Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Romains 4.3
Bible en Swahili de l’est


Exemples de justice par la foi dans l’Ancien Testament

1 Basi, tusemeje juu ya Ibrahimu, baba yetu kwa jinsi ya mwili?
Esaïe 51.2 Romains 4.16 Actes 13.26 Jean 8.56 2 Corinthiens 11.22
2 Kwa maana ikiwa Ibrahimu alihesabiwa haki kwa ajili ya matendo yake, analo la kujisifia; lakini si mbele za Mungu.
1 Corinthiens 1.31 1 Corinthiens 9.16 Genèse 12.12-12.13 Philippiens 3.9 Genèse 12.20
3 Maana maandiko yasemaje? Ibrahimu alimwamini Mungu, ikahesabiwa kwake kuwa haki.
Genèse 15.6 Jacques 2.23 Romains 4.9 Romains 4.5 Romains 11.2
4 Lakini kwa mtu afanyaye kazi, ujira wake hauhesabiwi kuwa ni neema, bali kuwa ni deni.
Romains 11.6 Matthieu 20.1-20.16 Romains 9.32 Romains 11.35
5 Lakini kwa mtu asiyefanya kazi, bali anamwamini yeye ambaye amhesabia haki asiyekuwa mtauwa, imani yake mtu huyo imehesabiwa kuwa haki.
Romains 3.22 Philippiens 3.9 Tite 3.3-3.7 Galates 3.8-3.14 Galates 2.16-2.17
6 Kama vile Daudi aunenavyo uheri wake mtu yule ambaye Mungu amhesabia kuwa na haki pasipo matendo,
Psaumes 146.5-146.6 Jérémie 33.16 Psaumes 112.1 Romains 4.9 Romains 3.27
7 Heri waliosamehewa makosa yao, Na waliositiriwa dhambi zao.
Psaumes 32.1-32.2 Luc 7.47-7.50 Psaumes 130.3-130.4 Esaïe 40.1-40.2 Psaumes 85.2
8 Heri mtu yule ambaye Bwana hamhesabii dhambi.
Psaumes 32.2 Esaïe 53.10-53.12 2 Corinthiens 5.19-5.20 1 Pierre 2.24 Philémon 1.18-1.19
9 Basi je! Uheri huo ni kwa hao waliotahiriwa, au kwa hao pia wasiotahiriwa? Kwa kuwa twanena ya kwamba kwake Ibrahimu imani yake ilihesabiwa kuwa ni haki.
Romains 4.3 Romains 3.29-3.30 Esaïe 49.6 Romains 15.8-15.19 Romains 10.12-10.13
10 Alihesabiwaje basi? Alipokwisha kutahiriwa, au kabla hajatahiriwa? Si baada ya kutahiriwa, bali kabla ya kutahiriwa.
Genèse 16.1-16.3 Genèse 17.23-17.27 Genèse 17.10 Genèse 15.16 1 Corinthiens 7.18-7.19
11 Naye aliipokea dalili hii ya kutahiriwa, muhuri ya ile haki ya imani aliyokuwa nayo kabla hajatahiriwa; apate kuwa baba yao wote waaminio, ijapokuwa hawakutahiriwa, ili na wao pia wahesabiwe haki;
Romains 3.22 Luc 19.9 Jean 6.35 Ezéchiel 20.12 Romains 2.28-2.29
12 tena awe baba ya kutahiriwa, kwa wale ambao si waliotahiriwa tu, bali pia wanazifuata nyayo za imani yake baba yetu Ibrahimu aliyokuwa nayo kabla hajatahiriwa.
Matthieu 3.9 Galates 4.22-4.31 2 Corinthiens 12.18 1 Pierre 2.21 Cantique 1.8
13 Kwa maana ahadi ile ya kwamba atakuwa mrithi wa ulimwengu alipewa Ibrahimu na uzao wake, si kwa sheria bali kwa haki aliyohesabiwa kwa imani.
Galates 3.29 Genèse 17.4-17.6 Galates 3.16-3.18 Genèse 28.14 Psaumes 72.11
14 Maana ikiwa wale wa sheria ndio warithi, imani imekuwa bure, na ahadi imebatilika.
Esaïe 55.11 Nombres 30.12 Hébreux 7.19 Galates 3.18-3.24 Galates 5.4
15 Kwa sababu sheria ndiyo ifanyayo hasira; maana pasipokuwapo sheria, hapana kosa.
Romains 5.13 1 Corinthiens 15.56 Galates 3.10 Romains 7.7-7.25 Romains 3.19-3.20
16 Kwa hiyo ilitoka katika imani, iwe kwa njia ya neema, ili kwamba ile ahadi iwe imara kwa wazao wote; si kwa wale wa torati tu, ila na kwa wale wa imani ya Ibrahimu; aliye baba yetu sisi sote;
Romains 9.8 Galates 3.22 Romains 3.24-3.26 Esaïe 51.2 Romains 15.8
17 (kama ilivyoandikwa, Nimekuweka kuwa baba wa mataifa mengi); mbele zake yeye aliyemwamini, yaani Mungu, mwenye kuwahuisha wafu, ayatajaye yale yasiyokuwako kana kwamba yamekuwako.
1 Corinthiens 1.28 Jean 5.21 Jean 6.63 Genèse 17.4-17.5 1 Pierre 2.10
18 Naye aliamini kwa kutarajia yasiyoweza kutarajiwa, ili apate kuwa baba wa mataifa mengi, kama ilivyonenwa, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.
Romains 5.5 Genèse 15.5-15.6 Actes 27.25 Ezéchiel 37.11 Romains 4.17
19 Yeye asiyekuwa dhaifu wa imani, alifikiri hali ya mwili wake uliokuwa umekwisha kufa, (akiwa amekwisha kupata umri wa kama miaka mia), na hali ya kufa ya tumbo lake Sara.
Genèse 17.17 Hébreux 11.11-11.19 Marc 9.23-9.24 Romains 14.21 Genèse 18.11-18.14
20 Lakini akiiona ahadi ya Mungu hakusita kwa kutokuamini, bali alitiwa nguvu kwa imani, akimtukuza Mungu;
2 Corinthiens 12.10 Jérémie 32.16-32.27 Zacharie 8.9 Nombres 11.13-11.23 Esaïe 35.4
21 huku akijua hakika ya kuwa Mungu aweza kufanya yale aliyoahidi.
Genèse 18.14 Hébreux 11.19 Psaumes 115.3 2 Timothée 1.12 Luc 1.37
22 Kwa hiyo ilihesabiwa kwake kuwa ni haki.
Romains 4.3 Romains 4.6
23 Walakini haikuandikwa kwa ajili yake tu kwamba ilihesabiwa kwake;
Romains 15.4 1 Corinthiens 10.11 2 Timothée 3.16-3.17 1 Corinthiens 10.6 1 Corinthiens 9.9-9.10
24 bali na kwa ajili yetu sisi mtakaohesabiwa vivyo hivyo, sisi tunaomwamini yeye aliyemfufua Yesu Bwana wetu katika wafu;
Actes 2.24 1 Pierre 1.21 Actes 13.30 Romains 10.9-10.10 Ephésiens 1.18-1.20
25 ambaye alitolewa kwa ajili ya makosa yetu, na kufufuliwa ili mpate kuhesabiwa haki.
Ephésiens 5.2 1 Jean 4.9-4.10 Matthieu 20.28 Esaïe 53.5-53.6 1 Corinthiens 15.17

Cette Bible est dans le domaine public.