Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Pierre 4.5
Bible en Swahili de l’est


1 Basi kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ile ile; kwa maana yeye aliyeteswa katika mwili ameachana na dhambi.
1 Pierre 3.18 Romains 6.11 Galates 5.24 Ephésiens 6.13 Romains 6.2
2 Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.
Ephésiens 4.22-4.24 Tite 3.3-3.8 Marc 3.35 2 Corinthiens 5.15 Romains 6.11
3 Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;
1 Thessaloniciens 4.5 Ephésiens 5.18 Ezéchiel 45.9 Actes 17.30 Galates 5.19
4 mambo ambayo wao huona kuwa ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana.
1 Pierre 3.16 Jude 1.10 2 Pierre 2.22 1 Pierre 2.12 2 Pierre 2.12
5 Nao watatoa hesabu kwake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa.
Actes 10.42 2 Timothée 4.1 Jacques 5.9 Romains 14.10-14.12 Ecclésiaste 12.14
6 Maana kwa ajili hiyo hata hao waliokufa walihubiriwa Injili, ili kwamba wahukumiwe katika mwili kama wahukumiwavyo wanadamu; bali wawe hai katika roho kama Mungu alivyo hai.
Tite 3.3-3.7 Ephésiens 2.3-2.5 Romains 8.9-8.11 Romains 8.2 1 Pierre 4.1-4.2
7 Lakini mwisho wa mambo yote umekaribia; basi, iweni na akili, mkeshe katika sala.
1 Pierre 1.13 1 Pierre 5.8 1 Thessaloniciens 5.6-5.8 Jacques 5.8-5.9 Tite 2.12
8 Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi.
Proverbes 10.12 Colossiens 3.14 Proverbes 17.9 1 Pierre 1.22 Jacques 5.20
9 Mkaribishane ninyi kwa ninyi, pasipo kunung’unika;
Philippiens 2.14 Hébreux 13.2 Romains 12.13 1 Timothée 3.2 Tite 1.8
10 kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; kama mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu.
1 Corinthiens 4.1-4.2 1 Corinthiens 12.4-12.11 Luc 12.42 Romains 12.6-12.8 Tite 1.7
11 Mtu akisema, na aseme kama mausia ya Mungu; mtu akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na milele. Amina.
1 Corinthiens 10.31 1 Pierre 5.11 1 Pierre 2.5 Romains 3.2 Actes 7.38
12 Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho.
1 Thessaloniciens 3.2-3.4 1 Pierre 1.6-1.7 2 Timothée 3.12 1 Pierre 5.9 Daniel 11.35
13 Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.
Romains 8.17 Jacques 1.2-1.3 2 Corinthiens 4.10 Philippiens 3.10 2 Corinthiens 1.7
14 Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia.
1 Pierre 3.14 1 Pierre 3.16 Matthieu 5.11 Psaumes 146.5 Luc 6.22
15 Maana mtu wa kwenu asiteswe kama mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au kama mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine.
1 Thessaloniciens 4.11 2 Thessaloniciens 3.11 1 Timothée 5.13 1 Pierre 3.17 1 Pierre 2.19-2.20
16 Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina hilo.
Actes 5.41 2 Timothée 1.12 Philippiens 1.29 1 Pierre 3.17-3.18 1 Pierre 4.19
17 Kwa maana wakati umefika wa hukumu kuanza katika nyumba ya Mungu; na ikianza kwetu sisi, mwisho wao wasioitii injili ya Mungu utakuwaje?
2 Thessaloniciens 1.8 Jérémie 25.29 Romains 2.9 1 Pierre 2.8 Ezéchiel 9.6
18 Na mwenye haki akiokoka kwa shida, yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi ataonekana wapi?
Proverbes 11.31 Luc 23.31 2 Pierre 3.7 2 Pierre 2.5-2.6 Ezéchiel 18.24
19 Basi wao wateswao kwa mapenzi ya Mungu na wamwekee amana roho zao, katika kutenda mema, kama kwa Muumba mwaminifu.
1 Pierre 3.17 Psaumes 31.5 Luc 23.46 2 Timothée 1.12 Psaumes 37.5

Cette Bible est dans le domaine public.