Rôle de Paul
 1 Kwa sababu hiyo mimi Paulo ni mfungwa wake Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi Mataifa;
Colossiens 1.24  Ephésiens 4.1  Philémon 1.9  Philippiens 1.7  Philippiens 1.13-1.16  
 2 ikiwa mmesikia habari ya uwakili wa neema ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu;
2 Timothée 1.11  Ephésiens 4.7  Romains 1.5  Actes 13.46  Galates 1.13  
 3 ya kwamba kwa kufunuliwa nalijulishwa siri hiyo, kama nilivyotangulia kuandika kwa maneno machache.
Ephésiens 3.9  Romains 16.25  Galates 1.12  Actes 22.17  Actes 22.21  
 4 Kwa hayo, myasomapo, mtaweza kuutambua ufahamu wangu katika siri yake Kristo.
2 Corinthiens 11.6  1 Corinthiens 4.1  Colossiens 4.3  1 Corinthiens 2.6-2.7  1 Timothée 3.16  
 5 Siri hiyo hawakujulishwa wanadamu katika vizazi vingine; kama walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi katika Roho;
Jude 1.17  2 Pierre 3.2  Actes 10.28  Ephésiens 2.20  Tite 1.1-1.3  
 6 ya kwamba Mataifa ni warithi pamoja nasi wa urithi mmoja, na wa mwili mmoja, na washiriki pamoja nasi wa ahadi yake iliyo katika Kristo Yesu kwa njia ya Injili;
Romains 8.15-8.17  Galates 3.14  1 Corinthiens 12.27  Ephésiens 2.13-2.22  1 Jean 1.3  
 7 Injili hiyo ambayo nalifanywa mhudumu wake, kwa kadiri ya kipawa cha neema ya Mungu niliyopewa kwa kadiri ya utendaji wa uweza wake.
Ephésiens 1.19  Ephésiens 3.20  Ephésiens 3.2  1 Corinthiens 3.5  Romains 1.5  
 8 Mimi, niliye mdogo kuliko yeye aliye mdogo wa watakatifu wote, nalipewa neema hii ya kuwahubiri Mataifa utajiri wake Kristo usiopimika;
1 Corinthiens 15.9  1 Timothée 1.13  1 Timothée 2.7  2 Timothée 1.11  Colossiens 2.1-2.3  
 9 na kuwaangaza watu wote wajue habari za madaraka ya siri hiyo, ambayo tangu zamani zote ilisitirika katika Mungu aliyeviumba vitu vyote;
Colossiens 1.26  Jean 10.30  Matthieu 13.35  2 Timothée 1.9  Romains 16.25-16.26  
 10 ili sasa, kwa njia ya kanisa, hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi ijulikane na falme na mamlaka katika ulimwengu wa roho;
1 Pierre 1.12  1 Corinthiens 2.7  Ephésiens 1.3  Romains 11.33  Ephésiens 1.21  
 11 kwa kadiri ya kusudi la milele alilolikusudia katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Ephésiens 1.11  2 Timothée 1.9  Romains 8.28-8.30  Esaïe 14.24-14.27  Romains 9.11  
 12 Katika yeye tunao ujasiri na uwezo wa kukaribia katika tumaini kwa njia ya kumwamini.
Ephésiens 2.18  Hébreux 4.14-4.16  Jean 14.6  Romains 5.2  Hébreux 10.19-10.22  
 13 Basi naomba msikate tamaa kwa sababu ya dhiki zangu kwa ajili yenu, zilizo utukufu kwenu.
Colossiens 1.24  Ephésiens 3.1  2 Corinthiens 1.6  Esaïe 40.30-40.31  Philippiens 1.12-1.14  
Prière de Paul pour les Éphésiens
 14 Kwa hiyo nampigia Baba magoti,
Actes 21.5  Ephésiens 1.16-1.19  Psaumes 95.6  1 Rois 8.54  Esaïe 45.23  
 15 ambaye kwa jina lake ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa,
Ephésiens 1.21  Ephésiens 1.10  Apocalypse 5.8-5.14  Jérémie 33.16  Philippiens 2.9-2.11  
 16 awajalieni, kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake, kufanywa imara kwa nguvu, kwa kazi ya Roho wake katika utu wa ndani.
Colossiens 1.11  Philippiens 4.13  Esaïe 40.29-40.31  Zacharie 10.12  2 Timothée 4.17  
 17 Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani mkiwa na shina na msingi katika upendo;
Colossiens 2.7  Jean 14.23  Colossiens 1.23  Galates 2.20  1 Jean 4.16  
 18 ili mpate kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, na urefu, na kimo, na kina;Psaumes 103.11-103.12  Ephésiens 1.15  Galates 2.20  1 Timothée 1.14-1.16  Philippiens 3.8-3.10  
 19 na kuujua upendo wake Kristo, upitao ufahamu kwa jinsi ulivyo mwingi, mpate kutimilika kwa utimilifu wote wa Mungu.
Ephésiens 1.23  Colossiens 1.10  Colossiens 2.9-2.10  1 Jean 4.9-4.14  Ephésiens 5.2  
 20 Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu;
2 Corinthiens 9.8  Romains 4.21  Jude 1.24  1 Corinthiens 2.9  Ephésiens 1.19  
 21 naam, atukuzwe katika Kanisa na katika Kristo Yesu hata vizazi vyote vya milele na milele. Amina.
Romains 11.36  Jude 1.25  1 Pierre 5.11  Romains 16.27  Philippiens 4.20