Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Corinthiens 3.5
Bible en Swahili de l’est


Le rôle de Paul et des serviteurs de Dieu

1 Lakini, ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama na watu wenye tabia ya rohoni, bali kama na watu wenye tabia ya mwilini, kama na watoto wachanga katika Kristo.
1 Corinthiens 2.14-2.15 Romains 7.14 1 Corinthiens 2.6 1 Corinthiens 14.20 Ephésiens 4.13-4.14
2 Naliwanywesha maziwa sikuwalisha chakula; kwa kuwa mlikuwa hamjakiweza. Naam, hata sasa hamkiwezi,
Jean 16.12 1 Pierre 2.2 Hébreux 5.11-5.14
3 kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu?
1 Corinthiens 11.18 1 Corinthiens 1.11 Jacques 3.16 2 Corinthiens 12.20 Jacques 4.1-4.2
4 Maana hapo mtu mmoja asemapo, Mimi ni wa Paulo; na mwingine, Mimi ni wa Apolo, je! Ninyi si wanadamu?
1 Corinthiens 1.12 1 Corinthiens 4.6 1 Corinthiens 3.3
5 Basi Apolo ni nani? Na Paulo ni nani? Ni wahudumu ambao kwao mliamini; na kila mtu kama Bwana alivyompa.
2 Corinthiens 6.4 1 Corinthiens 3.10 2 Corinthiens 3.6 Luc 1.2 1 Corinthiens 3.7
6 Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu.
Actes 18.4-18.11 Actes 18.26-18.27 2 Corinthiens 10.14-10.15 1 Corinthiens 9.1 1 Corinthiens 3.9-3.10
7 Hivyo, apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye.
Jean 15.5 Galates 6.3 1 Corinthiens 13.2 Psaumes 115.1 2 Corinthiens 12.9
8 Basi yeye apandaye, na yeye atiaye maji ni wamoja, lakini kila mtu atapata thawabu yake mwenyewe sawasawa na taabu yake mwenyewe.
Romains 2.6 Jean 4.36-4.38 Apocalypse 22.12 Psaumes 62.12 Matthieu 16.27
9 Maana sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu.
Ephésiens 2.20-2.22 2 Corinthiens 6.1 1 Pierre 2.5 1 Corinthiens 3.16 Esaïe 61.3
10 Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake.
1 Corinthiens 3.11 Romains 15.20 Romains 12.3 1 Pierre 4.11 Luc 11.35
11 Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo.
Ephésiens 2.20 Esaïe 28.16 1 Pierre 2.6-2.8 2 Timothée 2.19 Galates 1.7-1.9
12 Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri.
1 Timothée 4.6-4.7 Actes 20.30 Apocalypse 3.18 2 Corinthiens 2.17 Esaïe 54.11-54.13
13 Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani.
1 Pierre 1.7 Apocalypse 20.12 1 Corinthiens 4.5 1 Corinthiens 3.14-3.15 2 Thessaloniciens 1.7-1.10
14 Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu.
1 Corinthiens 3.8 Matthieu 25.21-25.23 1 Corinthiens 4.5 1 Pierre 5.4 Apocalypse 2.8-2.11
15 Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto.
Jude 1.23 1 Corinthiens 3.12-3.13 2 Jean 1.8 Apocalypse 3.18 1 Pierre 4.18
16 Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
1 Corinthiens 6.19 Ezéchiel 36.27 2 Corinthiens 6.16 Romains 8.9 Romains 8.11
17 Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi.
1 Corinthiens 6.18-6.20 Ezéchiel 7.22 Sophonie 3.4 Esaïe 64.11 Ezéchiel 43.12
18 Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima.
Esaïe 5.21 Galates 6.3 1 Corinthiens 8.1-8.2 1 Corinthiens 6.9 Jacques 1.22
19 Maana hekima ya dunia hii ni upuzi mbele za Mungu. Kwa maana imeandikwa, Yeye ndiye awanasaye wenye hekima katika hila yao.
Job 5.13 Psaumes 141.10 1 Corinthiens 2.6 Romains 1.21-1.22 Esaïe 44.25
20 Na tena, Bwana anayafahamu mawazo ya wenye hekima ya kwamba ni ya ubatili.
Psaumes 94.11 Colossiens 2.8 Romains 1.21 Job 11.11-11.12 Psaumes 2.1
21 Basi, mtu ye yote na asijisifie wanadamu. Kwa maana vyote ni vyenu;
1 Corinthiens 4.6 Romains 8.32 Romains 8.28 Apocalypse 21.7 2 Corinthiens 4.15
22 kwamba ni Paulo, au Apolo, au Kefa; au dunia, au uzima, au mauti; au vile vilivyopo sasa, au vile vitakavyokuwapo; vyote ni vyenu;
2 Corinthiens 4.5 Philippiens 1.21 1 Corinthiens 9.19-9.22 1 Corinthiens 3.5-3.8 Romains 8.37-8.39
23 nanyi ni wa Kristo, na Kristo ni wa Mungu.
Galates 3.29 2 Corinthiens 10.7 1 Corinthiens 11.3 1 Corinthiens 15.23 Jean 17.9-17.10

Cette Bible est dans le domaine public.