Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 3.1
Bible en Swahili de l’est


Appel de Samuel

1 Basi, mtoto Samweli akamtumikia Bwana mbele ya Eli. Na neno la Bwana lilikuwa adimu siku zile; hapakuwa na mafunuo dhahiri.
Psaumes 74.9 Amos 8.11-8.12 1 Samuel 2.11 1 Samuel 2.18 1 Samuel 3.21
2 Ikawa wakati huo, Eli alipokuwa amelala mahali pake (tena macho yake yalikuwa yameanza kupofuka, hata asiweze kuona),
1 Samuel 4.15 Genèse 27.1 Ecclésiaste 12.3 Psaumes 90.10 Genèse 48.10
3 na taa ya Mungu ilikuwa haijazimika bado, na Samweli alikuwa amelala katika hekalu la Bwana, palipokuwa na sanduku la Mungu;
Exode 27.20-27.21 Lévitique 24.2-24.4 2 Chroniques 13.11 1 Samuel 1.6 Psaumes 27.4
4 basi, wakati huo Bwana akamwita Samweli; naye akasema, Mimi hapa.
Esaïe 6.8 Actes 9.4 1 Corinthiens 12.28 Exode 3.4 Genèse 22.1
5 Akamwendea Eli kwa haraka, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akasema, Sikukuita; kalale tena. Naye akaenda, akalala tena.
6 Bwana akaita mara ya pili, Samweli! Samweli! Akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akajibu, Sikukuita, mwanangu; kalale tena.
Matthieu 9.2 2 Samuel 18.22 1 Samuel 4.16 Genèse 43.29
7 Basi Samweli alikuwa hamjui Bwana bado, na neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake.
Actes 19.2 Jérémie 9.24
8 Bwana akamwita Samweli mara ya tatu. Naye akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Ndipo Eli akatambua ya kuwa Bwana ndiye aliyemwita yule mtoto.
1 Corinthiens 13.11-13.12 Job 33.14-33.15
9 Kwa hivyo Eli akamwambia Samweli, Enenda, kalale; itakuwa, akikuita, utasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. Basi Samweli akaenda akalala mahali pake.
Psaumes 85.8 Exode 20.19 Daniel 10.19 Esaïe 6.8 Actes 9.6
10 Bwana akaja, akasimama, akaita vile vile kama kwanza, Samweli! Samweli! Ndipo Samweli akasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia.
11 Bwana akamwambia Samweli, Angalia, nitatenda tendo katika Israeli, ambalo kila atakayelisikia masikio yake yatamwasha.
2 Rois 21.12 Jérémie 19.3 Actes 13.41 Esaïe 28.19 Habakuk 1.5
12 Siku hiyo nitayatimiza maneno yale yote niliyoyasema juu ya Eli katika habari za nyumba yake, tangu mwanzo hata mwisho.
1 Samuel 2.27-2.36 Luc 21.33 Josué 23.15 Nombres 23.19 Zacharie 1.6
13 Kwa maana nimemwambia ya kwamba nitaihukumu nyumba yake milele, kwa ajili ya ule uovu alioujua; kwa kuwa wanawe walijiletea laana, wala yeye hakuwazuia.
1 Samuel 2.17 1 Samuel 2.12 1 Samuel 2.22-2.36 Proverbes 19.18 Matthieu 10.37
14 Na kwa hiyo nimeapa juu ya nyumba ya Eli, ya kwamba uovu wa nyumba ya Eli hautasafika kwa dhabihu wala kwa sadaka hata milele.
Esaïe 22.14 1 Samuel 2.25 Jérémie 15.1 Nombres 15.30-15.31 Jérémie 7.16
15 Naye Samweli akalala hata asubuhi, akaifungua milango ya nyumba ya Bwana. Samweli akaogopa kumjulisha Eli maono hayo.
Jérémie 1.6-1.8 1 Samuel 1.9 1 Corinthiens 16.10-16.11 Malachie 1.10
16 Basi Eli akamwita Samweli, akasema, Samweli, mwanangu. Naye akajibu, Mimi hapa.
17 Akamwuliza, Ni neno gani alilosema nawe? Nakusihi, usinifiche; Mungu akufanyie vivyo hivyo, na kuzidi, ukinificha lo lote katika hayo yote Bwana aliyosema nawe.
Ruth 1.17 2 Samuel 3.35 Michée 2.7 1 Samuel 20.13 Daniel 4.19
18 Basi Samweli akamwambia kila neno, asimfiche lo lote. Naye akasema, Ndiye Bwana; na afanye alionalo kuwa ni jema.
Esaïe 39.8 Job 2.10 Psaumes 39.9 Job 1.21 1 Pierre 5.6
19 Samweli akakua, naye Bwana alikuwa pamoja naye, wala hakuliacha neno lake lo lote lianguke chini.
1 Samuel 9.6 1 Samuel 2.21 Genèse 39.2 Luc 2.52 2 Corinthiens 13.11
20 Nao Waisraeli wote, toka Dani mpaka Beer-sheba, walitambua ya kwamba huyo Samweli amewekwa kuwa nabii wa Bwana.
Juges 20.1 2 Samuel 3.10 2 Samuel 17.11 1 Timothée 1.12
21 Naye Bwana akaonekana tena huko Shilo; kwa kuwa Bwana akajifunua kwa Samweli huko Shilo, kwa neno la Bwana. Nalo neno la Samweli likawajia Israeli wote.
1 Samuel 3.1 Genèse 12.7 1 Samuel 3.4 Amos 3.7 Genèse 15.1

Cette Bible est dans le domaine public.