1 Basi kwa hiyo, tulipokuwa hatuwezi kuvumilia zaidi, tuliona vema kuachwa Athene peke yetu.
Actes 17.15  1 Thessaloniciens 3.5  1 Thessaloniciens 2.17  Jérémie 20.9  2 Corinthiens 2.13  
 2 Tukamtuma Timotheo ndugu yetu, mtumishi wa Mungu katika Injili ya Kristo, ili kuwafanya ninyi imara na kuwafariji kwa habari ya imani yenu;
Actes 14.22-14.23  Ephésiens 6.21-6.22  Philippiens 1.25  1 Corinthiens 16.10-16.12  1 Corinthiens 4.17  
 3 mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo.
Actes 14.22  Actes 9.16  Actes 21.13  Jean 16.33  Luc 21.12  
 4 Kwa kuwa tulipokuwapo kwenu tulitangulia kuwaambia kwamba tutapata dhiki, kama ilivyotukia, nanyi mwajua.
1 Thessaloniciens 2.14  1 Thessaloniciens 2.2  Actes 20.24  Jean 16.1-16.3  Actes 17.13  
 5 Kwa hiyo mimi nami nilipokuwa siwezi kuvumilia tena, nalituma mtu ili niijue imani yenu, asije yule mjaribu akawajaribu, na taabu yetu ikawa haina faida.
Matthieu 4.3  Philippiens 2.16  Jacques 1.13-1.14  Ephésiens 4.14  2 Corinthiens 2.11  
 6 Lakini Timotheo alipotujia hivi sasa kutoka kwenu, alituletea habari njema za imani yenu na upendo wenu, na ya kwamba mnatukumbuka vema siku zote; mkitamani kutuona sisi vile vile kama sisi kuwaona ninyi.
1 Corinthiens 11.2  1 Thessaloniciens 1.3  Proverbes 25.25  Actes 18.5  Esaïe 52.7  
 7 Kwa sababu hiyo, ndugu, tulifarijiwa kwa habari zenu, katika msiba na dhiki yetu yote, kwa imani yenu.2 Corinthiens 1.4  2 Corinthiens 7.13  2 Jean 1.4  2 Corinthiens 11.23-11.28  2 Corinthiens 7.6-7.7  
 8 Kwa kuwa sasa twaishi, ikiwa ninyi mnasimama imara katika Bwana.
1 Corinthiens 16.13  Colossiens 1.23  Actes 11.23  Ephésiens 3.17  1 Pierre 5.10  
 9 Maana ni shukrani gani tuwezayo kumlipa Mungu kwa ajili yenu, kwa furaha ile yote tunayoifurahia, kwa sababu yenu mbele za Mungu wetu;
2 Corinthiens 9.15  1 Thessaloniciens 1.2-1.3  2 Corinthiens 2.14  2 Samuel 7.18-7.20  1 Thessaloniciens 3.7-3.8  
 10 usiku na mchana tunapoomba kwa juhudi tupate kuwaona nyuso zenu, na kuyatengeneza mapungufu ya imani yenu?
2 Timothée 1.3  2 Corinthiens 13.9  Romains 1.10-1.12  2 Corinthiens 1.24  1 Thessaloniciens 2.17-2.18  
 11 Basi Mungu mwenyewe, Baba yetu, na Bwana wetu Yesu, atuongoze njia yetu tufike kwenu.
2 Thessaloniciens 2.16  Proverbes 3.5-3.6  1 Thessaloniciens 3.13  Matthieu 6.14  Esaïe 63.16  
 12 Bwana na awaongeze na kuwazidisha katika upendo, ninyi kwa ninyi, na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tulivyo kwenu;
Philippiens 1.9  2 Thessaloniciens 1.3  1 Thessaloniciens 4.9-4.10  1 Thessaloniciens 5.15  1 Jean 3.11-3.19  
 13 apate kuifanya imara mioyo yenu iwe bila lawama katika utakatifu mbele za Mungu, Baba yetu, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu pamoja na watakatifu wake wote.
1 Thessaloniciens 5.23  1 Thessaloniciens 2.19  Colossiens 1.22  Ephésiens 5.27  1 Corinthiens 1.7-1.8