Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Aggée 2.17
Bible en Swahili de l’est


La gloire future du temple

1 Katika mwezi wa saba, siku ya ishirini na moja ya mwezi, neno la Bwana lilikuja kwa kinywa cha Hagai nabii, kusema,
Aggée 1.1 Aggée 2.10 2 Pierre 1.21 Aggée 2.20 Aggée 1.15
2 Sema sasa na Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, liwali wa Yuda, na Yoshua, mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu, na hayo mabaki ya watu, ukisema,
Aggée 1.1 Néhémie 8.9 Aggée 1.14 Esdras 2.63 Esdras 1.8
3 Miongoni mwenu amebaki nani aliyeiona nyumba hii katika utukufu wake wa kwanza? Nanyi mnaionaje sasa? Je! Mbele ya macho yenu, siyo kama si kitu?
Esdras 3.12 Luc 21.5-21.6 Aggée 2.9 Zacharie 4.9-4.10 Ezéchiel 7.20
4 Lakini sasa uwe hodari, Ee Zerubabeli, asema Bwana; nawe uwe hodari, Ee Yoshua, mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu, nanyi iweni hodari, enyi watu wote wa nchi hii, asema Bwana; mkafanye kazi, kwa kuwa mimi ni pamoja nanyi, asema Bwana wa majeshi;
Zacharie 8.9 1 Chroniques 28.20 Actes 7.9 2 Samuel 5.10 Ephésiens 6.10
5 kama neno lile nililoagana nanyi mlipotoka katika nchi ya Misri; na roho yangu inakaa kati yenu; msiogope.
Néhémie 9.20 Zacharie 8.13 Exode 29.45-29.46 Esaïe 41.13 Exode 34.10
6 Kwa maana Bwana wa majeshi asema hivi, Mara moja tena, ni kitambo kidogo tu, nami nitazitikisa hizo mbingu, na hii nchi, na bahari, na nchi kavu;
Esaïe 10.25 Hébreux 12.26-12.28 Esaïe 29.17 Apocalypse 11.9 Hébreux 10.37
7 nami nitatikisa mataifa yote, na vitu vinavyotamaniwa na mataifa yote vitakuja; nami nitaijaza nyumba hii utukufu, asema Bwana wa majeshi.
1 Rois 8.11 Malachie 3.1 Daniel 2.44-2.45 Esaïe 60.7 Ezéchiel 21.27
8 Fedha ni mali yangu, na dhahabu ni mali yangu, asema Bwana wa majeshi.
Psaumes 50.10-50.12 Esaïe 60.13 Esaïe 60.17 Psaumes 24.1 1 Chroniques 29.14-29.16
9 Utukufu wa mwisho wa nyumba hii utakuwa mkuu kuliko utukufu wake wa kwanza, asema Bwana wa majeshi; na katika mahali hapa nitawapa amani, asema Bwana wa majeshi.
Esaïe 9.6-9.7 Psaumes 85.8-85.9 Colossiens 1.19-1.21 Esaïe 57.18-57.21 1 Timothée 3.16

Appel à la pureté

10 Siku ya ishirini na nne, ya mwezi wa kenda, katika mwaka wa pili wa Dario, neno la Bwana lilikuja kwa kinywa cha Hagai nabii, kusema,
Aggée 2.20 Aggée 1.1 Aggée 1.15-2.1
11 Bwana wa majeshi asema hivi, Waulizeni sasa makuhani katika habari ya sheria, mkisema,
Malachie 2.7 Lévitique 10.10-10.11 Tite 1.9 Ezéchiel 44.23-44.24 Deutéronome 33.10
12 Mtu akichukua nyama takatifu katika upindo wa nguo yake, naye akagusa kwa upindo wake mkate, au ugali, au divai, au mafuta, au chakula cho chote, je! Kitu hicho kitakuwa kitakatifu? Makuhani wakajibu, wakasema, La.
Matthieu 23.19 Lévitique 6.27 Lévitique 6.29 Lévitique 7.6 Ezéchiel 44.19
13 Ndipo Hagai akasema, Kama mtu aliyetiwa unajisi kwa kugusa maiti, akigusa kimojawapo cha vitu hivi, je! Kitakuwa najisi? Makuhani wakajibu, wakasema, Kitakuwa najisi.
Nombres 9.6-9.10 Lévitique 22.4-22.6 Nombres 5.2-5.3 Nombres 19.11-19.22
14 Ndipo Hagai akajibu, akasema, Hivyo ndivyo walivyo watu hawa, na hivyo ndivyo lilivyo taifa hili mbele zangu, asema Bwana; na hivyo ndivyo ilivyo kila kazi ya mikono yao; na kitu hicho wakitoacho sadaka huko ni najisi.
Proverbes 28.9 Proverbes 15.8 Tite 1.15 Esaïe 1.11-1.15 Esdras 3.2-3.3
15 Na sasa nawaomba, tafakarini; tangu siku hii na siku zilizopita; kabla halijatiwa bado jiwe juu ya jiwe katika nyumba ya Bwana;
Aggée 1.5 Esdras 3.10 Esdras 4.24 Aggée 2.18 Aggée 1.7
16 katika wakati huo wote, mtu alipofikia chungu ya vipimo ishirini, palikuwa na vipimo kumi tu; na mtu alipofikia shinikizo apate kuteka divai ya vyombo hamsini, palikuwa na divai ya vyombo ishirini tu.
Aggée 1.6 Malachie 2.2 Proverbes 3.9-3.10 Aggée 1.9-1.11 Zacharie 8.10-8.12
17 Naliwapiga kwa ukavu, na ukungu, na mvua ya mawe, katika kazi zote za mikono yenu; lakini hamkunielekea mimi, asema Bwana.
Deutéronome 28.22 1 Rois 8.37 Aggée 1.9 Aggée 1.11 Jérémie 5.3
18 Tafakarini, nawaomba; tangu siku hii ya leo na siku zijazo; tangu siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kenda, naam, tangu siku hiyo ulipowekwa msingi wa hekalu la Bwana tafakarini haya.
Zacharie 8.9 Aggée 2.15 Esdras 5.1-5.2 Zacharie 8.12 Deutéronome 32.29
19 Je! Mbegu ingali ghalani? Naam, huo mzabibu, wala mtini, wala mkomamanga, wala mzeituni, haikuzaa kitu; tangu siku hii ya leo nitawabariki.
Psaumes 128.1-128.5 Malachie 3.10 Matthieu 6.33 Psaumes 84.12 Psaumes 133.3

Choix de Zorobabel

20 Kisha neno la Bwana likamjia Hagai mara ya pili, siku ya ishirini na nne ya mwezi, kusema,
21 Sema na Zerubabeli, liwali wa Yuda, ukisema, Nitazitikisa mbingu na dunia;
Aggée 1.1 Esdras 5.2 Apocalypse 16.17-16.19 Zacharie 4.6-4.10 Hébreux 12.26-12.27
22 nami nitakipindua kiti cha enzi cha falme, nami nitaziharibu nguvu za falme za mataifa; nami nitayapindua magari, na hao wapandao ndani yake; farasi na hao wawapandao wataanguka chini; kila mtu kwa upanga wa ndugu yake.
Michée 5.10 Juges 7.22 Psaumes 46.9 Matthieu 24.7 Sophonie 3.8
23 Katika siku ile, asema Bwana wa majeshi, nitakutwaa wewe, Ee Zerubabeli, mtumishi wangu, mwana wa Shealtieli, asema Bwana, nami nitakufanya kuwa kama pete yenye muhuri; kwa kuwa nimekuchagua, asema Bwana wa majeshi.
Esaïe 43.10 Jérémie 22.24 Esaïe 42.1 Zacharie 4.6-4.14 Cantique 8.6

Cette Bible est dans le domaine public.