Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Philippiens 4.21
Bible en Swahili de l’est


1 Basi, ndugu zangu, wapendwa wangu, ninaowaonea shauku, furaha yangu, na taji yangu, hivyo simameni imara katika Bwana, wapenzi wangu.
Philippiens 1.27 1 Corinthiens 16.13 Philippiens 1.8 1 Corinthiens 15.58 Philippiens 2.16

Recommandations diverses

2 Namsihi Euodia, namsihi na Sintike, wawe na nia moja katika Bwana.
Hébreux 12.14 1 Thessaloniciens 5.13 1 Pierre 3.8-3.11 Philippiens 2.2-2.3 Genèse 45.24
3 Naam, nataka na wewe pia, mjoli wa kweli, uwasaidie wanawake hao; kwa maana waliishindania Injili pamoja nami, na Klementi naye, na wale wengine waliotenda kazi pamoja nami, ambao majina yao yamo katika kitabu cha uzima.
Luc 10.20 Apocalypse 3.5 Apocalypse 13.8 Apocalypse 21.27 Philippiens 2.20-2.25
4 Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.
Philippiens 3.1 Romains 12.12 1 Thessaloniciens 5.16-5.18 Matthieu 5.12 1 Pierre 4.13
5 Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
Jacques 5.8-5.9 Matthieu 6.25 Tite 3.2 Matthieu 6.34 Luc 6.29-6.35
6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
Matthieu 6.25-6.33 Proverbes 3.5-3.6 1 Pierre 5.7 Psaumes 34.5-34.7 Matthieu 7.7-7.8
7 Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.
Jean 14.27 Colossiens 3.15 Esaïe 26.3 Jean 16.33 Romains 15.13
8 Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.
Jacques 3.17 Tite 2.7 Romains 12.9-12.21 1 Timothée 4.12 2 Pierre 1.3-1.7
9 Mambo mliyojifunza kwangu na kuyapokea, na kuyasikia na kuyaona kwangu, yatendeni hayo; na Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.
Philippiens 3.17 Philippiens 4.7 Romains 15.33 2 Pierre 1.10 Matthieu 7.24-7.27

Reconnaissance et salutations

10 Nalifurahi sana katika Bwana, kwa kuwa sasa mwisho mmehuisha tena fikira zenu kwa ajili yangu, kama vile mlivyokuwa mkinifikiri hali yangu lakini hamkupata nafasi.
2 Corinthiens 11.9 Galates 6.10 2 Corinthiens 7.6-7.7 Galates 6.6 Philippiens 2.30
11 Si kwamba nasema haya kwa kuwa nina mahitaji; maana nimejifunza kuwa radhi na hali yo yote niliyo nayo.
1 Timothée 6.6-6.9 Matthieu 6.31-6.34 Hébreux 13.5-13.6 Philippiens 3.8 2 Corinthiens 9.8
12 Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa.
2 Corinthiens 11.27 2 Corinthiens 11.9 2 Corinthiens 12.7-12.10 2 Corinthiens 6.4-6.10 Matthieu 11.29
13 Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
Esaïe 41.10 2 Corinthiens 12.9-12.10 Colossiens 1.11 Ephésiens 6.10 Esaïe 40.29-40.31
14 Lakini mlifanya vema, mliposhiriki nami katika dhiki yangu.
Philippiens 1.7 Hébreux 13.16 1 Corinthiens 9.10-9.11 Hébreux 10.34 Apocalypse 1.9
15 Nanyi pia, ninyi wenyewe mnajua, enyi Wafilipi, ya kuwa katika mwanzo wa Injili, nilipotoka Makedonia, hakuna kanisa lingine lililoshirikiana nami katika habari hii ya kutoa na kupokea, ila ninyi peke yenu.
Philippiens 1.5 2 Corinthiens 11.8-11.12 2 Rois 5.16 2 Corinthiens 12.11-12.15 Actes 16.40-17.5
16 Kwa kuwa hata huko Thesalonike mliniletea msaada kwa mahitaji yangu, wala si mara moja.
1 Thessaloniciens 2.9 1 Thessaloniciens 2.18 Actes 17.1
17 Si kwamba nakitamani kile kipawa, bali nayatamani mazao yanayozidi kuwa mengi, katika hesabu yenu.
Tite 3.14 Hébreux 6.10 Tite 1.7 Luc 14.12-14.14 1 Corinthiens 9.11-9.15
18 Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa tele; nimepokea kwa mkono wa Epafrodito vitu vile vilivyotoka kwenu, harufu ya manukato, sadaka yenye kibali, impendezayo Mungu.
Philippiens 4.12 Hébreux 13.16 Philippiens 2.25-2.26 Ephésiens 5.2 2 Corinthiens 9.12
19 Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.
2 Corinthiens 9.8-9.11 Psaumes 84.11 1 Timothée 6.17 Psaumes 23.1-23.5 1 Pierre 5.10
20 Sasa atukuzwe Mungu, Baba yetu, milele na milele. Amina.
Romains 11.36 Galates 1.4-1.5 Apocalypse 7.12 Psaumes 72.19 Apocalypse 14.7
21 Mnisalimie kila mtakatifu katika Kristo Yesu. Ndugu walio pamoja nami wawasalimu.
Galates 1.2 Romains 16.21-16.22 Galates 2.3 Philémon 1.23-1.24 1 Corinthiens 1.2
22 Watakatifu wote wawasalimu, hasa wao walio wa nyumbani mwa Kaisari.
2 Corinthiens 13.13 Philippiens 1.13 Hébreux 13.24 3 Jean 1.14 Romains 16.16
23 Neema ya Bwana Yesu Kristo na iwe pamoja na roho zenu.
Romains 16.20 Romains 16.23 2 Corinthiens 13.14

Cette Bible est dans le domaine public.