Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Apocalypse 20.2
Bible en Swahili de l’est


Satan enchaîné et relâché

1 Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake.
Apocalypse 1.18 2 Pierre 2.4 Apocalypse 10.1 Jude 1.6 Apocalypse 9.1-9.2
2 Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu;
Apocalypse 12.9 2 Pierre 2.4 Esaïe 27.1 Jude 1.6 Matthieu 8.29
3 akamtupa katika kuzimu, akamfunga, akatia muhuri juu yake, asipate kuwadanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe muda mchache.
Apocalypse 12.9 Daniel 6.17 Matthieu 27.66 Apocalypse 20.1 Apocalypse 20.7-20.10
4 Kisha nikaona viti vya enzi, wakaketi juu yake, nao wakapewa hukumu; nami nikaona roho zao waliokatwa vichwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu, na kwa ajili ya neno la Mungu, na hao wasiomsujudia yule mnyama, wala sanamu yake, wala hawakuipokea ile chapa katika vipaji vya nyuso zao, wala katika mikono yao; nao wakawa hai, wakatawala pamoja na Kristo miaka elfu.
Daniel 7.27 Matthieu 19.28 Daniel 7.9 Daniel 7.22 Apocalypse 6.9
5 Hao wafu waliosalia hawakuwa hai, hata itimie ile miaka elfu.
Luc 14.14 Apocalypse 11.11 Apocalypse 20.8-20.9 Philippiens 3.11 Romains 11.15
6 Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri, na mtakatifu, ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hao mauti ya pili haina nguvu; bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye hiyo miaka elfu.
Apocalypse 1.6 Apocalypse 2.11 Apocalypse 20.14 Apocalypse 5.10 Apocalypse 14.13
7 Na hiyo miaka elfu itakapokwisha, Shetani atafunguliwa, atoke kifungoni mwake;
Apocalypse 20.2
8 naye atatoka kuwadanganya mataifa walio katika pembe nne za nchi, Gogu na Magogu, kuwakusanya kwa vita, ambao hesabu yao ni kama mchanga wa bahari.
Apocalypse 16.14 Apocalypse 20.3 Apocalypse 20.10 Ezéchiel 38.1-39.1 Hébreux 11.12
9 Wakapanda juu ya upana wa nchi, wakaizingira kambi ya watakatifu, na mji huo uliopendwa. Moto ukashuka kutoka mbinguni, ukawala.
Ezéchiel 38.16 Ezéchiel 38.22 Ezéchiel 38.9 Ezéchiel 39.6 Apocalypse 13.13
10 Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele.
Apocalypse 19.20 Matthieu 25.41 Apocalypse 20.2-20.3 Apocalypse 16.13 Apocalypse 20.14-20.15

Le jugement dernier

11 Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana.
Daniel 2.35 Apocalypse 21.1 Matthieu 24.35 Jérémie 4.23-4.26 Apocalypse 6.14
12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.
2 Corinthiens 5.10 Matthieu 16.27 Daniel 7.10 Apocalypse 2.23 Apocalypse 3.5
13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
Apocalypse 6.8 Apocalypse 20.12 Jean 5.28-5.29 1 Corinthiens 15.50-15.58 Esaïe 26.19
14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto.
1 Corinthiens 15.26 Apocalypse 20.6 Apocalypse 19.20 Apocalypse 21.8 Apocalypse 1.18
15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.
Jean 3.36 Matthieu 13.50 Apocalypse 19.20 Marc 9.43-9.48 Matthieu 25.41

Cette Bible est dans le domaine public.