Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 7.13
Bible en Swahili de l’est


Les relations humaines

1 Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi.
Luc 6.37 Jacques 4.11-4.12 Romains 2.1-2.2 Romains 14.10-14.13 Matthieu 7.5
2 Kwa kuwa hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayohukumiwa; na kipimo kile mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa.
Marc 4.24 Luc 6.38 Jacques 2.13 Juges 1.7 Psaumes 137.7-137.8
3 Basi, mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huiangalii?
Jean 8.7-8.9 Galates 6.1 2 Samuel 12.5-12.6 Luc 18.11 2 Chroniques 28.9-28.10
4 Au utamwambiaje nduguyo, Niache nikitoe kibanzi katika jicho lako; na kumbe! Mna boriti ndani ya jicho lako mwenyewe?
5 Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe; ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi katika jicho la ndugu yako.
Luc 13.15 Matthieu 23.13-23.28 Luc 4.23 Psaumes 51.9-51.13 Matthieu 22.18
6 Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua.
Proverbes 9.7-9.8 Proverbes 23.9 Actes 13.45-13.47 2 Timothée 4.14-4.15 Proverbes 26.11
7 Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa;
Matthieu 21.22 1 Jean 3.22 Jean 15.7 Marc 11.24 Jean 15.16
8 kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.
Luc 23.42-23.43 Actes 9.11 Psaumes 81.16 Matthieu 15.22-15.28 2 Chroniques 33.19
9 Au kuna mtu yupi kwenu, ambaye, mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe?
Luc 11.11-11.13
10 Au akiomba samaki, atampa nyoka?
11 Basi ikiwa ninyi, mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema wao wamwombao?
Luc 11.11-11.13 Romains 8.32 Psaumes 86.5 Genèse 8.21 Genèse 6.5
12 Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; maana hiyo ndiyo torati na manabii.
Romains 13.8-13.10 Luc 6.31 Galates 5.13-5.14 Lévitique 19.18 Zacharie 8.16-8.17

L’entrée dans le royaume

13 Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo.
Luc 13.24-13.25 Proverbes 16.25 Esaïe 55.7 Ezéchiel 18.27-18.32 Galates 5.24
14 Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache.
Marc 8.34 Matthieu 16.24-16.25 Romains 12.2 Esaïe 35.8 Luc 13.23-13.30
15 Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.
1 Jean 4.1 2 Pierre 2.1-2.3 Matthieu 24.11 Deutéronome 13.1-13.3 Colossiens 2.8
16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?
Luc 6.43-6.45 Jacques 3.12 Matthieu 12.33 Matthieu 7.20 2 Pierre 2.10-2.18
17 Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.
Galates 5.22-5.24 Psaumes 92.13-92.14 Ephésiens 5.9 Matthieu 12.33-12.35 Psaumes 1.3
18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.
1 Jean 3.9-3.10 Galates 5.17
19 Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.
Matthieu 3.10 Jude 1.12 Luc 3.9 Hébreux 6.8 Esaïe 5.5-5.7
20 Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.
Matthieu 7.16 Actes 5.38
21 Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
Romains 2.13 Jacques 1.22 Luc 11.28 Matthieu 25.11-25.12 Jean 6.40
22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
1 Corinthiens 13.1-13.2 Luc 13.25-13.27 Nombres 24.4 Malachie 3.17-3.18 Jean 11.51
23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.
Matthieu 25.41 Psaumes 6.8 Luc 13.27 Luc 13.25 Matthieu 25.12
24 Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;
Luc 6.47-6.49 Jean 13.17 Proverbes 10.8 Jean 14.15 Luc 11.28
25 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.
Jacques 1.12 Psaumes 125.1-125.2 1 Pierre 1.7 1 Corinthiens 3.13-3.15 1 Pierre 1.5
26 Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;
Jacques 2.20 Luc 6.49 Jérémie 8.9 Proverbes 14.1 1 Samuel 2.30
27 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.
Matthieu 13.19-13.22 Ezéchiel 13.10-13.16 1 Corinthiens 3.13 Hébreux 10.26-10.31 2 Pierre 2.20-2.22
28 Ikawa, Yesu alipoyamaliza maneno hayo, makutano walishangaa mno kwa mafundisho yake;
Luc 4.32 Marc 1.22 Marc 6.2 Jean 7.46 Jean 7.15
29 kwa maana alikuwa akiwafundisha kama mtu mwenye amri, wala si kama waandishi wao.
Hébreux 4.12-4.13 Matthieu 15.1-15.9 Matthieu 28.18 Ecclésiaste 8.4 Luc 20.46-20.47

Cette Bible est dans le domaine public.