1 Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.
1 Timothée 4.1-4.3  2 Pierre 3.3  Ezéchiel 38.16  2 Timothée 4.3  Michée 4.1  
 2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi,
Jude 1.16  Philippiens 2.21  Psaumes 10.3  2 Pierre 2.12  2 Timothée 3.4  
 3 wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema,
Romains 1.31  1 Timothée 3.11  Daniel 8.23  1 Corinthiens 7.5  Tite 1.8  
 4 wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu;
Philippiens 3.18-3.19  1 Timothée 3.6  1 Timothée 5.6  Romains 11.20  Jude 1.8-1.9  
 5 wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.
Matthieu 23.27-23.28  Romains 2.20-2.24  Esaïe 29.13  Ezéchiel 33.30-33.32  1 Timothée 5.8  
 6 Kwa maana katika hao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu, na kuchukua mateka wanawake wajinga wenye mizigo ya dhambi, waliochukuliwa na tamaa za namna nyingi;
Jude 1.4  Jude 1.18  Tite 1.11  Tite 3.3  Marc 4.19  
 7 wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli.
2 Timothée 2.25  Esaïe 30.10-30.11  2 Timothée 4.3-4.4  Jean 5.44  Proverbes 14.6  
 8 Na kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Musa, vivyo hivyo na hawa wanapingana na ile kweli; ni watu walioharibika akili zao, wamekataliwa kwa mambo ya imani.
Exode 7.11  1 Timothée 6.5  Actes 13.8-13.11  Tite 1.16  Exode 7.22  
 9 Lakini hawataendelea sana; maana upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama vile na upumbavu wa hao ulivyokuwa dhahiri.
Exode 7.12  Exode 9.11  Jérémie 28.15-28.17  Actes 19.15-19.17  2 Timothée 3.8  
 10 Bali wewe umeyafuata mafundisho yangu, na mwenendo wangu, na makusudi yangu, na imani, na uvumilivu,1 Timothée 6.11  Philippiens 2.22  1 Timothée 4.6  Tite 2.7  2 Jean 1.9-1.10  
 11 na upendo, na saburi; tena na adha zangu na mateso, mambo yaliyonipata katika Antiokia, katika Ikonio, na katika Listra, kila namna ya adha niliyoistahimili, naye Bwana aliniokoa katika hayo yote.
Actes 13.45  Actes 14.5-14.6  Psaumes 34.19  2 Corinthiens 11.23-11.28  Actes 13.14  
 12 Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa.
Actes 14.22  1 Pierre 4.12-4.16  1 Pierre 2.20-2.21  1 Corinthiens 15.19  Tite 2.12  
 13 lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.
2 Pierre 2.20  Tite 3.3  2 Timothée 3.8  1 Timothée 4.1  Ezéchiel 14.9-14.10  
 14 Bali wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao;
2 Timothée 1.13  1 Thessaloniciens 2.13  2 Timothée 2.2  1 Thessaloniciens 1.5  Hébreux 10.22  
 15 na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu.
2 Timothée 1.5  2 Pierre 1.20-1.21  Psaumes 119.98-119.99  Proverbes 8.17  Luc 24.45  
 16 Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;
Romains 15.4  Hébreux 4.12  2 Pierre 1.19-1.21  Marc 12.24  Psaumes 19.7-19.11  
 17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.
2 Timothée 2.21  1 Timothée 6.11  2 Corinthiens 9.8  Hébreux 10.24  Néhémie 2.18