Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lévitique 24
Bible en Swahili de l’est


L’huile et les pains consacrés

1 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
2 Waagize wana wa Israeli kwamba wakuletee mafuta ya zeituni safi ya kupondwa kwa ajili ya ile nuru, ili hiyo taa iwake daima.
Exode 27.20-27.21 Psaumes 119.105 Matthieu 25.1-25.8 2 Chroniques 13.11 Ephésiens 5.8-5.14
3 Hapo nje ya pazia la ushahidi, ndani ya hema ya kukutania, Haruni ataitengeza tangu jioni hata asubuhi mbele za Bwana daima; ni amri ya milele katika vizazi vyenu.
4 Atazitengeza hizo taa katika kile kinara kilicho safi mbele za Bwana daima.
Exode 31.8 Exode 39.37 Apocalypse 2.5 1 Rois 7.49 Jérémie 52.19
5 Nawe utatwaa unga mwembamba, na kuoka mikate kumi na miwili ya huo unga; sehemu za kumi mbili za efa, zitakuwa katika mkate mmoja.
Exode 25.30 Exode 40.23 1 Rois 18.31 1 Samuel 21.4-21.5 Matthieu 12.4
6 Nawe iweke mistari miwili, mikate sita kwa kila mstari, juu ya hiyo meza safi, mbele za Bwana.
1 Rois 7.48 Exode 25.23-25.24 2 Chroniques 4.19 Hébreux 9.2 2 Chroniques 13.11
7 Nawe utatia ubani safi juu ya kila mstari, ili uwe ukumbusho kwa hiyo mikate, sadaka ya kusongezwa kwa Bwana kwa moto.
Lévitique 2.2 Hébreux 7.25 Genèse 9.16 Actes 10.4 Exode 12.14
8 Kila siku ya Sabato ataipanga mbele za Bwana daima; ni kwa ajili ya wana wa Israeli, agano la milele.
Nombres 4.7 2 Chroniques 2.4 1 Chroniques 9.32 1 Chroniques 23.29 Matthieu 12.3-12.5
9 Nayo itakuwa ya Haruni na wanawe; nao wataila katika mahali patakatifu; kwa sababu kwake ni takatifu sana katika sadaka zisongezwazo kwa Bwana kwa moto, kwa amri ya milele.
Lévitique 8.31 Marc 2.26 Luc 6.4 Matthieu 12.4 Lévitique 10.17

Peine sanctionnant le blasphème et la violence

10 Ikawa mwana wa mwanamke wa Kiisraeli, ambaye babaye alikuwa Mmisri, akatokea kati ya wana wa Israeli; na huyo mwana wa mwanamke wa Kiisraeli, na Mwisraeli mmoja, wakapigana pamoja ndani ya marago;
Exode 12.38 Nombres 11.4
11 kisha huyo mwana wa mwanamke wa Kiisraeli akalikufuru hilo Jina, na kuapiza; nao wakamleta kwa Musa. Na jina la mamaye alikuwa akiitwa Shelomithi, binti ya Dibri, wa kabila ya Dani.
Job 2.5 Esaïe 8.21 Exode 18.26 Exode 3.15 Exode 18.22
12 Nao wakamtia kifungoni, ili wapate kuambiwa neno litakalotoka kinywani pa Bwana.
Exode 18.15-18.16 Nombres 27.5 Nombres 15.34 Nombres 36.5-36.6 Exode 18.23
13 Na Bwana akasema na Musa, na kumwambia,
14 Mtoe huyo aliyeapiza nje ya marago; na wale wote waliomsikia na waweke mikono yao kichwani mwake, kisha mkutano wote na wamwue kwa kumpiga kwa mawe.
Deutéronome 17.7 Deutéronome 21.21 Lévitique 20.27 Lévitique 20.2 Jean 10.31-10.33
15 Nawe nena na wana wa Israeli na kuwaambia, Mtu awaye yote atakayemlaani Mungu wake atachukua dhambi yake.
Lévitique 5.1 Nombres 9.13 Exode 22.28 Lévitique 20.16-20.17
16 Na yeye atakayelikufuru jina la Bwana hakika atauawa; mkutano wote watamwua kwa kumpiga kwa mawe; kama ni mgeni, kama ni mzalia, hapo atakapolikufuru jina la Bwana atauawa.
Matthieu 12.31 Matthieu 26.66 Jean 8.58-8.59 Actes 26.11 Jacques 2.7
17 Na mtu ampigaye mtu hata akafa, lazima atauawa;
Genèse 9.5-9.6 Deutéronome 19.11-19.12 Nombres 35.30-35.31 Deutéronome 27.24 Exode 21.12-21.14
18 na atakayempiga mnyama hata akafa atalipa; uhai kwa uhai.
Lévitique 24.21 Exode 21.34-21.36
19 Na mtu akimtia mwenziwe kilema; vile vile kama alivyofanya, naye atafanyiwa vivyo;
Deutéronome 19.21 Matthieu 7.2 Matthieu 5.38
20 jeraha kwa jeraha, jicho kwa jicho, jino kwa jino; vile vile kama alivyomtia mtu kilema, naye atalipwa vivyo.
Matthieu 5.38 Deutéronome 19.21 Exode 21.23-21.25
21 Na mtu amwuaye mnyama atalipa; na yeye atakayemwua binadamu atauawa.
Lévitique 24.17-24.18 Exode 21.33
22 Mtakuwa na sheria moja tu, kwa huyo aliye mgeni, na kwa mzalia; kwa kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Exode 12.49 Nombres 9.14 Nombres 15.29 Nombres 15.15-15.16 Lévitique 19.34
23 Musa akanena na wana wa Israeli, nao wakamtoa huyo aliyeapiza nje ya marago, wakamwua kwa kumpiga kwa mawe. Wana wa Israeli wakafanya kama Bwana alivyomwagiza Musa.
Hébreux 2.2-2.3 Hébreux 10.28-10.29 Lévitique 24.14-24.16 Nombres 15.35-15.36

Cette Bible est dans le domaine public.