Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 23.27
Bible en Swahili de l’est


Oracles de Balaam

1 Balaamu akamwambia Balaki, Nijengee hapa madhabahu saba, ukaniandalie hapa ng’ombe waume saba, na kondoo waume saba.
Nombres 23.29 Psaumes 50.8-50.9 1 Samuel 15.22 Ezéchiel 33.31 Jude 1.11
2 Balaki akafanya kama Balaamu alivyonena. Balaki na Balaamu wakatoa sadaka, ng’ombe mume mmoja na kondoo mume mmoja juu ya kila madhabahu.
Nombres 23.30 Nombres 23.14
3 Balaamu akamwambia Balaki, Simama karibu na sadaka yako, nami nitakwenda, labda Bwana atakuja kuonana nami; na lo lote atakalonionyesha nitakuambia. Akaenda hata mahali peupe juu ya kilima.
Nombres 23.15 Nombres 24.1 Genèse 22.2 Genèse 22.7-22.8 Exode 18.12
4 Mungu akakutana na Balaamu; naye Balaamu akamwambia, Nimetengeneza madhabahu saba, nami nimetoa sadaka ng’ombe mume mmoja na kondoo mume mmoja juu ya kila madhabahu.
Nombres 23.16 Nombres 22.20 Jean 16.2 Luc 18.12 Matthieu 20.12
5 Bwana akatia neno katika kinywa chake Balaamu, akasema, Umrudie Balaki; ukaseme maneno haya.
Deutéronome 18.18 Jérémie 1.9 Nombres 23.16 Esaïe 59.21 Esaïe 51.16
6 Akarudi kwake, na tazama, amesimama karibu na sadaka yake ya kuteketezwa, yeye na wakuu wote wa Moabu pamoja naye.
7 Akatunga mithali yake, akasema, Balaki amenileta kutoka Aramu, Mfalme wa Moabu kutoka milima ya mashariki, Njoo! Unilaanie Yakobo, Njoo! Unishutumie Israeli.
Nombres 22.5-22.6 Nombres 24.3 Nombres 23.18 Deutéronome 23.4 Job 27.1
8 Nimlaanije, yeye ambaye Mungu hakumlaani? Nimshutumuje, yeye ambaye Bwana hakumshutumu?
Nombres 22.12 Esaïe 44.25 Esaïe 47.12-47.13 Nombres 23.23 Nombres 23.20
9 Kutoka kilele cha majabali namwona; Na kutoka milimani namtazama; Angalia, ni watu wakaao peke yao, Wala hawatahesabiwa pamoja na mataifa.
Deutéronome 33.28 Deutéronome 32.8 Exode 33.16 Esdras 9.2 Esther 3.8
10 Ni nani awezaye kufanya idadi ya mavumbi ya Yakobo, Au kuhesabu robo ya Israeli? Na nife kifo chake mwenye haki, Na mwisho wangu uwe mfano wa mwisho wake.
Psaumes 37.37 Genèse 13.16 Psaumes 116.15 Apocalypse 14.13 Genèse 28.14
11 Balaki akamwambia Balaamu, Umenitendea nini? Nimekuleta ili Uwalaani adui zangu, na tazama, umewabariki kabisa kabisa.
Nombres 24.10 Nombres 22.11 Néhémie 13.2 Nombres 22.17 Psaumes 109.17-109.20
12 Naye akajibu, akasema, Je! Hainipasi kuangalia, niseme neno lile Bwana atialo kinywani mwangu?
Nombres 22.38 Tite 1.16 Proverbes 26.25 Romains 16.18 Nombres 22.20
13 Balaki akamwambia, Haya! Njoo, tafadhali, hata mahali pengine, na kutoka huko utaweza kuwaona; utaona upande wa mwisho wao tu, wala hutawaona wote, ukanilaanie hao kutoka huko.
1 Rois 20.28 Jacques 3.9-3.10 1 Rois 20.23 Michée 6.5 Nombres 22.41
14 Akamchukua mpaka shamba la Sofimu, hata kilele cha Pisga, akajenga madhabahu saba, akatoa sadaka ng’ombe mume mmoja na kondoo mume mmoja juu ya kila madhabahu.
Nombres 23.1-23.2 Nombres 21.20 Deutéronome 3.27 Deutéronome 4.49 Esaïe 1.10-1.11
15 Akamwambia Balaki, Simama hapa karibu na sadaka yako ya kuteketezwa, nami nitaonana na Bwana kule.
Nombres 23.3 Nombres 22.8
16 Bwana akaonana na Balaamu akatia neno kinywani mwake, akasema, Umrudie Balaki, ukaseme hivi.
Nombres 23.5 Nombres 24.1 Nombres 22.35
17 Akafika kwake, na tazama, amesimama karibu na sadaka yake ya kuteketezwa, na wakuu wa Moabu pamoja naye. Balaki akamwambia, Bwana amenena nini?
1 Samuel 3.17 Nombres 23.26 Jérémie 37.17
18 Naye akatunga mithali yake, akasema, Ondoka Balaki, ukasikilize; Nisikilize, Ee mwana wa Sipori;
Juges 3.20
19 Mungu si mtu, aseme uongo; Wala si mwanadamu, ajute; Iwapo amesema, hatalitenda? Iwapo amenena, hatalifikiliza?
Hébreux 6.18 Romains 11.29 1 Samuel 15.29 Malachie 3.6 Tite 1.2
20 Tazama, nimepewa amri kubariki, Yeye amebariki, nami siwezi kulitangua.
Nombres 22.12 Genèse 22.17 Genèse 12.2 Romains 8.38-8.39 Jean 10.27-10.29
21 Hakutazama uovu katika Yakobo, Wala hakuona ukaidi katika Israeli. Bwana, Mungu wake, yu pamoja naye, Na sauti kuu ya mfalme i katikati yao.
Jérémie 50.20 Exode 29.45-29.46 Romains 4.7-4.8 Romains 8.1 Esaïe 33.22
22 Mungu amewaleta kutoka Misri, Naye ana nguvu kama nguvu za nyati.
Nombres 24.8 Deutéronome 33.17 Psaumes 22.21 Job 39.9-39.11 Exode 9.16
23 Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!
Josué 13.22 Luc 10.18-10.19 Nombres 24.1 Matthieu 12.27 Michée 6.4-6.5
24 Tazama, watu hawa wanaondoka kama simba mke, Na kama simba anajiinua nafsi yake, Hatalala hata atakapokula mawindo, Na kunywa damu yao waliouawa.
Genèse 49.9 Genèse 49.27 Michée 5.8-5.9 Amos 3.8 Psaumes 17.12
25 Balaki akamwambia Balaamu, Basi usiwalaani kabisa, wala usiwabariki kabisa.
Psaumes 2.1-2.3
26 Lakini Balaamu akajibu akamwambia Balaki, Je! Sikukuambia ya kwamba, Kila neno Bwana atakalolisema sina budi kulitenda?
Nombres 22.18 1 Rois 22.14 Nombres 23.12-23.13 2 Chroniques 18.13 Actes 4.19-4.20
27 Kisha Balaki akamwambia Balaamu, Haya, njoo sasa, nikupeleke mahali pengine; labda Mungu ataridhia kwamba unilaanie watu hao huko.
Romains 11.29 Nombres 23.19-23.20 Esaïe 14.27 Job 23.13 Nombres 23.13
28 Basi Balaki akamchukua Balaamu akaenda naye mpaka kilele cha mlima Peori, mahali paelekeapo upande wa nyika iliyo chini yake.
Nombres 21.20 Psaumes 106.28
29 Balaamu akamwambia Balaki, Haya, unijengee hapa madhabahu saba, kisha uniandalie ng’ombe waume saba, na kondoo waume saba.
Nombres 23.1-23.2
30 Basi Balaki akafanya kama Balaamu alivyosema, akasongeza sadaka ng’ombe mume na kondoo mume juu ya kila madhabahu.

Cette Bible est dans le domaine public.