Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 9.26
Bible en Swahili de l’est


Souvenir des rébellions d’Israël

1 Sikiza, Ee Israeli; hivi leo unataka kuvuka Yordani uingie kwa kuwamiliki mataifa yaliyo makubwa, na yenye nguvu kukupita wewe, miji mikubwa iliyojengewa kuta hata mbinguni,
Deutéronome 4.38 Deutéronome 1.28 Deutéronome 11.31 Deutéronome 11.23 Josué 1.11
2 watu wakubwa, warefu, wana wa Waanaki, uwajuao, uliokuwa ukisikia wakitajwa hivi, Ni nani awezaye kusimama mbele ya wana wa Anaki?
Nombres 13.22 Nombres 13.33 Daniel 8.4 Nahum 1.6 Deutéronome 7.24
3 Basi jua siku hii ya leo kuwa Bwana, Mungu wako, ndiye atanguliaye kuvuka mbele yako kama moto uteketezao; atawaangamiza, tena atawaangusha mbele yako; ndivyo utakavyowafukuza na kuwapoteza upesi, kama alivyokuambia Bwana.
Exode 23.29-23.31 Deutéronome 4.24 Josué 3.11 Hébreux 12.29 Deutéronome 7.23-7.24
4 Usiseme moyoni mwako, Bwana, Mungu wako, atakapokwisha kuwasukumia nje mbele yako, ukasema, Ni kwa haki yangu alivyonitia Bwana niimiliki nchi hii; kwani ni kwa ajili ya uovu wa mataifa haya Bwana awafukuza nje mbele yako.
Deutéronome 8.17 Deutéronome 12.31 Ezéchiel 36.22 Genèse 15.16 Deutéronome 18.9-18.14
5 Si kwa haki yako, wala kwa unyofu wa moyo wako, hivi uingiavyo kuimiliki nchi yao; lakini ni kwa uovu wa mataifa haya Bwana, Mungu wako, awafukuza nje mbele yako; tena apate kuliweka imara hilo neno Bwana alilowaapia baba zako Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo.
Tite 3.5 Genèse 12.7 Genèse 26.4 Genèse 15.7 Genèse 13.15
6 Basi jua ya kuwa Bwana, Mungu wako, hakupi nchi hii nzuri uimiliki kwa ajili ya haki yako, kwa maana u taifa lenye shingo ngumu.
Deutéronome 31.27 Deutéronome 9.13 Deutéronome 10.16 Exode 32.9 2 Chroniques 30.8
7 Kumbuka, usisahau ulivyomtia Bwana, Mungu wako, kasirani jangwani; tangu siku uliyotoka nchi ya Misri hata mlipofika mahali hapa, mmekuwa na uasi juu ya Bwana
Nombres 11.4 Nombres 25.2 Exode 16.2 Deutéronome 31.27 Exode 14.11
8 Tena mlimkasirisha Bwana katika Horebu, Bwana akakasirika nanyi hata akataka kuwaangamiza.
Exode 32.7-32.10 Exode 32.16 Psaumes 106.19-106.22
9 Na hapo nilipokwea mlimani kwenda kuzipokea mbao za mawe, nazo ni mbao za agano Bwana alilofanya nanyi, ndipo nikakaa mle mlimani siku arobaini usiku na mchana; sikula chakula wala kunywa maji.
Exode 34.28 Exode 24.18 Exode 24.15 1 Rois 19.8 Exode 24.12
10 Bwana akanipa zile mbao mbili za mawe zimeandikwa kwa kidole cha Mungu; na juu yake yameandikwa maneno mfano wa yote aliyosema nanyi Bwana mle mlimani toka kati ya moto siku ya mkutano.
Exode 31.18 Deutéronome 18.16 Deutéronome 10.4 Exode 20.1-20.18 Hébreux 8.10
11 Ikawa mwisho wa siku arobaini usiku na mchana, Bwana alinipa zile mbao mbili za mawe, nazo ni mbao za agano.
Deutéronome 9.9 Nombres 10.33 Hébreux 8.6-8.10 Hébreux 9.4
12 Bwana akaniambia, Ondoka huko, shuka upesi; kwa kuwa watu wako uliowatoa Misri wamejiharibu; wamekengeuka mara katika njia niliyowaamuru; wamejifanyia sanamu ya kusubu.
Exode 32.7-32.8 Juges 2.17 Deutéronome 31.29 Galates 1.6 Psaumes 78.57
13 Tena Bwana akasema nami zaidi, akaniambia, Nimeliona taifa hili; na tazama, ni taifa lenye shingo ngumu;
Deutéronome 9.6 Deutéronome 10.16 2 Rois 17.14 Deutéronome 31.27 Genèse 11.5
14 niache, nipate kuwaangamiza, na kulifuta jina lao chini ya mbingu; nami nitakufanya wewe uwe taifa kubwa lenye nguvu kuwapita wao.
Deutéronome 29.20 Psaumes 109.13 Exode 32.10-32.13 Psaumes 9.5 Proverbes 10.7
15 Basi nikageuka nikashuka mle mlimani, mlima ukawaka moto; na zile mbao mbili za agano zilikuwa katika mikono yangu miwili.
Exode 19.18 Deutéronome 4.11 Deutéronome 5.23 Exode 32.14-32.35 Exode 9.23
16 Nikaangalia, na tazama, mlikuwa mmefanya dhambi juu ya Bwana, Mungu wenu; mmefanya ndama ya ng’ombe ya kusubu; mmekengeuka upesi katika njia aliyowaamuru Bwana.
Exode 32.19 Actes 7.40-7.41
17 Nikazishika zile mbao mbili, nikazitupa kutoka katika mikono yangu miwili, nikazivunja mbele ya macho yenu.
18 Nikaanguka nchi mbele za Bwana siku arobaini usiku na mchana, kama pale kwanza; sikula chakula wala kunywa maji; kwa sababu ya makosa yenu yote mliyokosa, kwa kufanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, kwa kumkasirisha.
Exode 34.28 Deutéronome 9.9 Psaumes 106.23 2 Samuel 12.16 Deutéronome 10.10
19 Kwa kuwa niliogopa hasira na makamio aliyowakasirikia Bwana kutaka kuwaangamiza. Lakini Bwana alinisikiza wakati huo nao.
Deutéronome 10.10 Exode 32.14 Exode 32.10-32.11 Exode 33.17 Psaumes 99.6
20 Bwana akamkasirikia sana Haruni akataka kumwangamiza; nikamwombea Haruni naye wakati huo.
Exode 32.21 Exode 32.35 Exode 32.2-32.5 Hébreux 7.26-7.28
21 Kisha nikaitwaa ile dhambi yenu, huyo ndama mliyemfanya, nikamteketeza kwa moto, nikamponda, nikamsaga tikitiki, hata akawa laini kama vumbi; nikalitupa vumbi lake katika kijito kilichoshuka kutoka mlimani.
Exode 32.20 Osée 8.11 Esaïe 2.18-2.21 Esaïe 30.22 Esaïe 31.7
22 Tena huko Tabera, na Masa, na Kibroth-hataava mlimtia Bwana hasira.
Nombres 11.34 Exode 17.7 Nombres 11.1-11.5
23 Na wakati alipowatuma Bwana kutoka Kadesh-barnea, akiwaambia, Kweeni mkaimiliki nchi niliyowapa; ndipo mkaasi juu ya maagizo ya Bwana, Mungu wenu, hamkumsadiki wala hamkusikiza sauti yake.
Psaumes 106.24-106.25 Esaïe 63.10 Hébreux 4.2 Psaumes 78.22 Hébreux 3.18-3.19
24 Mmekuwa na uasi juu ya Bwana tokea siku nilipowajua ninyi.
Deutéronome 31.27 Actes 7.51 Deutéronome 9.6-9.7
25 Ndipo nikaanguka nchi mbele za Bwana siku zile arobaini usiku na mchana nilizokuwa nimeanguka nchi; kwa kuwa Bwana alisema atawaangamiza.
Deutéronome 9.18 Deutéronome 9.16
26 Nikamwomba Bwana, nikasema, Ee Bwana Mungu, usiwaangamize watu wako, urithi wako, uliowakomboa kwa ukuu wako, uliowatoa Misri kwa mkono wa nguvu.
Exode 32.11-32.13 Jérémie 14.21 Deutéronome 32.9 Exode 15.13 Psaumes 77.15
27 Wakumbuke watumwa wako, Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo; usiangalie upotofu wa watu hawa, wala uovu wao, wala dhambi yao;
1 Samuel 25.25 Psaumes 78.8 Jérémie 50.20 Exode 13.5 Michée 7.18-7.19
28 isije nchi uliyotutoa ikasema, Ni kwa sababu Bwana hakuweza kuwaleta katika nchi aliyowapa ahadi, tena ni kwa kuwa aliwachukia, alivyowatoa nje ili kuwaua jangwani.
Nombres 14.16 Exode 32.12
29 Nao ni watu wako, urithi wako, uliowatoa kwa nguvu zako kuu na mkono wako ulionyoka.
Deutéronome 4.20 Néhémie 1.10 Deutéronome 9.26 Deutéronome 4.34 Psaumes 95.7

Cette Bible est dans le domaine public.