Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 21.32
Bible en Swahili de l’est


Les serpents brûlants

1 Na Mkanaani, mfalme wa Aradi, aliyeketi upande wa Negebu, alisikia habari ya kuwa Israeli alikuja kwa njia ya Atharimu; basi akapigana na Israeli, na watu kadha wa kadha miongoni mwao akawateka mateka.
Juges 1.16 Nombres 33.40 Josué 12.14 Josué 7.5 Nombres 13.21-13.22
2 Basi Israeli akaweka nadhiri kwa Bwana akasema, Kama wewe utawatia watu hawa mikononi mwangu kweli ndipo mimi nitaiharibu miji yao kabisa.
Genèse 28.20 Juges 11.30 1 Samuel 1.11 Josué 6.17 Josué 6.26
3 Bwana akasikiza sauti ya Israeli, akawatia Wakanaani mikononi mwao; nao wakawaharibu wao na miji yao kabisa; na jina la mahali hapo likaitwa Horma.
Nombres 14.45 Deutéronome 1.44 Psaumes 10.17 Psaumes 91.15 Psaumes 102.17
4 Wakasafiri kutoka mlima wa Hori kwa njia ya Bahari ya Shamu; ili kuizunguka nchi ya Edomu, watu wakafa moyo kwa sababu ya ile njia.
Juges 11.18 Exode 6.9 Nombres 33.41 Nombres 32.9 Nombres 20.18-20.23
5 Watu wakamnung’unikia Mungu, na Musa, Mbona mmetupandisha huku kutoka nchi ya Misri, ili tufe jangwani? Maana hapana chakula, wala hapana maji, na roho zetu zinakinai chakula hiki dhaifu.
Psaumes 78.19 Psaumes 78.24-78.25 Nombres 17.12 Exode 15.24 Exode 16.15
6 Bwana akatuma nyoka za moto kati ya watu, wakawauma, watu wengi wakafa.
1 Corinthiens 10.9 Jérémie 8.17 Deutéronome 8.15 Esaïe 14.29 Esaïe 30.6
7 Watu wakamwendea Musa, wakasema, Tumefanya dhambi kwa sababu tumemnung’unikia Mungu, na wewe; utuombee kwa Bwana, atuondolee nyoka hawa. Basi Musa akawaombea watu.
Actes 8.24 Psaumes 78.34 Nombres 11.2 Exode 8.8 1 Rois 13.6
8 Bwana akamwambia Musa, Jifanyie nyoka ya shaba, ukaiweke juu ya mti, na itakuwa kila mtu aliyeumwa, aitazamapo ataishi.
Jean 3.14 Psaumes 106.43-106.45 Psaumes 145.8
9 Musa akafanya nyoka ya shaba, akaiweka juu ya mti, hata ikiwa nyoka amemwuma mtu, alipoitazama ile nyoka ya shaba, akaishi.
2 Rois 18.4 Jean 3.14-3.15 Zacharie 12.10 Jean 6.40 1 Jean 3.8
10 Kisha wana wa Israeli wakasafiri, wakapanga marago Obothi.
Nombres 33.43-33.45
11 Wakasafiri kutoka Obothi, wakapanga Iye-abarimu, katika jangwa iliyoelekea Moabu, upande wa maawio ya jua.
12 Kutoka huko wakasafiri, wakapanga katika bonde la Zeredi.
Deutéronome 2.13-2.14
13 Kutoka huko wakasafiri, wakapanga upande wa pili wa Arnoni, ulio jangwani, utokao katika mpaka wa Waamori; maana, Arnoni ndio mpaka wa Moabu, kati ya Moabu na Waamori.
Juges 11.18 Nombres 22.36 Deutéronome 2.24 Esaïe 16.2 Jérémie 48.20
14 Kwa hiyo imesemwa katika chuo cha Vita vya Bwana, Wahebu katika Sufa, Na bonde za Arnoni,
2 Samuel 1.18 Josué 10.13
15 Na matelemko ya hizo bonde Kwenye kutelemkia maskani ya Ari, Na kutegemea mpaka wa Moabu.
Deutéronome 2.9 Nombres 21.28 Deutéronome 2.18 Deutéronome 2.29 Esaïe 15.1
16 Kutoka huko wakasafiri kwenda Beeri; ni kisima ambacho Bwana alimwambia Musa, Uwakutanishe watu, nami nitawapa maji.
Exode 17.6 Nombres 20.8 Esaïe 12.3 Juges 9.21 Jean 4.14
17 Ndipo Israeli wakaimba wimbo huu; Bubujika Ee kisima; kiimbieni;
Psaumes 105.2 Exode 15.1-15.2 Psaumes 106.12 Esaïe 12.1-12.2 Jacques 5.13
18 Kisima walichokichimba wakuu, Ambacho wakuu wa watu wakakifukua, Kwa fimbo za enzi, kwa fimbo zao.
1 Timothée 6.17-6.18 2 Chroniques 17.7-17.9 Jacques 4.12 Jean 1.17 Néhémie 3.1
19 na kutoka Matana wakaenda Nahalieli; na kutoka Nahalieli wakaenda Bamothi;
20 na kutoka Bamothi wakaenda bondeni kwenye konde la Moabu, hata kilele cha Pisga, kielekeacho chini jangwani.
Nombres 23.28 Deutéronome 3.27 Deutéronome 4.49 Deutéronome 34.1 Nombres 22.1

Victoires d’Israël

21 Kisha Israeli akatuma wajumbe kumwendea Sihoni mfalme wa Waamori, na kusema,
Deutéronome 2.26-2.28 Juges 11.19-11.21 Nombres 20.14-20.19
22 Nipe ruhusa nipite katika nchi yako; hatutageuka kando kwenda mashambani, wala kuingia katika mashamba ya mizabibu hatutakunywa maji ya visimani; tutakwenda kwa njia kuu ya mfalme, hata tutakapokuwa tumepita mpaka wako.
Nombres 20.17
23 Lakini Sihoni hakukubali kumwacha Israeli kupita katika mpaka wake; bali Sihoni akawakutanisha watu wake wote, akatoka aende kupigana na Israeli jangwani, akafika mpaka Yahasa; akapigana na Israeli.
Juges 11.20 Nombres 20.21 Esaïe 15.4 Jérémie 48.34 Deutéronome 29.7-29.8
24 Israeli wakampiga kwa makali ya upanga, na kuimiliki nchi yake, tangu mto wa Arnoni hata mto wa Yaboki, mpaka nchi ya wana wa Amoni; kwa kuwa mpaka wa wana wa Amoni ulikuwa una nguvu.
Amos 2.9 Josué 24.8 Néhémie 9.22 Psaumes 136.19 Genèse 32.22
25 Basi Israeli wakaitwaa miji hiyo yote; Israeli wakakaa katika miji yote ya Waamori, katika Heshboni, na miji yake yote.
Cantique 7.4 Esaïe 15.4 Jérémie 48.34 Nombres 21.31 Jérémie 48.2
26 Kwa kuwa Heshboni ulikuwa ni mji wa Sihoni mfalme wa Waamori, aliyekuwa akipigana na mfalme wa Moabu wa mbele, na kumpokonya nchi yake yote mkononi mwake, mpaka mto wa Arnoni.
27 Kwa hiyo, hao wanenao kwa mithali wasema, Njoni Heshboni, Mji wa Sihoni na ujengwe na kuthibitishwa;
Esaïe 14.4 Nombres 21.14 Habakuk 2.6
28 Maana, moto umetoka Heshboni, Umekuwa Ari ya Moabu, Mwali wa moto umetoka mji wa Sihoni; Wakuu wa mahali palipoinuka Arnoni
Nombres 21.15 Jérémie 48.45-48.46 Deutéronome 2.18 Juges 9.20 Esaïe 15.1-15.2
29 Ole wako Moabu! Umeangamia, enyi watu wa Kemoshi; Amewatoa wanawe kuwa wakimbizi, Na binti zake waende utumwani, Wamwendee Sihoni mfalme wa Waamori.
Juges 11.24 2 Rois 23.13 Jérémie 48.46 Jérémie 48.7 1 Rois 11.7
30 Tumewapigia mishale; Heshboni umepotea mpaka Diboni, Nasi tumeharibu mpaka Nofa, Ifikiliayo Medeba.
Esaïe 15.2 Jérémie 48.18 Jérémie 48.22 Nombres 32.3 Josué 13.17
31 Basi hivyo Israeli akaketi katika nchi ya Waamori.
Nombres 32.33-32.42 Deutéronome 3.16-3.17 Josué 12.1-12.6 Josué 13.8-13.12
32 Kisha Musa akapeleka watu ili kupeleleza Yazeri, nao wakaitwaa miji yake, wakawafukuza Waamori waliokuwamo.
Nombres 32.1 Jérémie 48.32 Nombres 32.35 Esaïe 16.8-16.9 Nombres 32.3
33 Kisha wakageuka na kukwea kwa njia ya Bashani; na Ogu mfalme wa Bashani akaondoka apigane nao huko Edrei, yeye na watu wake wote.
Josué 13.12 Deutéronome 29.7 Deutéronome 1.4 Deutéronome 3.1-3.6 Psaumes 68.15
34 Bwana akamwambia Musa, Usimche; kwa kuwa nimekwisha mtia mkononi mwako, na watu wake wote, na nchi yake; nawe utamtenda kama ulivyomtenda Sihoni mfalme wa Waamori, aliyeketi Heshboni.
Esaïe 41.13 Deutéronome 3.11 Deutéronome 3.2-3.3 Josué 10.8 Josué 8.7
35 Basi wakampiga, na wanawe, na watu wake wote, hata wasisaze kwake mtu ye yote; nao wakaimiliki nchi yake.
Josué 13.12 Romains 8.37 Deutéronome 3.3-3.17 Psaumes 135.10-135.12 Josué 12.4-12.6

Cette Bible est dans le domaine public.