Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jacques 5.7
Bible en Swahili de l’est


1 Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia.
Jacques 4.13 Proverbes 11.28 Esaïe 13.6 Deutéronome 8.12-8.14 Luc 6.24-6.25
2 Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo.
Job 13.28 Matthieu 6.19-6.20 Esaïe 50.9 Osée 5.12 Luc 12.33
3 Dhahabu yenu na fedha yenu zimeingia kutu, na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama moto. Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho.
Romains 2.5 Job 14.16-14.17 Josué 24.27 2 Timothée 2.17 Genèse 31.52
4 Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi.
Lévitique 19.13 Romains 9.29 Malachie 3.5 Jérémie 22.13 Genèse 4.10
5 Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa; mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo.
1 Timothée 5.6 Luc 16.19 Jérémie 12.3 Jérémie 25.34 Job 21.11-21.15
6 Mmehukumu mwenye haki mkamwua; wala hashindani nanyi.
Luc 22.51-22.53 Jacques 4.2 1 Pierre 2.22-2.23 Jean 19.9-19.11 Actes 8.32

Appel à la patience et à la foi

7 Kwa hiyo ndugu, vumilieni, hata kuja kwake Bwana. Tazama, mkulima hungoja mazao ya nchi yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho.
Deutéronome 11.14 Joël 2.23 Jérémie 5.24 Galates 6.9 Colossiens 1.11
8 Nanyi vumilieni, mthibitishe mioyo yenu, kwa maana kuja kwake Bwana kunakaribia.
1 Pierre 4.7 Psaumes 130.5 Philippiens 4.5 Psaumes 40.1-40.3 Hébreux 10.25-10.37
9 Ndugu, msinung’unikiane, msije mkahukumiwa. Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango.
Jacques 4.11 1 Corinthiens 4.5 Matthieu 24.33 Matthieu 7.1-7.2 Lévitique 19.18
10 Ndugu, watwaeni manabii walionena kwa jina la Bwana, wawe mfano wa kustahimili mabaya, na wa uvumilivu.
Hébreux 11.32-11.38 Actes 7.52 Actes 3.21 Matthieu 5.11-5.12 2 Chroniques 36.16
11 Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.
Job 1.21-1.22 Exode 34.6 Job 2.10 Psaumes 103.8 Matthieu 5.10-5.11
12 Lakini zaidi ya yote, ndugu zangu, msiape, wala kwa mbingu wala kwa nchi; wala kwa kiapo kinginecho chote; bali ndiyo yenu na iwe ndiyo, na siyo yenu iwe siyo, msije mkaangukia hukumu.
Matthieu 5.33-5.37 2 Corinthiens 1.17-1.20 1 Corinthiens 11.34 Matthieu 23.16-23.22
13 Mtu wa kwenu amepatikana na mabaya? Na aombe. Ana moyo wa kuchangamka? Na aimbe zaburi.
Psaumes 50.15 Hébreux 5.7 Ephésiens 5.19 Actes 16.24-16.25 Matthieu 26.30
14 Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.
Marc 6.13 Marc 16.18 Actes 9.40 1 Rois 17.21 Actes 28.8
15 Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.
Marc 11.22-11.24 Jacques 1.6 Jacques 5.13 1 Jean 5.14-5.16 Jacques 5.16
16 Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.
Jean 9.31 Proverbes 15.29 1 Jean 3.22 Psaumes 34.15 Matthieu 21.22
17 Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, akaomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita.
1 Rois 17.1 Actes 14.15 Luc 4.25 1 Rois 18.1 Romains 11.2
18 Akaomba tena, mbingu zikatoa mvua, nayo nchi ikazaa matunda yake.
1 Rois 18.42-18.45 1 Rois 18.18 Jérémie 14.22 Actes 14.17
19 Ndugu zangu, ikiwa mtu wa kwenu amepotelea mbali na kweli, na mtu mwingine akamrejeza;
Galates 6.1 Matthieu 18.15 Jacques 5.20 Ezéchiel 34.16 Psaumes 119.21
20 jueni ya kuwa yeye amrejezaye mwenye dhambi hata atoke katika njia ya upotevu, ataokoa roho na mauti, na kufunika wingi wa dhambi.
Proverbes 10.12 1 Pierre 4.8 Romains 11.14 1 Timothée 4.16 Proverbes 11.30

Cette Bible est dans le domaine public.