Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lévitique 6.30
Bible en Swahili de l’est


Instructions aux prêtres sur les sacrifices

1 Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
2 Mtu awaye yote akifanya dhambi, na kuasi juu ya Bwana, akamdanganya mwenziwe katika jambo la amana, au la mapatano, au la kunyang’anya, au kumwonea mwenziwe;
Colossiens 3.9 Exode 22.7-22.10 Proverbes 24.28 Actes 5.4 Lévitique 19.11
3 au kuzumbua kitu kilichopotea na kutenda la uongo juu yake, na kuapa kwa uongo; katika mambo hayo yote mojawapo atakalolitenda mtu, na kufanya dhambi kwalo;
Exode 23.4 Lévitique 19.12 Jérémie 5.2 Deutéronome 22.1-22.4 Exode 22.9-22.11
4 ndipo itakapokuwa, akiwa amefanya dhambi, na kupata hatia, atarudisha hicho alichokipata kwa kunyang’anya, au kitu kile alichokipata kwa kuonea, au ile amana aliyowekewa, au kitu kile kilichopotea alichokizumbua yeye,
Ezéchiel 18.18 Michée 2.2 Amos 3.10 Job 24.2 Lévitique 4.13-4.15
5 au kitu cho chote ambacho amekiapia uongo; atakirudisha hata kwa utimilifu wake, kisha ataongeza na sehemu ya tano zaidi juu yake; naye atampa huyo mwenyewe, siku hiyo ambayo atakapohukumiwa kuwa mwenye hatia.
Lévitique 5.16 Nombres 5.7-5.8 Luc 19.8 2 Samuel 12.6 Exode 22.1
6 Kisha ataleta sadaka yake ya hatia kwa Bwana, ni kondoo mume wa katika kundi lake, mkamilifu, sawasawa na hesabu utakayomwandikia, kuwa sadaka ya hatia, na kumpa kuhani;
Lévitique 5.15 Lévitique 5.18 Esaïe 53.10-53.11
7 na huyo kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana, naye atasamehewa; katika jambo lo lote alifanyalo hata akapata kuwa mwenye hatia kwalo.
Lévitique 4.26 Lévitique 5.18 Lévitique 5.15-5.16 1 Jean 2.1-2.2 Ezéchiel 33.19
8 Bwana akanena na Musa na kumwambia,
9 Haya, mwagize Haruni na wanawe, uwaambie, Amri ya sadaka ya kuteketezwa ni hii; hiyo sadaka ya kuteketezwa itakuwa pale motoni juu ya madhabahu usiku wote hata asubuhi; na huo moto wa madhabahu utawaka juu yake usizimike.
Nombres 28.3 Lévitique 6.12-6.13 Exode 29.38-29.42 Nombres 28.9 Lévitique 1.1-1.17
10 Naye kuhani atavaa nguo yake ya kitani, na suruali zake za kitani atazivaa mwilini mwake; naye atayazoa majivu ambayo huo moto umeiteketezea sadaka juu ya madhabahu, kisha atayaweka kando ya madhabahu.
Exode 28.39-28.43 Lévitique 16.4 Exode 39.27-39.29 Apocalypse 7.13 Lévitique 1.13
11 Kisha atayavua mavazi yake, na kuvaa mavazi mengine, kisha atayachukua yale majivu kwenda nayo nje ya marago hata mahali safi.
Lévitique 4.12 Ezéchiel 44.19 Hébreux 13.11-13.13 Lévitique 16.27 Lévitique 16.23-16.24
12 Na huo moto ulio madhabahuni atautunza uwake daima juu yake, usizimike; naye kuhani atateketeza kuni katika moto huo kila siku asubuhi; naye ataipanga sadaka ya kuteketezwa juu yake, naye atayateketeza mafuta ya sadaka za amani juu yake.
Lévitique 9.24 Hébreux 10.27 Marc 9.48-9.49 Néhémie 13.31 Lévitique 3.14-3.16
13 Moto utatunzwa uwake juu ya madhabahu daima; usizimike.
14 Na amri ya hiyo sadaka ya unga ni hii; wana wa Haruni wataisongeza mbele za Bwana, mbele ya madhabahu.
Nombres 15.4 Jean 6.32 Nombres 15.9 Nombres 15.6 Lévitique 2.1-2.2
15 Naye atatwaa konzi yake katika huo unga, katika huo unga mwembamba wa sadaka ya unga, na katika mafuta yake, na ubani wote ulio juu ya sadaka ya unga, kisha atauteketeza juu ya madhabahu kuwa harufu ya kupendeza, kuwa ukumbusho wake kwa Bwana.
Lévitique 2.2 Lévitique 2.9
16 Na unga uliosalia Haruni na wanawe wataula; utaliwa pasipo kutiwa chachu, katika mahali patakatifu; katika ua wa hema ya kukutania ndipo watakapoula.
Ezéchiel 44.29 Lévitique 2.3 Lévitique 10.12-10.13 Lévitique 6.26 Exode 12.8
17 Hautaokwa na chachu. Nimewapa kuwa sehemu yao katika matoleo yangu yasongezwayo kwa njia ya moto; ni kitu kitakatifu sana, kama hiyo sadaka ya dhambi, na kama hiyo sadaka ya hatia.
Lévitique 6.25 Lévitique 2.11 Lévitique 6.29 Lévitique 7.1 Lévitique 2.3
18 Kila mwana mume miongoni mwa wana wa Haruni atakula katika huo, kuwa ni haki yao milele katika vizazi vyenu, katika matoleo ya Bwana yasongezwayo kwa njia ya moto; mtu awaye yote atakayevigusa atakuwa ni mtakatifu
Nombres 18.10 Lévitique 6.29 1 Pierre 1.16 Aggée 2.12-2.14 Zacharie 14.20-14.21
19 Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
20 Matoleo ya Haruni na wanawe watakayomtolea Bwana, katika siku atakayotiwa mafuta, ni haya; sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba kuwa sadaka ya unga daima, nusu yake asubuhi, na nusu yake jioni.
Exode 29.2 Exode 16.36 Lévitique 5.11 Nombres 28.3 Hébreux 7.27
21 Utaandaliwa kaangoni pamoja na mafuta; ukisha kulowama utauleta ndani; utasongeza hiyo sadaka ya unga vipande vilivyookwa, iwe harufu ya kupendeza kwa Bwana.
Lévitique 2.5 Lévitique 7.9 1 Chroniques 9.31
22 Na huyo kuhani aliyetiwa mafuta badala yake katika hao wanawe ataisongeza; itateketezwa kabisa kwa Bwana kwa amri ya milele.
Hébreux 7.23 Lévitique 4.3 Lévitique 8.21 Exode 29.22-29.25 Esaïe 53.10
23 Tena kila sadaka ya unga ya kuhani itateketezwa kabisa; isiliwe.
Lévitique 6.16-6.17 Lévitique 2.10
24 Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
25 Nena na Haruni na wanawe, uwaambie, Amri ya hiyo sadaka ya dhambi ni hii; mahali hapo pachinjwapo sadaka ya kuteketezwa ndipo itakapochinjwa sadaka ya dhambi, mbele za Bwana; ni takatifu sana.
Lévitique 4.24 Lévitique 1.11 Lévitique 4.29 Lévitique 1.5 Lévitique 1.3
26 Huyo kuhani atakayeisongeza kwa ajili ya dhambi ndiye atakayeila; italiwa katika mahali patakatifu, katika ua wa hema ya kukutania.
Lévitique 10.17-10.18 Ezéchiel 42.13 Osée 4.8 Ezéchiel 44.28-44.29 Ezéchiel 46.20
27 Kila kitu kitakachoigusa nyama ya sadaka hiyo kitakuwa kitakatifu; tena itakapomwagika damu yake yo yote katika nguo yo yote, utaifua nguo hiyo iliyomwagiwa, katika mahali patakatifu.
Exode 29.37 2 Corinthiens 7.1 Exode 30.29 Matthieu 14.36 Lévitique 6.18
28 Lakini hicho chombo cha udongo ambacho hiyo nyama ilipikwa ndani yake kitavunjwa; na kama ikipikwa katika chombo cha shaba, kitasuguliwa, na kuoshwa kwa maji.
Lévitique 15.12 Lévitique 11.33 Hébreux 9.9-9.10
29 Kila mwana mume miongoni mwa makuhani atakula katika hiyo; ni takatifu sana.
Lévitique 6.17-6.18 Nombres 18.10 Lévitique 6.25
30 Wala haitaliwa sadaka ya dhambi yo yote, ambayo damu yake yo yote ililetwa ndani ya hema ya kukutania, ili kufanya upatanisho katika mahali patakatifu; itachomwa moto.
Lévitique 4.3-4.21 Hébreux 13.11 Lévitique 10.18 Lévitique 16.27-16.28 Hébreux 9.11-9.12

Cette Bible est dans le domaine public.