Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Timothée 3.12
Bible en Swahili de l’est


Conseils pour les temps difficiles

1 Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.
2 Pierre 3.3 1 Timothée 4.1-4.3 2 Timothée 4.3 Ezéchiel 38.16 Michée 4.1
2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi,
Jude 1.16 Philippiens 2.21 Psaumes 10.3 2 Pierre 2.12 Luc 16.14
3 wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema,
Romains 1.31 1 Timothée 3.11 Matthieu 10.21 Jude 1.16 2 Pierre 3.3
4 wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu;
Philippiens 3.18-3.19 1 Timothée 3.6 Romains 16.18 1 Timothée 5.6 Romains 11.20
5 wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.
Matthieu 23.27-23.28 Romains 2.20-2.24 Esaïe 29.13 Ezéchiel 33.30-33.32 Matthieu 7.15
6 Kwa maana katika hao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu, na kuchukua mateka wanawake wajinga wenye mizigo ya dhambi, waliochukuliwa na tamaa za namna nyingi;
Jude 1.4 Tite 3.3 Jude 1.18 Tite 1.11 2 Pierre 3.17
7 wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli.
Esaïe 30.10-30.11 2 Timothée 2.25 Matthieu 13.11 1 Timothée 2.4 2 Timothée 4.3-4.4
8 Na kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Musa, vivyo hivyo na hawa wanapingana na ile kweli; ni watu walioharibika akili zao, wamekataliwa kwa mambo ya imani.
Exode 7.11 1 Timothée 6.5 Actes 13.8-13.11 Tite 1.16 1 Jean 4.1
9 Lakini hawataendelea sana; maana upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama vile na upumbavu wa hao ulivyokuwa dhahiri.
Exode 7.12 Exode 9.11 Actes 13.11 Psaumes 76.10 Jérémie 28.15-28.17
10 Bali wewe umeyafuata mafundisho yangu, na mwenendo wangu, na makusudi yangu, na imani, na uvumilivu,
Philippiens 2.22 1 Timothée 4.6 1 Timothée 6.11 Tite 2.7 2 Pierre 3.11
11 na upendo, na saburi; tena na adha zangu na mateso, mambo yaliyonipata katika Antiokia, katika Ikonio, na katika Listra, kila namna ya adha niliyoistahimili, naye Bwana aliniokoa katika hayo yote.
Actes 13.45 Psaumes 34.19 Actes 14.5-14.6 Actes 13.14 2 Corinthiens 11.23-11.28
12 Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa.
Actes 14.22 1 Pierre 4.12-4.16 1 Pierre 2.20-2.21 1 Pierre 3.14 Jean 15.19-15.21
13 lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.
2 Pierre 2.20 Tite 3.3 1 Timothée 4.1 Ezéchiel 14.9-14.10 2 Timothée 3.8
14 Bali wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao;
2 Timothée 1.13 1 Thessaloniciens 2.13 2 Timothée 2.2 1 Thessaloniciens 1.5 Hébreux 10.22
15 na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu.
2 Timothée 1.5 2 Pierre 1.20-1.21 Psaumes 119.98-119.99 Actes 10.43 Luc 24.27
16 Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;
Romains 15.4 Hébreux 4.12 2 Pierre 1.19-1.21 Marc 12.24 Psaumes 19.7-19.11
17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.
2 Timothée 2.21 1 Timothée 6.11 2 Corinthiens 9.8 Hébreux 10.24 Néhémie 2.18

Cette Bible est dans le domaine public.