Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Jean 4.10
Bible en Swahili de l’est


Caractéristiques de l’Esprit de vérité

1 Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.
2 Pierre 2.1 1 Thessaloniciens 5.21 1 Jean 2.18 1 Timothée 4.1 Luc 12.57
2 Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu.
1 Corinthiens 12.3 Jean 1.14 1 Jean 5.1 1 Timothée 3.16 1 Jean 4.3
3 Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani.
1 Jean 2.22 1 Jean 2.18 2 Jean 1.7 2 Thessaloniciens 2.3-2.8
4 Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika dunia.
1 Jean 5.4 Jean 12.31 Romains 8.31 1 Jean 5.19 Romains 8.37
5 Hao ni wa dunia; kwa hiyo wanena ya dunia na dunia huwasikia
Jean 17.14 Jean 8.23 Jean 17.16 Jean 3.31 2 Timothée 4.3
6 Sisi twatokana na Mungu. Yeye amjuaye Mungu atusikia; yeye asiyetokana na Mungu hatusikii. Katika hili twamjua Roho wa kweli, na roho ya upotevu.
Jean 14.17 1 Corinthiens 14.37 Jean 10.27 1 Jean 4.1 Jean 15.26

L’amour de Dieu et l’amour mutuel

7 Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.
1 Jean 4.8 1 Jean 4.20-5.1 1 Jean 2.29 1 Thessaloniciens 4.9-4.10 1 Jean 2.10
8 Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo.
1 Jean 4.16 1 Jean 1.5 Psaumes 86.15 2 Corinthiens 13.11 Psaumes 86.5
9 Katika hili pendo la Mungu lilionekana kwetu, kwamba Mungu amemtuma Mwanawe pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kwa yeye.
Jean 3.16 1 Jean 5.11 1 Jean 4.10 Jean 6.57 Romains 8.32
10 Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu.
Ephésiens 2.4-2.5 1 Jean 2.2 1 Jean 3.1 Romains 5.8-5.10 Jean 15.16
11 Wapenzi ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana.
1 Jean 3.23 Colossiens 3.13 Jean 13.34 2 Corinthiens 8.8-8.9 1 Jean 3.16-3.17
12 Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote. Tukipendana, Mungu hukaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu.
Jean 1.18 1 Jean 2.5 1 Jean 4.20 1 Timothée 6.16 1 Jean 3.24
13 Katika hili tunafahamu ya kuwa tunakaa ndani yake, naye ndani yetu, kwa kuwa ametushirikisha Roho wake.
1 Jean 3.24 Galates 5.22-5.25 1 Jean 4.15-4.16 1 Corinthiens 3.16-3.17 Jean 14.20-14.26
14 Na sisi tumeona na kushuhudia ya kuwa Baba amemtuma Mwana kuwa Mwokozi wa ulimwengu.
Jean 4.42 1 Jean 4.10 Jean 15.26-15.27 Jean 1.14 Jean 3.16-3.17
15 Kila akiriye ya kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu hukaa ndani yake, naye ndani ya Mungu.
1 Jean 5.5 Romains 10.9 1 Jean 3.24 1 Jean 4.2 Philippiens 2.11
16 Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.
1 Jean 4.8-4.10 Esaïe 64.4 1 Jean 3.24 1 Jean 3.1 1 Corinthiens 2.9
17 Katika hili pendo limekamilishwa kwetu, ili tuwe na ujasiri katika siku ya hukumu; kwa kuwa, kama yeye alivyo, ndivyo tulivyo na sisi ulimwenguni humu.
1 Jean 2.5 1 Jean 2.28 1 Jean 4.12 1 Jean 3.19-3.21 Romains 8.29
18 Katika pendo hamna hofu; lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu, kwa maana hofu ina adhabu; na mwenye hofu hakukamilishwa katika pendo.
2 Timothée 1.7 Romains 8.15 1 Jean 4.12 Luc 1.74-1.75 Hébreux 12.28
19 Sisi twapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza.
1 Jean 4.10 Luc 7.47 Galates 5.22 Jean 3.16 Tite 3.3-3.5
20 Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona.
1 Jean 3.17 1 Jean 4.12 1 Jean 2.4 1 Jean 2.9 1 Jean 2.11
21 Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.
1 Jean 3.11 Matthieu 22.37-22.39 1 Thessaloniciens 4.9 Lévitique 19.18 Romains 13.9-13.10

Cette Bible est dans le domaine public.