Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Pierre 5.11
Bible en Swahili de l’est


Les relations dans l’Église

1 Nawasihi wazee walio kwenu, mimi niliye mzee, mwenzi wao, na shahidi wa mateso ya Kristo, na mshirika wa utukufu utakaofunuliwa baadaye;
Luc 24.48 Romains 8.17-8.18 Apocalypse 1.9 Actes 11.30 Colossiens 3.3-3.4
2 lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo.
Tite 1.7 1 Timothée 3.8 Tite 3.1 1 Timothée 3.3 Apocalypse 18.12-18.13
3 Wala si kama wajifanyao mabwana juu ya mitaa yao, bali kwa kujifanya vielelezo kwa lile kundi.
Philippiens 3.17 Tite 2.7 2 Thessaloniciens 3.9 Ezéchiel 34.4 1 Timothée 4.12
4 Na Mchungaji mkuu atakapodhihirishwa, mtaipokea taji ya utukufu, ile isiyokauka.
1 Corinthiens 9.25 Jacques 1.12 2 Timothée 4.8 1 Pierre 1.4 Apocalypse 2.10
5 Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.
Jacques 4.6 Ephésiens 5.21 Esaïe 66.2 Psaumes 132.9 Philippiens 2.3
6 Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake;
Jacques 4.10 Matthieu 23.12 Proverbes 29.23 Luc 1.52 Luc 18.14
7 huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.
Psaumes 55.22 Psaumes 37.5 Philippiens 4.6 Psaumes 56.3-56.4 Matthieu 6.25-6.26
8 Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.
Ephésiens 6.11 Jacques 4.7 1 Pierre 1.13 Job 2.2 1 Thessaloniciens 5.6-5.8
9 Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani.
Jacques 4.7 Actes 14.22 1 Corinthiens 10.13 2 Timothée 4.7 1 Thessaloniciens 3.3
10 Na Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika Kristo, mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawatengeneza, na kuwathibitisha, na kuwatia nguvu.
2 Corinthiens 4.17 2 Thessaloniciens 3.3 1 Pierre 1.6-1.7 2 Thessaloniciens 2.17 1 Corinthiens 1.9
11 Uweza una yeye hata milele na milele. Amina.
1 Pierre 4.11 Romains 11.36 Apocalypse 5.13 Apocalypse 1.6

Salutations

12 Kwa mkono wa Silwano, ndugu mwaminifu kama nionavyo, nimewaandikia kwa maneno machache, kuonya na kushuhudia ya kuwa hii ndiyo neema ya kweli ya Mungu. Simameni imara katika hiyo.
Hébreux 13.22 1 Corinthiens 15.1 2 Corinthiens 1.19 Actes 11.23 Actes 20.24
13 Mwenzenu mteule hapa Babeli awasalimu, na Marko mwanangu.
Actes 12.12 Actes 12.25 Psaumes 87.4 Apocalypse 17.5 Apocalypse 18.2
14 Salimianeni kwa busu la upendo. Amani na iwe kwenu nyote, mlio katika Kristo. Amina.
Ephésiens 6.23 Romains 16.16 Romains 1.7 Romains 8.1 1 Pierre 1.2

Cette Bible est dans le domaine public.