Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ephésiens 3.17
Bible en Swahili de l’est


Rôle de Paul

1 Kwa sababu hiyo mimi Paulo ni mfungwa wake Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi Mataifa;
Colossiens 1.24 Ephésiens 4.1 Philémon 1.9 2 Timothée 1.8 Ephésiens 6.20
2 ikiwa mmesikia habari ya uwakili wa neema ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu;
2 Timothée 1.11 Ephésiens 4.7 Romains 1.5 Actes 22.21 Ephésiens 1.10
3 ya kwamba kwa kufunuliwa nalijulishwa siri hiyo, kama nilivyotangulia kuandika kwa maneno machache.
Ephésiens 3.9 Romains 16.25 Actes 22.17 Galates 1.12 Actes 22.21
4 Kwa hayo, myasomapo, mtaweza kuutambua ufahamu wangu katika siri yake Kristo.
2 Corinthiens 11.6 Colossiens 4.3 1 Corinthiens 4.1 Ephésiens 6.19 1 Corinthiens 2.6-2.7
5 Siri hiyo hawakujulishwa wanadamu katika vizazi vingine; kama walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi katika Roho;
Jude 1.17 2 Pierre 3.2 Actes 10.28 Ephésiens 2.20 Tite 1.1-1.3
6 ya kwamba Mataifa ni warithi pamoja nasi wa urithi mmoja, na wa mwili mmoja, na washiriki pamoja nasi wa ahadi yake iliyo katika Kristo Yesu kwa njia ya Injili;
Galates 3.14 Romains 8.15-8.17 Galates 4.5-4.7 Colossiens 2.19 Ephésiens 5.30
7 Injili hiyo ambayo nalifanywa mhudumu wake, kwa kadiri ya kipawa cha neema ya Mungu niliyopewa kwa kadiri ya utendaji wa uweza wake.
Ephésiens 1.19 Ephésiens 3.20 Ephésiens 3.2 1 Timothée 1.14-1.15 2 Corinthiens 3.6
8 Mimi, niliye mdogo kuliko yeye aliye mdogo wa watakatifu wote, nalipewa neema hii ya kuwahubiri Mataifa utajiri wake Kristo usiopimika;
1 Corinthiens 15.9 1 Timothée 1.13 1 Timothée 2.7 2 Timothée 1.11 Romains 12.10
9 na kuwaangaza watu wote wajue habari za madaraka ya siri hiyo, ambayo tangu zamani zote ilisitirika katika Mungu aliyeviumba vitu vyote;
Colossiens 1.26 Jean 10.30 Matthieu 13.35 2 Timothée 1.9 Romains 16.25-16.26
10 ili sasa, kwa njia ya kanisa, hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi ijulikane na falme na mamlaka katika ulimwengu wa roho;
1 Pierre 1.12 Ephésiens 1.3 Romains 11.33 Ephésiens 1.21 1 Corinthiens 2.7
11 kwa kadiri ya kusudi la milele alilolikusudia katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Ephésiens 1.11 2 Timothée 1.9 Romains 8.28-8.30 Esaïe 14.24-14.27 Romains 9.11
12 Katika yeye tunao ujasiri na uwezo wa kukaribia katika tumaini kwa njia ya kumwamini.
Ephésiens 2.18 Hébreux 4.14-4.16 Jean 14.6 Romains 5.2 Hébreux 10.19-10.22
13 Basi naomba msikate tamaa kwa sababu ya dhiki zangu kwa ajili yenu, zilizo utukufu kwenu.
Colossiens 1.24 Ephésiens 3.1 Esaïe 40.30-40.31 Philippiens 1.12-1.14 2 Corinthiens 1.6

Prière de Paul pour les Éphésiens

14 Kwa hiyo nampigia Baba magoti,
Ephésiens 1.16-1.19 Actes 21.5 Esaïe 45.23 Esdras 9.5 Luc 22.41
15 ambaye kwa jina lake ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa,
Ephésiens 1.21 Ephésiens 1.10 Philippiens 2.9-2.11 Actes 11.26 Apocalypse 5.8-5.14
16 awajalieni, kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake, kufanywa imara kwa nguvu, kwa kazi ya Roho wake katika utu wa ndani.
Colossiens 1.11 Philippiens 4.13 Esaïe 40.29-40.31 Zacharie 10.12 2 Timothée 4.17
17 Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani mkiwa na shina na msingi katika upendo;
Colossiens 2.7 Jean 14.23 Colossiens 1.23 Galates 2.20 1 Jean 4.16
18 ili mpate kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, na urefu, na kimo, na kina;
Psaumes 103.11-103.12 Galates 2.20 Ephésiens 1.15 Philippiens 3.8-3.10 Job 11.7-11.9
19 na kuujua upendo wake Kristo, upitao ufahamu kwa jinsi ulivyo mwingi, mpate kutimilika kwa utimilifu wote wa Mungu.
Ephésiens 1.23 Colossiens 1.10 Colossiens 2.9-2.10 Apocalypse 22.3-22.5 Galates 2.20
20 Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu;
2 Corinthiens 9.8 Romains 4.21 Jude 1.24 1 Corinthiens 2.9 Ephésiens 1.19
21 naam, atukuzwe katika Kanisa na katika Kristo Yesu hata vizazi vyote vya milele na milele. Amina.
Romains 11.36 1 Pierre 5.11 Jude 1.25 Philippiens 4.20 Romains 16.27

Cette Bible est dans le domaine public.