Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Timothée 3.8
Bible en Swahili de l’est


Conseils pour les temps difficiles

1 Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.
2 Pierre 3.3 1 Timothée 4.1-4.3 2 Timothée 4.3 Ezéchiel 38.16 Michée 4.1
2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi,
Jude 1.16 Psaumes 10.3 Philippiens 2.21 2 Pierre 2.12 2 Timothée 3.4
3 wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema,
Romains 1.31 1 Timothée 3.11 Luc 16.14 Tite 2.3 Psaumes 15.4
4 wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu;
Philippiens 3.18-3.19 1 Timothée 3.6 Romains 16.18 1 Timothée 5.6 Romains 11.20
5 wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.
Matthieu 23.27-23.28 Romains 2.20-2.24 Esaïe 29.13 Ezéchiel 33.30-33.32 1 Timothée 5.8
6 Kwa maana katika hao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu, na kuchukua mateka wanawake wajinga wenye mizigo ya dhambi, waliochukuliwa na tamaa za namna nyingi;
Jude 1.4 Jude 1.18 Tite 1.11 Tite 3.3 Matthieu 23.13
7 wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli.
Esaïe 30.10-30.11 2 Timothée 2.25 1 Timothée 2.4 2 Timothée 4.3-4.4 Jean 5.44
8 Na kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Musa, vivyo hivyo na hawa wanapingana na ile kweli; ni watu walioharibika akili zao, wamekataliwa kwa mambo ya imani.
Exode 7.11 1 Timothée 6.5 Actes 13.8-13.11 Tite 1.16 Ephésiens 4.14
9 Lakini hawataendelea sana; maana upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama vile na upumbavu wa hao ulivyokuwa dhahiri.
Exode 7.12 Exode 9.11 Jérémie 28.15-28.17 Actes 19.15-19.17 2 Timothée 3.8
10 Bali wewe umeyafuata mafundisho yangu, na mwenendo wangu, na makusudi yangu, na imani, na uvumilivu,
Philippiens 2.22 1 Timothée 4.6 1 Timothée 6.11 Tite 2.7 Daniel 1.8
11 na upendo, na saburi; tena na adha zangu na mateso, mambo yaliyonipata katika Antiokia, katika Ikonio, na katika Listra, kila namna ya adha niliyoistahimili, naye Bwana aliniokoa katika hayo yote.
Actes 13.45 Actes 14.5-14.6 Psaumes 34.19 Actes 13.14 2 Corinthiens 11.23-11.28
12 Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa.
Actes 14.22 1 Pierre 4.12-4.16 1 Pierre 2.20-2.21 Jean 15.19-15.21 1 Corinthiens 15.19
13 lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.
2 Pierre 2.20 Tite 3.3 Ezéchiel 14.9-14.10 2 Timothée 3.8 1 Timothée 4.1
14 Bali wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao;
2 Timothée 1.13 1 Thessaloniciens 2.13 2 Timothée 2.2 1 Thessaloniciens 1.5 Hébreux 10.22
15 na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu.
2 Timothée 1.5 Psaumes 119.98-119.99 2 Pierre 1.20-1.21 Romains 16.26 Actes 13.29
16 Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;
Romains 15.4 Hébreux 4.12 2 Pierre 1.19-1.21 Marc 12.24 Psaumes 19.7-19.11
17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.
2 Timothée 2.21 1 Timothée 6.11 2 Corinthiens 9.8 Hébreux 10.24 Néhémie 2.18

Cette Bible est dans le domaine public.