Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Habakuk 2.1
Bible en Swahili de l’est


1 Mimi nitasimama katika zamu yangu, nitajiweka juu ya mnara, nitaangalia ili nione atakaloniambia, na jinsi nitakavyojibu katika habari ya kulalamika kwangu.
Esaïe 21.8 Psaumes 85.8 Job 31.35 Esaïe 21.11-21.12 2 Rois 9.17
2 Bwana akanijibu, akasema, Iandike njozi ukaifanye iwe wazi sana katika vibao, ili aisomaye apate kuisoma kama maji.
Esaïe 30.8 Jérémie 36.2-36.4 Esaïe 8.1 Deutéronome 27.8 Deutéronome 31.22
3 Maana njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia, ingojee; kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia.
Psaumes 27.14 Daniel 10.14 Lamentations 3.25-3.26 Ezéchiel 12.25 2 Thessaloniciens 2.6-2.8
4 Tazama, roho yake hujivuna, haina unyofu ndani yake; lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake.
Romains 1.17 Hébreux 10.38 Galates 3.11-3.12 Jean 3.36 Daniel 5.20-5.23

Causes du jugement de l’oppresseur

5 Naam, pamoja na hayo, divai ni mchumi mdanganyifu, mtu wa kiburi asiyekaa nyumbani mwake; huongeza tamaa yake kama kuzimu, naye huwa kama mauti, hawezi kushibishwa; bali hujikusanyia mataifa yote; hujiwekea kabila zote chungu chungu.
Proverbes 27.20 Proverbes 20.1 2 Rois 14.10 Ecclésiaste 5.10 Proverbes 31.4-31.5
6 Je! Hawa wote hawatapiga mfano juu yake, na mithali ya kusimanga juu yake, wakisema, Ole wake yeye aongezaye kisicho mali yake! Hata lini? Na ole wake yeye ajitwikaye mzigo wa rehani!
Job 20.15-20.29 Michée 2.4 Nombres 23.7 Jérémie 50.13 Esaïe 55.2
7 Je! Hawatainuka ghafula wao watakaokuuma, hawataamka wao watakaokusumbua, nawe utakuwa mateka kwao?
Proverbes 29.1 Esaïe 47.11 Esaïe 45.1-45.3 Ecclésiaste 10.8 Esaïe 13.1-13.5
8 Kwa sababu umeteka nyara mataifa mengi, mabaki yote ya kabila watakuteka wewe; kwa sababu ya damu ya watu, na kwa sababu ya udhalimu iliotendwa nchi hii, na mji huu, na watu wote wanaokaa ndani yake.
Esaïe 33.1 Habakuk 2.17 Zacharie 2.8-2.9 Jérémie 27.7 Habakuk 2.10
9 Ole wake yeye aipatiaye nyumba yake mapato mabaya, ili apate kukiweka kioto chake juu, apate kujiepusha na mkono wa uovu!
Jérémie 49.16 1 Rois 21.19-21.24 Psaumes 52.7 Actes 1.17-1.25 Proverbes 18.11-18.12
10 Wewe umeifanyia nyumba yako kusudi la aibu, kwa kukatilia mbali watu wengi, nawe umetenda dhambi juu ya roho yako.
Nahum 1.14 2 Rois 9.26 Esaïe 33.11 Matthieu 27.25 Jérémie 22.30
11 Kwa maana jiwe litapiga kelele katika ukuta, nayo boriti katika miti italijibu.
Luc 19.40 Josué 24.27 Job 31.38-31.40 Genèse 4.10 Apocalypse 6.10
12 Ole wake yeye ajengaye mji kwa damu, awekaye imara mji mkubwa kwa uovu!
Michée 3.10 Nahum 3.1 Ezéchiel 24.9 Josué 6.26 Apocalypse 17.6
13 Angalieni; je! Jambo hili halikutoka kwa Bwana wa majeshi, kwamba watu wajishughulikie moto, na mataifa wajisumbue kwa ajili ya ubatili?
Jérémie 51.58 Esaïe 50.11 Malachie 1.4 Proverbes 21.30 Esaïe 55.2
14 Kwa maana dunia itajazwa maarifa ya utukufu wa Bwana, kama maji yaifunikavyo bahari.
Esaïe 11.9 Psaumes 22.27 Psaumes 72.19 Esaïe 6.3 Psaumes 86.9
15 Ole wake yeye ampaye jirani yake kileo, wewe utiaye sumu yako, na kumlevya pia, ili kuutazama uchi wao!
Jérémie 51.7 Genèse 9.22 2 Samuel 11.13 Exode 32.25 Genèse 19.32-19.35
16 Umejaa aibu badala ya utukufu; unywe nawe, uwe kama mtu asiyetahiriwa; kikombe cha mkono wa kuume wa Bwana kitageuzwa ukipokee, na aibu kuu itakuwa juu ya utukufu wako.
Esaïe 47.3 Lamentations 4.21 Jérémie 51.57 Osée 4.7 Nahum 3.5-3.6
17 Kwa maana udhalimu uliotendwa juu ya Lebanoni utakufunikiza, na kuangamizwa kwao wanyama kutakutia hofu; kwa sababu ya damu ya watu, na kwa sababu ya udhalimu iliotendwa nchi hii, na mji huu, na watu wote wanaokaa ndani yake.
Habakuk 2.8 Zacharie 11.1 Psaumes 55.23 Apocalypse 18.20-18.24 Jérémie 50.28
18 Sanamu ya kuchora yafaa nini, hata yeye aliyeifanya ameichora? Sanamu ya kuyeyuka, nayo ni mwalimu wa uongo, yafaa nini, hata yeye aliyeifanya aiwekee tumaini lake, na kufanya sanamu zisizoweza kusema?
Esaïe 42.17 Zacharie 10.2 Jérémie 10.8 1 Corinthiens 12.2 Esaïe 44.9-44.10
19 Ole wake yeye auambiaye mti, Amka; aliambiaye jiwe lisiloweza kusema, Ondoka! Je! Kitu hicho kitafundisha? Tazama, kimefunikwa kwa dhahabu na fedha, wala hamna pumzi ndani yake kabisa.
Psaumes 135.17 Jérémie 10.4 1 Rois 18.26-18.29 Jérémie 10.9 Esaïe 40.19
20 Lakini Bwana yumo ndani ya hekalu lake takatifu; dunia yote na inyamaze kimya mbele zake.
Zacharie 2.13 Sophonie 1.7 Psaumes 11.4 Psaumes 46.10 Jonas 2.7

Cette Bible est dans le domaine public.