Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Michée 6.12
Bible en Swahili de l’est


Procès de l’Éternel avec son peuple

1 Basi sasa, sikieni asemavyo Bwana; Simama, ujitetee mbele ya milima, vilima navyo na visikie sauti yako.
Michée 1.2 Jérémie 22.29 Deutéronome 32.1 Ezéchiel 36.1 Psaumes 50.4
2 Sikieni, enyi milima, mateto ya Bwana, na ninyi, enyi misingi ya dunia iliyo imara; kwa maana Bwana ana mateto na watu wake, naye atahojiana na Israeli.
Osée 12.2 Osée 4.1 Esaïe 1.18 2 Samuel 22.16 Psaumes 104.5
3 Enyi watu wangu, nimewatenda nini? Nami nimewachosha kwa habari gani? Shuhudieni juu yangu.
Jérémie 2.5 Esaïe 43.22-43.23 Psaumes 81.13 Psaumes 50.7 Jérémie 2.31
4 Kwa maana nalikupandisha kutoka nchi ya Misri, na kukukomboa utoke katika nyumba ya utumwa, nami naliwapeleka Musa, na Haruni, na Miriamu, watangulie mbele yako.
Exode 12.51 Deutéronome 7.8 Amos 2.10 2 Samuel 7.23 Nombres 12.1
5 Enyi watu wangu, kumbukeni sasa alivyouliza Balaki, mfalme wa Moabu, na alivyojibu Balaamu, mwana wa Beori; kumbukeni toka Shitimu hata Gilgali, mpate kuyajua matendo ya haki ya Bwana.
Nombres 25.1 Josué 5.9-5.10 Juges 5.11 Josué 4.19 Josué 24.9-24.10
6 Nimkaribie Bwana na kitu gani, na kuinama mbele za Mungu aliye juu? Je! Nimkaribie na sadaka za kuteketezwa, na ndama za umri wa mwaka mmoja?
Romains 10.2-10.3 Matthieu 19.16 Exode 12.5 Nombres 23.14-23.15 Nombres 23.29-23.30
7 Je! Bwana atapendezwa na elfu za kondoo waume, au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je! Nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa kosa langu, mzao wa mwili wangu kwa dhambi ya roho yangu?
2 Rois 16.3 Psaumes 50.9 Esaïe 40.16 1 Samuel 15.22 2 Rois 21.6
8 Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na Bwana anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!
Deutéronome 10.12-10.13 1 Samuel 15.22 Jérémie 22.3 Esaïe 66.2 Colossiens 3.12
9 Sauti ya Bwana inaulilia mji, na mtu mwenye akili ataliona jina lako; isikieni hiyo fimbo na yeye aliyeiagiza.
Sophonie 3.2 Esaïe 10.5-10.6 Esaïe 30.27 Amos 2.5 Jonas 3.4-3.10
10 Je! Hata sasa hazina za uovu zingalimo nyumbani mwa wabaya, na kipimo kilichopunguka, ambacho ni chukizo?
Amos 8.5-8.6 Amos 3.10 Jérémie 5.26-5.27 Jacques 5.1-5.4 Deutéronome 25.13-25.16
11 Je! Naweza kuwa safi nami nina mizani ya udhalimu, na mfuko wa mawe ya kupimia ya udanganyifu?
Osée 12.7 Lévitique 19.36 Proverbes 16.11
12 Kwa maana matajiri wake wamejaa jeuri, na wenyeji wake wamesema uongo, na ulimi wao una udanganyifu kichwani mwao.
Esaïe 1.23 Osée 7.13 Jérémie 9.8 Esaïe 5.7 Michée 2.1-2.2
13 Basi, kwa ajili ya hayo, mimi nami nimekupiga kwa pigo liumizalo sana; nimekufanya kuwa ukiwa, kwa sababu ya dhambi zako.
Deutéronome 28.21-28.22 Esaïe 1.5-1.7 Actes 12.23 Psaumes 107.17-107.18 Jérémie 14.18
14 Utakula, lakini hutashiba; na fedheha yako itakuwa kati yako; nawe utahama, lakini hutachukua kitu salama; na hicho utakachochukua nitakitoa kwa upanga.
Osée 4.10 Lévitique 26.26 Deutéronome 32.22-32.25 Amos 9.1-9.4 Ezéchiel 5.12
15 Utapanda, lakini hutavuna; utazikanyaga zeituni, lakini hutajipaka mafuta; na hizo zabibu, lakini hutakunywa divai.
Sophonie 1.13 Amos 5.11 Jérémie 12.13 Aggée 1.6 Lévitique 26.20
16 Kwa maana amri za Omri ndizo zishikwazo, na matendo yote ya nyumba ya Ahabu, nanyi mnakwenda katika mashauri yao; ili nikufanye kuwa ukiwa, na wenyeji waliomo humo kuwa zomeo; nanyi mtayachukua matukano waliyotukanwa watu wangu.
Jérémie 51.51 Jérémie 7.24 1 Rois 16.25-16.33 1 Rois 21.25-21.26 Psaumes 44.13

Cette Bible est dans le domaine public.