Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 10.21
Bible en Swahili de l’est


Onction de Saül comme roi d’Israël

1 Ndipo Samweli akatwaa kichupa cha mafuta, akayamimina kichwani pake, akambusu, akasema, Je! Bwana hakukutia mafuta [uwe mkuu juu ya watu wake Israeli? Nawe utamiliki watu wa Bwana, na kuwaokoa na mikono ya adui zao; kisha hii itakuwa ishara kwako ya kuwa Bwana amekutia mafuta] uwe mkuu juu ya urithi wake.
1 Samuel 16.13 Deutéronome 32.9 Psaumes 78.71 Psaumes 2.12 1 Samuel 9.16
2 Utakapoondoka kwangu leo, utakutana na wanaume wawili karibu na kaburi la Raheli, katika mpaka wa Benyamini huko Selsa; nao watakuambia, Punda hao uliokwenda kuwatafuta wameonekana; na tazama, baba yako ameacha kufikiri habari za punda, anafikiri habari zenu, akisema, Nifanye nini kwa ajili ya mwanangu?
1 Samuel 9.3-9.5 Genèse 35.19-35.20 Josué 18.28 1 Samuel 10.16 Jérémie 31.15
3 Kisha utakwenda mbele kutoka hapo, na kufika kwa mwaloni wa Tabori, na hapo watu watatu watakutana nawe, wanaokwea kumwendea Mungu huko Betheli, mmoja anachukua wana-mbuzi watatu, na mwingine anachukua mikate mitatu, na mwingine anachukua kiriba cha divai;
Genèse 35.3 Genèse 28.22 Genèse 35.1 Genèse 28.19 Lévitique 3.12
4 nao watakusalimu na kukupa mikate miwili; nawe utaipokea mikononi mwao.
Juges 18.15
5 Baada ya hayo utafika Gibea ya Mungu, hapo palipo na ngome ya Wafilisti; kisha itakuwa, utakapofika mjini, utakutana na kundi la manabii wakishuka kutoka mahali pa juu, wenye kinanda, na tari, na kinubi, na filimbi mbele yao, nao watakuwa wakitabiri;
1 Samuel 13.3 1 Samuel 19.20 2 Rois 3.15 2 Rois 2.3 1 Chroniques 25.1-25.6
6 na roho ya Bwana itakujilia kwa nguvu, nawe utatabiri pamoja nao, nawe utageuzwa kuwa mtu mwingine.
1 Samuel 10.10 1 Samuel 19.23-19.24 Nombres 11.25 1 Samuel 16.13 Juges 3.10
7 Basi, hapo ishara hizi zitakapokutukia, fanya kama uonavyo vema; kwa kuwa Mungu yu pamoja nawe.
Juges 6.12 Luc 2.12 Exode 4.8 Josué 1.5 Juges 9.33
8 Nawe utatelemka mbele yangu mpaka Gilgali; nami, angalia, nitakutelemkia huko, ili kutoa sadaka za kuteketezwa, na kuchinja sadaka za amani; siku saba utangoja, hata nitakapokujia, na kukuonyesha yatakayokupasa kuyafanya.
1 Samuel 11.14-11.15 1 Samuel 13.4 1 Samuel 15.33 1 Samuel 13.8-13.15
9 Ikawa, alipogeuka kumwacha Samweli, Mungu akambadilisha moyo; nazo ishara zile zote zikatukia siku ile ile.
Juges 6.36-6.40 1 Samuel 10.2-10.6 Marc 14.16 Juges 6.21 Esaïe 38.7-38.8
10 Basi, walipofika Gibea, tazama, kikosi cha manabii wakakutana naye; kisha roho ya Mungu ikamjilia kwa nguvu, naye akatabiri kati yao.
1 Samuel 10.5-10.6 1 Samuel 19.20-19.24
11 Ikawa, wote waliomjua zamani walipoliona jambo hilo, kwamba, tazama, huyo anatabiri pamoja na manabii, ndipo watu wakasemezana, Ni nini hilo lililompata mwana wa Kishi? Je! Sauli pia yumo miongoni mwa manabii?
Jean 7.15 1 Samuel 19.24 Matthieu 13.54-13.55 Actes 9.21 Actes 4.13
12 Naye akajibu mtu mmoja wa mahali hapo, akasema, Na baba yao n’nani? Kwa hiyo ikawa mithali, Je! Sauli pia yumo miongoni mwa manabii?
Esaïe 54.13 Jean 6.45 Jacques 1.17 Jean 7.16
13 Naye alipokwisha kutabiri, alipafikilia mahali pale pa juu.
14 Basi babaye mdogo akamwuliza Sauli na mtumishi wake, Je! Mlikwenda wapi? Naye akajibu, Tulikwenda ili kuwatafuta hao punda; na tulipoona ya kwamba hawakuonekana, tulimwendea Samweli.
1 Samuel 14.50 1 Samuel 9.3-9.10 2 Rois 5.25
15 Babaye mdogo Sauli akasema, Tafadhali uniambie, huyo Samweli aliwaambiaje?
16 Lakini Sauli akamjibu babaye mdogo, Alituambia waziwazi ya kuwa hao punda wamekwisha onekana. Lakini habari ya ufalme, ambayo Samweli alimwambia, hakuitaja habari hiyo.
1 Samuel 9.20 Juges 14.6 1 Samuel 9.27 Exode 4.18 Proverbes 29.11
17 Basi Samweli akawakusanya watu mbele za Bwana huko Mispa
Juges 20.1 1 Samuel 7.5-7.6
18 akawaambia wana wa Israeli, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Naliwatoa Israeli kutoka Misri, nami naliwaokoa ninyi na mikono ya Wamisri, na ya falme zote zilizowaonea;
Juges 6.8-6.9 Néhémie 9.27-9.28 Juges 2.1 Néhémie 9.9-9.12
19 lakini leo mmemkataa Mungu wenu, naye ndiye awaponyaye katika misiba yenu yote na shida zenu; nanyi mmemwambia, Sivyo, lakini weka mfalme juu yetu. Basi, sasa, hudhurieni mbele za Bwana, kwa kabila zenu na kwa elfu zenu.
1 Samuel 12.12 1 Samuel 8.19 Josué 24.1 Josué 7.14-7.26 1 Samuel 12.17-12.19
20 Basi Samweli akawaleta kabila zote za Israeli karibu; na kabila ya Benyamini ikatwaliwa.
Actes 1.24-1.26 1 Samuel 14.41 Josué 7.16-7.18
21 Kisha akaileta kabila ya Benyamini karibu, kwa jamaa zao; jamaa ya Wamatri ikatwaliwa. Akaileta jamaa ya Wamatri karibu, mtu baada ya mtu; kisha Sauli, mwana wa Kishi, akatwaliwa; lakini walipomtafuta hakuonekana.
22 Basi wakazidi kumwuliza Bwana, Amebaki mtu asiyekuja huku bado? Naye Bwana akajibu, Tazama, amejificha penye mizigo.
Nombres 27.21 Juges 1.1 Juges 20.18 1 Samuel 23.11-23.12 Juges 20.28
23 Basi wakaenda mbio wakamleta kutoka huko; naye aliposimama kati ya watu, alikuwa mrefu kuliko watu wote, tangu mabega yake kwenda juu.
1 Samuel 9.2 1 Samuel 16.7 1 Samuel 17.4
24 Samweli akawaambia watu wote, Mnamwona mtu huyu aliyechaguliwa na Bwana, ya kuwa hakuna mtu mfano wake katika watu wote. Ndipo watu wote wakapiga kelele, wakasema, Mfalme na aishi!
1 Rois 1.25 1 Rois 1.39 2 Samuel 21.6 Deutéronome 17.15 2 Rois 11.12
25 Kisha Samweli aliwaambia watu madaraka ya ufalme, akayaandika katika kitabu, akakiweka mbele za Bwana. Samweli akawaruhusu watu wote, waende kila mtu nyumbani kwake.
Deutéronome 17.14-17.20 1 Samuel 8.11-8.18 1 Timothée 2.2 1 Pierre 2.13-2.14 Tite 3.1
26 Sauli naye akaenda nyumbani kwake huko Gibea; na pamoja naye wakaenda kikosi cha watu, ambao Mungu alikuwa ameigusa mioyo yao.
1 Samuel 11.4 1 Samuel 15.34 Juges 20.14 Actes 7.10 Josué 18.28
27 Walakini wengine wasiofaa kitu wakasema, Huyu je! Atatuokoaje? Nao wakamdharau, wasimletee zawadi.
Deutéronome 13.13 2 Chroniques 17.5 1 Rois 10.25 1 Samuel 2.12 Matthieu 2.11

Cette Bible est dans le domaine public.