Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Zacharie 6.6
Bible en Swahili de l’est


Vision de quatre chars

1 Nikainua macho yangu tena, nikaona, na tazama, yanatokea magari ya vita manne, yanatoka kati ya milima miwili, na milima hiyo ilikuwa ni milima ya shaba.
Daniel 8.22 Zacharie 6.5 Job 34.29 Daniel 2.38-2.40 Ephésiens 1.11
2 Katika gari la kwanza walikuwa farasi wekundu; na katika gari la pili walikuwa farasi weusi;
Zacharie 1.8 Apocalypse 6.2-6.6 Apocalypse 17.3 Apocalypse 12.3 Zacharie 6.6
3 na katika gari la tatu walikuwa farasi weupe; na katika gari la nne walikuwa farasi wa rangi ya kijivujivu.
Apocalypse 6.2 Apocalypse 6.8 Zacharie 1.8 Daniel 2.40-2.41 Apocalypse 20.11
4 Nikajibu, nikamwuliza yule malaika aliyesema nami, Hawa ni nini, Bwana wangu?
Zacharie 1.9 Zacharie 1.19-1.21 Zacharie 5.10 Zacharie 5.5-5.6
5 Malaika akajibu, akaniambia, Hawa ni pepo nne za mbinguni, zitokeazo baada ya kusimama mbele za Bwana wa dunia yote.
Hébreux 1.7 Hébreux 1.14 2 Chroniques 18.18-18.19 Zacharie 4.14 Zacharie 4.10
6 Gari lile lenye farasi weusi latoka kwenda hata nchi ya kaskazini; nao farasi weupe wakatoka wakafuata nyuma yao; na wale wa rangi ya kijivujivu wakatoka kwenda hata nchi ya kusini.
Jérémie 6.1 Jérémie 4.6 Jérémie 46.10 Jérémie 1.14-1.15 Ezéchiel 1.4
7 Na wale wekundu wakatoka, wakataka kwenda huko na huko katika dunia; naye akawaambia, Haya! Tokeni, mwende huko na huko katika dunia. Basi wakaenda huko na huko katika dunia.
Zacharie 1.10 Job 2.1-2.2 Genèse 13.17 2 Chroniques 16.9 Daniel 7.19
8 Ndipo akaniita, akaniambia akisema, Tazama, wale waendao mpaka nchi ya kaskazini wameituliza roho yangu katika nchi ya kaskazini.
Ezéchiel 5.13 Zacharie 1.15 Esaïe 51.22-51.23 Esaïe 48.14 Jérémie 51.48-51.49
9 Neno la Bwana likanijia, kusema,
Zacharie 8.1 Zacharie 1.1 Zacharie 7.1
10 Pokea vitu mikononi mwa baadhi ya watu waliohamishwa, yaani, Heldai, na Tobia, na Yedaya; na siku iyo hiyo enenda ukaingie katika nyumba ya Yosia, mwana wa Sefania, waliyoifikia kutoka Babeli;
Esdras 7.14-7.16 Esdras 8.26-8.30 Actes 24.17 Esaïe 66.20 Romains 15.25-15.26
11 naam, pokea fedha na dhahabu, ukafanye taji, ukamvike kichwani Yoshua, mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu;
Zacharie 3.1 Psaumes 21.3 Aggée 1.1 Cantique 3.11 Zacharie 3.5
12 ukamwambie, ukisema, Bwana wa majeshi asema hivi, ya kwamba, Tazama, mtu huyu ndiye ambaye jina lake ni Chipukizi; naye atakua katika mahali pake, naye atalijenga hekalu la Bwana.
Zacharie 3.8 Zacharie 4.6-4.9 Esaïe 4.2 Ephésiens 2.20-2.22 Matthieu 16.18
13 Naam, yeye atalijenga hekalu la Bwana; naye atauchukua huo utukufu; ataketi akimiliki katika kiti chake cha enzi; na kutakuwa na kuhani katika kiti chake cha enzi; na shauri la amani litakuwa kati ya hao wawili.
Psaumes 110.4 Hébreux 3.1 Esaïe 22.24 Esaïe 11.10 Psaumes 21.5
14 Na hizo taji zitakuwa za Heldai, na Tobia, na Yedaya; na kwa fadhili za mwana wa Sefania; ziwe ukumbusho katika hekalu la Bwana.
Matthieu 26.13 Marc 14.9 Exode 12.14 Exode 28.12 Zacharie 6.10
15 Nao walio mbali watakuja na kujenga katika hekalu la Bwana, nanyi mtajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma kwenu. Na haya yatatokea, kama mkijitahidi kuitii sauti ya Bwana, Mungu wenu.
Esaïe 60.10 Zacharie 3.7 Esaïe 57.19 Esaïe 58.10-58.14 Esaïe 56.6-56.8

Cette Bible est dans le domaine public.