 Akamwuliza, Ni neno gani alilosema nawe? Nakusihi, usinifiche; Mungu akufanyie vivyo hivyo, na kuzidi, ukinificha lo lote katika hayo yote Bwana aliyosema nawe.
2 Samuel 3.35 Ruth 1.17 Psaumes 141.5 2 Samuel 19.13 1 Rois 22.16
18 Basi Samweli akamwambia kila neno, asimfiche lo lote. Naye akasema, Ndiye Bwana; na afanye alionalo kuwa ni jema.
Job 2.10 Esaïe 39.8 Psaumes 39.9 Job 1.21 Lamentations 3.39
19 Samweli akakua, naye Bwana alikuwa pamoja naye, wala hakuliacha neno lake lo lote lianguke chini.
1 Samuel 9.6 1 Samuel 2.21 Genèse 39.2 Luc 2.52 Juges 13.24
20 Nao Waisraeli wote, toka Dani mpaka Beer-sheba, walitambua ya kwamba huyo Samweli amewekwa kuwa nabii wa Bwana.
Juges 20.1 2 Samuel 3.10 2 Samuel 17.11 1 Timothée 1.12
21 Naye Bwana akaonekana tena huko Shilo; kwa kuwa Bwana akajifunua kwa Samweli huko Shilo, kwa neno la Bwana. Nalo neno la Samweli likawajia Israeli wote.
1 Samuel 3.1 Genèse 12.7 1 Samuel 3.4 1 Samuel 3.10 Hébreux 1.1

Cette Bible est dans le domaine public.