Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 14.26
Bible en Swahili de l’est


Lois sur les animaux purs et impurs

1 Ninyi mmekuwa wana wa Bwana, Mungu wenu; msijitoje miili yenu, wala msifanye upaa katikati ya macho yenu kwa ajili ya aliyekufa.
Jérémie 41.5 Romains 9.8 Galates 3.26 Lévitique 21.5 Jérémie 16.6
2 Kwa kuwa u taifa takatifu kwa Bwana, Mungu wako, na Bwana amekuchagua kuwa watu wake hasa, kuliko mataifa yote yaliyo juu ya uso wa nchi.
Deutéronome 7.6 Lévitique 20.26 Deutéronome 26.18-26.19 Exode 19.5-19.6 1 Pierre 2.9
3 Usile kitu cho chote kichukizacho.
Ezéchiel 4.14 Lévitique 11.43 Esaïe 65.4 Actes 10.12-10.14 Lévitique 20.25
4 Wanyama mtakaokula ni hawa ng’ombe, na kondoo, na mbuzi,
Actes 10.14 1 Rois 4.23 Lévitique 11.2-11.45
5 kulungu, na paa, na kongoni, na mbuzi wa mwitu, na paa mweupe, na pofu, na mbuzi wa mlima;
6 na kila mnyama aliyepasuliwa ukwato, ukapasuka ukwato wake zikawa mbili, naye ni mnyama mwenye kucheua akatafuna tena, katika wanyama wote, ndiye mnyama mtakayemla.
Psaumes 1.1-1.2 Proverbes 18.1 2 Corinthiens 6.17
7 Lakini, hawa msile katika wale wenye kucheua, na hao waliopasuliwa ukwato; ngamia, na sungura, na kwang’a, kwa kuwa hucheua, lakini hawakupasuliwa kwato, ni najisi kwenu;
Lévitique 11.5 2 Timothée 3.5 2 Pierre 2.18-2.22 Matthieu 7.26 Tite 1.16
8 na nguruwe, kwa kuwa amepasuliwa ukwato lakini hacheui, huyu ni najisi kwenu msile nyama zao, wala mizoga yao msiiguse.
Lévitique 11.26-11.27 Esaïe 66.17 Luc 15.15-15.16 Esaïe 66.3 2 Pierre 2.22
9 Mtakula hawa katika wote walio majini; kila kilicho na mapezi na magamba mtakula;
Lévitique 11.9-11.12
10 na kila kisichokuwa na mapezi na magamba msile; ni najisi kwenu.
11 Mna ruhusa kula katika nyuni wote walio safi.
12 Lakini hawa msiwale; tai, na furukombe, na kipungu;
Lévitique 11.13-11.19
13 na kengewa, na kozi, na mwewe kwa aina zake;
14 na kila kunguru kwa aina zake;
15 na mbuni, na kirukanjia, na dudumizi, na kipanga kwa aina zake;
Job 30.29
16 na bundi, na mumbi, na bundi mkubwa;
17 na mwari, na nderi, na mnandi;
18 na membe, na koikoi, kwa aina zake; na hudihudi, na popo.
19 Na wadudu wote watambaao wenye mabawa ni najisi kwenu; msiwale.
Philippiens 3.19 Lévitique 11.20-11.23
20 Mna ruhusa kula katika nyuni wote walio safi.
21 Msile nyamafu yo yote; waweza kumpa mgeni aliye ndani ya malango yako, ili apate kula; au kumliza mtu wa mataifa; kwa kuwa wewe u taifa takatifu kwa Bwana, Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mamaye.
Exode 23.19 Exode 34.26 Deutéronome 14.2 Lévitique 22.8 Lévitique 17.15

Les dîmes

22 Usiache kutoa zaka ya fungu la kumi katika maongeo yote ya mbegu zako, yatokayo shamba mwaka baada ya mwaka.
Deutéronome 12.17 Néhémie 10.37 Deutéronome 12.6 Nombres 18.21 Lévitique 27.30-27.33
23 Nawe utakula mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua apakalishe jina lake, zaka ya nafaka zako, na divai yako, na mafuta yako, na wazaliwa wa kwanza wa makundi yako ya ng’ombe na ya kondoo; ili upate kujifunza kumcha Bwana, Mungu wako, daima.
Deutéronome 4.10 Deutéronome 12.5-12.7 Deutéronome 12.17-12.18 Deutéronome 15.19-15.20
24 Na njia ikiwa ndefu mno nawe, usiweze kuzichukua kwa kuwa mahali ni mbali nawe mno atakapochagua Bwana, Mungu wako, apakalishe jina lake, hapo atakapokubarikia Bwana, Mungu wako;
Deutéronome 12.21 Deutéronome 12.5 Deutéronome 11.24 Exode 23.31
25 ndipo uzibadili ziwe fedha, na kufunga zile fedha uende nazo mkononi mwako, hata mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako;
26 na zile fedha zitumie kwa cho chote itakachotamani roho yako, ng’ombe, au kondoo, au divai, au kileo, au roho yako itakacho kwako cho chote; nawe utakula huko mbele za Bwana, Mungu wako; tena furahi, wewe na nyumba yako;
Deutéronome 12.7 Ecclésiaste 9.7 Marc 11.15 Deutéronome 12.18 Psaumes 106.14
27 na Mlawi aliye ndani ya malango yako usimwache, kwani hana fungu wala urithi pamoja nawe.
Nombres 18.20 Deutéronome 14.29 Deutéronome 12.12 Deutéronome 18.1-18.2 Galates 6.6
28 Kila mwaka wa tatu, mwisho wake, toa fungu la kumi lote la maongeo yako ya mwaka huo, uliweke ndani ya malango yako;
Deutéronome 14.22 Amos 4.4 Deutéronome 26.12-26.15
29 na Mlawi kwa kuwa hana fungu wala urithi pamoja nawe, na mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe, walio ndani ya malango yako, na waje wale na kushiba; ili kwamba Bwana, Mungu wako, akubarikie katika kazi yote ya mkono wako uifanyayo.
Deutéronome 14.27 Deutéronome 15.10 Proverbes 19.17 Deutéronome 16.11 Deutéronome 16.14

Cette Bible est dans le domaine public.