Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 30.16
Bible en Swahili de l’est


Promesses et menaces

1 Tena itakuwa, mambo haya yote yatakapokujilia, baraka na laana nilizoweka mbele yako, nawe utakapozikumbuka kati ya mataifa yote, huko atakakokupeleka Bwana, Mungu wako,
Deutéronome 30.19 Deutéronome 30.15 1 Rois 8.47-8.48 Deutéronome 28.64 Deutéronome 11.26-11.28
2 nawe utakapomrudia Bwana, Mungu wako, na kuitii sauti yake, mfano wa yote nikuagizayo leo, wewe na wanao, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote;
Néhémie 1.9 Joël 2.12-2.13 Lamentations 3.40 Lamentations 3.32 Ephésiens 6.24
3 ndipo Bwana, Mungu wako, atakapougeuza utumwa wako, naye atakuhurumia, tena atarejea na kukukusanya kutoka mataifa yote, huko alikokutawanyia Bwana, Mungu wako.
Jérémie 29.14 Psaumes 147.2 Ezéchiel 34.12-34.13 Lamentations 3.32 Ezéchiel 36.24
4 Watu wako waliotawanyika wakiwako katika ncha za mbingu za mwisho, kutoka huko atakukusanya Bwana, Mungu wako; kutoka huko atakutwaa;
Néhémie 1.9 Deutéronome 28.64 Esaïe 43.6 Esaïe 11.11-11.16 Sophonie 3.19-3.20
5 atakuleta Bwana, Mungu wako, uingie nchi waliyomiliki baba zako, nawe utaimiliki; naye atakutendea mema, na kukufanya uwe watu wengi kuliko baba zako.
Jérémie 29.14
6 Bwana, Mungu wako, atautahiri moyo wako, na moyo wa uzao wako, ili umpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, upate kuwa hai.
Deutéronome 10.16 Ezéchiel 36.26-36.27 Jérémie 32.39 Jérémie 4.4 Ezéchiel 11.19-11.20
7 Na laana hizi zote Bwana, Mungu wako, atawatia adui zako na hao wakuchukiao, waliokuwa wakikutesa.
Lamentations 4.21-4.22 Ezéchiel 25.6 Ezéchiel 25.15 Abdias 1.10 Amos 1.6
8 Nawe utarudi, uitii sauti ya Bwana, na kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo.
Romains 11.26-11.27 Esaïe 1.25-1.26 Proverbes 16.1 Ezéchiel 11.19-11.20 Ephésiens 2.16
9 Na Bwana, Mungu wako, atakufanya uwe na wingi wa uheri katika kazi yote ya mkono wako, katika uzao wa tumbo lako, na katika uzao wa ng’ombe wako, na katika uzao wa nchi yako; kwa kuwa Bwana atafurahi tena juu yako kwa wema, kama alivyofurahi juu ya baba zako;
Jérémie 32.41 Jean 15.11 Deutéronome 28.11-28.14 Lévitique 26.6 Sophonie 3.17
10 ukiwa utaifuata sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa kuyashika maagizo yake, na amri zake zilizoandikwa katika chuo hiki cha torati; ukimwelekea Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote.
Ezéchiel 33.14 Ezéchiel 33.11 Deutéronome 30.8 Deutéronome 30.2 Actes 26.20
11 Kwa maana maagizo haya nikuagizayo leo, si mazito mno kwako, wala si mbali.
Esaïe 45.19 Psaumes 147.19-147.20 Colossiens 1.26-1.27 Romains 16.25-16.26
12 Si mbinguni, hata useme, Ni nani atakayetupandia mbinguni akatuletee, aje atuambie tusikie, tupate kuyafanya?
Romains 10.6-10.8 Proverbes 30.4 Jean 3.13
13 Wala si ng’ambo ya pili ya bahari, hata useme, Ni nani atakayetuvukia bahari, akatuletee, aje atuambie, tusikie, tupate kuyafanya?
Actes 10.33 Matthieu 12.42 Actes 8.27-8.40 Proverbes 3.13-3.18 Jean 6.27
14 Lakini neno li karibu nawe sana, li katika kinywa chako na moyo wako, upate kulifanya.
Romains 10.8-10.10 Jérémie 12.2 Luc 10.11-10.12 Actes 13.26 Actes 28.23-28.28
15 Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya;
Deutéronome 11.26 Deutéronome 30.19 Galates 5.6 Deutéronome 32.47 Galates 3.13-3.14
16 kwa hivi nikuagizavyo leo kumpenda Bwana, Mungu wako, kuenenda katika njia zake, na kushika maagizo yake, na amri zake, na hukumu zake, upate kuwa hai na kuongezeka; Bwana, Mungu wako, apate kukubarikia katika nchi uingiayo kuimiliki.
Deutéronome 30.6 1 Corinthiens 7.19 Jean 14.21 1 Jean 5.2-5.3 Deutéronome 6.5
17 Lakini moyo wako ukikengeuka, usipotaka kusikiza, lakini ukavutwa kando kwenda kuabudu miungu mingine, na kuitumikia;
Hébreux 3.12 2 Timothée 4.4 Deutéronome 17.17 Proverbes 1.32 Deutéronome 29.18-29.28
18 nawahubiri hivi leo hakika mtaangamia; hamtazifanya siku zenu kuwa nyingi juu ya nchi, uivukiayo Yordani, uingie kuimiliki.
Esaïe 63.17-63.18 Deutéronome 8.19-8.20 Deutéronome 4.26 Deutéronome 31.29 Josué 23.15-23.16
19 Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako;
Deutéronome 30.15 Deutéronome 11.26 Deutéronome 30.1 Proverbes 8.36 Deutéronome 4.26
20 kumpenda Bwana, Mungu wako, kuitii sauti yake, na kushikamana naye; kwani hiyo ndiyo uzima wako, na wingi wa siku zako; upate kukaa katika nchi Bwana aliyowaapia baba zako, Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kuwa atawapa.
Deutéronome 10.20 Actes 17.28 Actes 17.25 Psaumes 27.1 Josué 23.8

Cette Bible est dans le domaine public.