Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Corinthiens 9
Bible en Swahili de l’est


Fruits de la générosité

1 Kwa habari za kuwahudumia watakatifu sina haja ya kuwaandikia.
Philippiens 3.5-3.6 1 Samuel 20.23 2 Corinthiens 9.12-9.14 2 Corinthiens 8.4-8.15 Matthieu 22.31
2 Maana najua utayari wenu, ninaojisifia kwa ajili yenu kwa Wamakedonia, kwamba Akaya ilikuwa tayari tangu mwaka mzima; na bidii yenu imewatia moyo wengi wao.
2 Corinthiens 8.10 2 Corinthiens 8.8 2 Corinthiens 8.24 1 Corinthiens 16.15 Hébreux 10.24
3 Lakini naliwatuma hao ndugu, ili kujisifu kwetu kwa ajili yenu kusibatilike katika jambo hili; mpate kuwa tayari, kama nilivyosema;
2 Corinthiens 8.6 2 Corinthiens 9.4-9.5 2 Corinthiens 7.14 2 Corinthiens 8.17-8.24 Tite 3.1
4 kusudi, wakija Wamakedonia pamoja nami, na kuwakuta hamjawa tayari, tusije tukatahayarika sisi, (tusiseme ninyi), katika hali hiyo ya kutumaini.
2 Corinthiens 8.1-8.5 2 Corinthiens 9.2 2 Corinthiens 11.17 Romains 15.26 2 Corinthiens 8.24
5 Basi naliona ya kuwa ni lazima niwaonye ndugu hawa watangulie kufika kwenu, na kutengeneza mapema karama yenu mliyoahidi tangu zamani, ili iwe tayari, na hivi iwe kama kipawa, wala si kama kitu kitolewacho kwa unyimivu.
Genèse 33.11 Philippiens 4.17 1 Samuel 25.27 2 Corinthiens 12.17-12.18 1 Samuel 30.26
6 Lakini nasema neno hili, Apandaye haba atavuna haba; apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu.
Proverbes 22.9 Proverbes 11.24-11.25 Luc 6.38 Proverbes 11.18 Hébreux 6.10
7 Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.
Exode 25.2 2 Corinthiens 8.12 Romains 12.8 1 Chroniques 29.17 Actes 20.35
8 Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;
Ephésiens 3.20 Proverbes 10.22 2 Corinthiens 8.7 Malachie 3.10 Philippiens 4.18-4.19
9 kama ilivyoandikwa, Ametapanya, amewapa maskini, Haki yake yakaa milele.
Psaumes 112.9 Esaïe 51.8 1 Corinthiens 13.13 Proverbes 21.21 Galates 5.5-5.6
10 Na yeye ampaye mbegu mwenye kupanda, na mkate uwe chakula, atawapa mbegu za kupanda na kuzizidisha, naye atayaongeza mazao ya haki yenu;
Esaïe 55.10 Osée 10.12 Matthieu 6.1 1 Thessaloniciens 3.12 Genèse 47.19
11 mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu.
2 Corinthiens 1.11 1 Timothée 6.17-6.18 1 Corinthiens 1.5 2 Corinthiens 8.2-8.3 Proverbes 3.9-3.10
12 Maana utumishi wa huduma hii hauwatimizii watakatifu riziki walizopungukiwa tu, bali huzidi sana kuwa na faida kwa shukrani nyingi apewazo Mungu;
Philippiens 2.25 1 Jean 3.17 Philémon 1.4-1.7 2 Corinthiens 8.4 Philippiens 4.18-4.19
13 kwa kuwa mkijaribiwa kwa utumishi huo, wanamtukuza Mungu kwa ajili ya utii wenu katika kuikiri Injili ya Kristo, na kwa ajili ya ukarimu wenu mliowashirikisha wao na watu wote.
Matthieu 5.16 2 Corinthiens 8.4 Matthieu 9.8 1 Timothée 6.12 Jean 15.8
14 Nao wenyewe, wakiomba dua kwa ajili yenu, wawaonea shauku kwa sababu ya neema ya Mungu iliyozidi sana ndani yenu.
Esdras 6.8-6.10 1 Timothée 1.14 Philippiens 4.1 1 Corinthiens 1.4-1.5 2 Corinthiens 1.11
15 Mungu ashukuriwe kwa sababu ya kipawa chake, tusichoweza kukisifu kama ipasavyo.
2 Corinthiens 2.14 Ephésiens 5.20 Jean 3.16 1 Corinthiens 15.57 Jacques 1.17

Cette Bible est dans le domaine public.