Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Hébreux 8.12
Bible en Swahili de l’est


Imperfection de l’ancienne alliance

1 Basi, katika hayo tunayosema, neno lililo kuu ndilo hili: Tunaye kuhani mkuu wa namna hii, aliyeketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Ukuu mbinguni,
Hébreux 1.3 Hébreux 2.17 Hébreux 7.26-7.28 Colossiens 3.1 Hébreux 12.2
2 mhudumu wa patakatifu, na wa ile hema ya kweli, ambayo Bwana aliiweka wala si mwanadamu.
Hébreux 9.8-9.12 Colossiens 2.11 Exode 28.1 2 Corinthiens 5.1 Hébreux 9.23-9.24
3 Maana kila kuhani mkuu huwekwa ili atoe vipawa na dhabihu; kwa hiyo lazima huyu naye awe na kitu cha kutoa.
Hébreux 5.1 Hébreux 9.14 Ephésiens 5.2 Hébreux 10.9-10.12 Tite 2.14
4 Kama angekuwa juu ya nchi, asingekuwa kuhani; maana wako watoao sadaka kama iagizavyo sheria;
Hébreux 7.11-7.15 Hébreux 5.1 Hébreux 11.4 Nombres 16.40 2 Chroniques 26.18-26.19
5 watumikiao mfano na kivuli cha mambo ya mbinguni, kama Musa alivyoagizwa na Mungu, alipokuwa tayari kuifanya ile hema; maana asema, Angalia ukavifanye vitu vyote kwa mfano ule ulioonyeshwa katika mlima.
Exode 25.40 Hébreux 10.1 Colossiens 2.17 Hébreux 9.9 Hébreux 12.25
6 Lakini sasa amepata huduma iliyo bora zaidi, kwa kadiri alivyo mjumbe wa agano lililo bora, lililoamriwa juu ya ahadi zilizo bora.
Hébreux 7.22 Hébreux 12.24 2 Corinthiens 3.6-3.11 2 Pierre 1.4 Hébreux 9.15-9.20
7 Maana kama lile la kwanza lingalikuwa halina upungufu, nafasi isingalitafutwa kwa lile la pili.
Hébreux 7.11 Hébreux 7.18 Galates 3.21 Hébreux 8.6
8 Maana, awalaumupo, asema Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, Nami nitawatimizia nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda agano jipya;
Jérémie 31.31-31.34 2 Corinthiens 3.6 Hébreux 12.24 Luc 22.20 Hébreux 10.16-10.17
9 Halitakuwa kama agano lile nililoagana na baba zao, Katika siku ile nilipowashika mikono yao niwatoe katika nchi ya Misri. Kwa sababu hawakudumu katika agano langu, Mimi nami sikuwajali asema Bwana.
Deutéronome 5.2-5.3 Jérémie 31.32 Galates 4.24 Ezéchiel 16.59 Deutéronome 31.16-31.18
10 Maana hili ndilo agano nitakaloagana na nyumba ya Israeli Baada ya siku zile, asema Bwana; Nitawapa sheria zangu katika nia zao, Na katika mioyo yao nitaziandika; Nami nitakuwa Mungu kwao, Nao watakuwa watu wangu.
Jérémie 31.33 2 Corinthiens 3.3 Ezéchiel 36.26-36.28 Ezéchiel 11.19-11.20 Hébreux 10.16-10.17
11 Nao hawatafundishana kila mtu na jirani yake, Na kila mtu na ndugu yake, akisema, Mjue Bwana; Kwa maana wote watanijua, Tangu mdogo wao hata mkubwa wao.
Esaïe 54.13 Jean 6.45 1 Jean 2.27 Jérémie 31.34 2 Chroniques 30.22
12 Kwa sababu nitawasamehe maovu yao, Na dhambi zao sitazikumbuka tena.
Romains 11.27 Esaïe 43.25 Jérémie 50.20 Hébreux 10.16-10.17 1 Jean 1.7-1.9
13 Kwa kule kusema, Agano jipya, amelifanya lile la kwanza kuwa kuukuu. Lakini kitu kianzacho kuwa kikuukuu na kuchakaa ki karibu na kutoweka.
2 Corinthiens 5.17 Hébreux 7.18-7.19 Hébreux 7.11-7.12 Hébreux 9.15 Matthieu 24.35

Cette Bible est dans le domaine public.