Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nahum 1.1
Bible en Swahili de l’est


Description de l’Éternel

1 Ufunuo juu ya Ninawi. Kitabu cha maono aliyoyaona Nahumuu, Mwelkoshi.
Sophonie 2.13 Genèse 10.11 Zacharie 9.1 Jonas 1.2 Esaïe 13.1
2 Bwana ni Mungu mwenye wivu, naye hujilipiza kisasi; Bwana hujilipiza kisasi, naye ni mwingi wa hasira; Bwana hujilipiza kisasi juu ya adui zake, huwawekea adui zake akiba ya hasira.
Exode 20.5 Zacharie 8.2 Psaumes 94.1 Esaïe 42.13 Josué 24.19
3 Bwana si mwepesi wa hasira, ana uweza mwingi, wala hatamhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; Bwana ana njia yake katika kisulisuli na tufani, na mawingu ni mavumbi ya miguu yake.
Psaumes 104.3 Néhémie 9.17 Psaumes 147.5 Exode 34.6-34.7 Jacques 1.19
4 Yeye huikemea bahari na kuikausha, pia huikausha mito yote; Bashani hulegea, na Karmeli; hulegea nalo ua la Lebanoni.
Esaïe 33.9 Psaumes 106.9 Matthieu 8.26 Josué 3.13-3.15 Esaïe 51.10
5 Milima hutetema mbele zake, navyo vilima huyeyuka; nayo dunia huinuliwa mbele za uso wake, naam, dunia na wote wakaao ndani yake.
Michée 1.4 2 Samuel 22.8 Jérémie 4.24 Psaumes 97.4-97.5 Esaïe 64.1-64.2
6 Ni nani awezaye kusimama mbele za ghadhabu yake, naye ni nani awezaye kukaa katika ukali wa hasira yake? Hasira yake kali humwagwa kama moto, nayo majabali yapasuliwa na yeye.
Malachie 3.2 Jérémie 10.10 Nahum 1.2 Lamentations 2.4 Apocalypse 16.8
7 Bwana ni mwema, ni ngome siku ya taabu; naye huwajua hao wamkimbiliao.
Jérémie 33.11 2 Timothée 2.19 Jean 10.27 Psaumes 1.6 Jean 10.14
8 Lakini kwa gharika ifurikayo atapakomesha kabisa mahali pake, na kuwafuatia adui zake hata gizani.
Esaïe 28.17 Esaïe 8.22 Amos 8.8 Nahum 2.8 Daniel 11.40

Annonce de la destruction de Ninive

9 Mnawaza nini juu ya Bwana? Yeye atakomesha kabisa; mateso hayatainuka mara ya pili.
Psaumes 33.10 Psaumes 2.1-2.4 2 Corinthiens 10.5 Proverbes 21.30 Actes 4.25-4.28
10 Kwa maana wangawa kama miiba iliyotatana, na kunyweshwa kana kwamba ni katika kunywa kwao, wataliwa kabisa kama mabua makavu.
Michée 7.4 Malachie 4.1 Nahum 3.11 1 Samuel 25.36 1 Thessaloniciens 5.2-5.3
11 Ametoka mmoja kwako, aniaye mabaya juu ya Bwana, atoaye mashauri yasiyofaa kitu.
Nahum 1.9 2 Chroniques 32.15-32.19 2 Rois 18.30 2 Chroniques 13.7 2 Rois 18.13-18.14
12 Bwana asema hivi, Ijapokuwa wana nguvu zilizo timilifu, ijapokuwa ni wengi, hata hivyo watakatwa, naye atapita na kwenda zake. Ingawa nimekutesa, sitakutesa tena.
Esaïe 14.24-14.27 Esaïe 7.20 Esaïe 37.36 Esaïe 31.8 Esaïe 30.28-30.33
13 Na sasa nitakuvunjia nira yake, nami nitakupasulia mafungo yako.
Esaïe 9.4 Esaïe 10.27 Psaumes 107.14 Jérémie 5.5 Jérémie 2.20
14 Tena Bwana ametoa amri katika habari zako, ya kwamba asipandwe tena mtu awaye yote mwenye jina lako; toka nyumba ya miungu yako nitakatilia mbali sanamu ya kuchora, na sanamu ya kuyeyusha; nitakufanyia kaburi lako; kwa maana u mbovu.
Psaumes 109.13 Esaïe 46.1-46.2 2 Rois 19.37 Ezéchiel 32.22-32.23 Proverbes 10.7
15 Tazama, juu ya milima iko miguu yake aletaye habari njema, atangazaye amani. Zishike sikukuu zako, Ee Yuda, uziondoe nadhiri zako; kwa maana yule asiyefaa kitu hatapita kati yako tena kamwe; amekwisha kukatiliwa mbali.
Romains 10.15 Esaïe 52.7 Esaïe 29.7-29.8 Esaïe 40.9-40.10 Psaumes 116.17-116.18

Cette Bible est dans le domaine public.