1 Basi kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ile ile; kwa maana yeye aliyeteswa katika mwili ameachana na dhambi.
Galates 5.24  1 Pierre 3.18  Romains 6.11  Romains 6.7  Ephésiens 6.13  
 2 Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.
Ephésiens 4.22-4.24  Tite 3.3-3.8  Ephésiens 2.3  Marc 3.35  2 Corinthiens 5.15  
 3 Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;
Ephésiens 5.18  1 Thessaloniciens 4.5  Galates 5.21  Ezéchiel 44.6  Ezéchiel 45.9  
 4 mambo ambayo wao huona kuwa ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana.
1 Pierre 3.16  Jude 1.10  2 Pierre 2.22  1 Pierre 2.12  2 Pierre 2.12  
 5 Nao watatoa hesabu kwake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa.Actes 10.42  2 Timothée 4.1  Jacques 5.9  Romains 14.10-14.12  Psaumes 1.6  
 6 Maana kwa ajili hiyo hata hao waliokufa walihubiriwa Injili, ili kwamba wahukumiwe katika mwili kama wahukumiwavyo wanadamu; bali wawe hai katika roho kama Mungu alivyo hai.
Tite 3.3-3.7  Ephésiens 2.3-2.5  Romains 8.2  Romains 8.9-8.11  1 Pierre 4.1-4.2  
 7 Lakini mwisho wa mambo yote umekaribia; basi, iweni na akili, mkeshe katika sala.
1 Pierre 1.13  1 Thessaloniciens 5.6-5.8  Jacques 5.8-5.9  1 Pierre 5.8  Marc 14.37-14.38  
 8 Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi.
Proverbes 10.12  Proverbes 17.9  Colossiens 3.14  1 Pierre 1.22  Jacques 5.20  
 9 Mkaribishane ninyi kwa ninyi, pasipo kunung’unika;
Philippiens 2.14  Hébreux 13.2  Romains 12.13  Tite 1.8  1 Timothée 3.2  
 10 kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; kama mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu.
1 Corinthiens 12.4-12.11  1 Corinthiens 4.1-4.2  Luc 19.13  Luc 12.42  Romains 12.6-12.8  
 11 Mtu akisema, na aseme kama mausia ya Mungu; mtu akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na milele. Amina.
1 Corinthiens 10.31  Romains 3.2  Actes 7.38  1 Pierre 5.11  1 Pierre 2.5  
 12 Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho.
1 Thessaloniciens 3.2-3.4  1 Pierre 1.6-1.7  2 Timothée 3.12  1 Pierre 5.9  Daniel 11.35  
 13 Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.
Romains 8.17  Jacques 1.2-1.3  Philippiens 3.10  2 Corinthiens 4.10  Romains 5.3  
 14 Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia.
1 Pierre 3.14  1 Pierre 3.16  Psaumes 146.5  Matthieu 5.11  1 Pierre 2.19-2.20  
 15 Maana mtu wa kwenu asiteswe kama mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au kama mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine.
1 Thessaloniciens 4.11  2 Thessaloniciens 3.11  1 Timothée 5.13  1 Pierre 3.17  1 Pierre 2.19-2.20  
 16 Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina hilo.
Actes 5.41  2 Timothée 1.12  Philippiens 1.29  1 Pierre 4.19  1 Pierre 3.17-3.18  
 17 Kwa maana wakati umefika wa hukumu kuanza katika nyumba ya Mungu; na ikianza kwetu sisi, mwisho wao wasioitii injili ya Mungu utakuwaje?
2 Thessaloniciens 1.8  Jérémie 25.29  Romains 2.9  1 Pierre 2.8  Ezéchiel 9.6  
 18 Na mwenye haki akiokoka kwa shida, yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi ataonekana wapi?
Proverbes 11.31  Luc 23.31  2 Pierre 3.7  2 Pierre 2.5-2.6  Ezéchiel 18.24  
 19 Basi wao wateswao kwa mapenzi ya Mungu na wamwekee amana roho zao, katika kutenda mema, kama kwa Muumba mwaminifu.
2 Timothée 1.12  1 Pierre 3.17  Psaumes 31.5  Luc 23.46  Esaïe 43.21