Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lévitique 18.15
Bible en Swahili de l’est


Les unions sexuelles interdites

1 Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
2 Nena wewe na wana wa Israeli, uwaambie, Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Exode 6.7 Lévitique 11.44 Ezéchiel 20.5 Lévitique 20.7 Lévitique 19.34
3 Nanyi msifanye matendo kama yale ya nchi ya Misri mliyokaa; wala msifanye matendo kama yale ya nchi ya Kanaani, nitakayowapeleka; wala msiende katika amri zao hao.
Exode 23.24 Ezéchiel 20.7-20.8 Lévitique 20.23 Deutéronome 12.30-12.31 Ezéchiel 23.8
4 Mtazifanya hukumu zangu, nanyi mtazishika amri zangu, ili mwenende katika hizo; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Ezéchiel 20.19 Lévitique 18.2 Deutéronome 6.1 Lévitique 20.22 Lévitique 18.26
5 Kwa ajili ya hayo mtazishika amri zangu na hukumu zangu; ambazo mtu akizitumia ataishi kwa hizo; mimi ndimi Bwana.
Galates 3.12 Ezéchiel 20.11 Romains 10.5 Ezéchiel 20.21 Luc 10.28
6 Mtu ye yote aliye wa kwenu asimkaribie mwenziwe aliye wa jamaa yake ya karibu ili kumfunua utupu; mimi ndimi Bwana.
Lévitique 18.7-18.19 Lévitique 20.11-20.12 Lévitique 20.17-20.21
7 Utupu wa baba yako, wala utupu wa mama yako, usifunue, maana ndiye mama yako; usifunue utupu wake.
Lévitique 20.11 Ezéchiel 22.10 Lévitique 20.14 Lévitique 18.8-18.16
8 Utupu wa mke wa baba yako, usifunue; maana, ni utupu wa baba yako.
1 Corinthiens 5.1 Lévitique 20.11 Deutéronome 27.20 Deutéronome 22.30 Genèse 49.4
9 Utupu wa umbu lako, binti ya baba yako, au binti ya mama yako, kwamba alizaliwa nyumbani mwenu au kwamba alizaliwa kwengine, utupu wa hao usifunue.
Lévitique 20.17 Deutéronome 27.22 Ezéchiel 22.11 2 Samuel 13.11-13.14 Lévitique 18.11
10 Utupu wa binti ya mwanao mume, au wa binti ya binti yako, utupu wao hao usifunue; kwa kuwa ndio utupu wako mwenyewe.
11 Utupu wa binti ya mkewe baba yako, aliyezaliwa na baba yako, yeye ni umbu lako, usifunue utupu wake.
12 Usifunue utupu wa umbu lake baba yako; maana, yeye ni jamaa aliye karibu.
Lévitique 20.19 Exode 6.20
13 Usifunue utupu wa umbu la mama yako; maana, yeye ni jamaa ya mama yako ya karibu.
14 Usifunue utupu wa ndugu ya baba yako, usimkaribie mkewe huyo; yeye ni shangazi lako.
Lévitique 20.20
15 Usifunue utupu wa mkweo mwanamke; yeye ni mke wa mwanao; usifunue utupu wake huyo.
Lévitique 20.12 Genèse 38.26 Ezéchiel 22.11 Genèse 38.18-38.19
16 Usifunue utupu wa mke wa nduguyo; maana, ni utupu wa nduguyo.
Lévitique 20.21 Deutéronome 25.5 Matthieu 22.24 Marc 12.19 Luc 3.19
17 Usifunue utupu wa mwanamke na binti yake; usimtwae binti ya mwanawe mume, au binti ya binti yake, ili kufunua utupu wake; hao ni jamaa ya karibu; ni uovu mkuu.
Lévitique 20.14 Deutéronome 27.23 Amos 2.7
18 Wala usitwae mwanamke pamoja na nduguye, awe mtesi wake, na kufunua utupu wake, huyo wa pili atakapokuwa yu hai.
Genèse 29.28 Malachie 2.15 1 Samuel 1.6-1.8 Exode 26.3 Genèse 30.15
19 Nawe usimkaribie mwanamke kufunua utupu wake wakati wa kutengwa kwa ajili ya unajisi wake.
Lévitique 15.24 Lévitique 20.18 Lévitique 15.19 Ezéchiel 22.10 Ezéchiel 18.6
20 Usilale na mke wa mwenzio, ukajitia unajisi naye.
Lévitique 20.10 Exode 20.14 Hébreux 13.4 1 Corinthiens 6.9 Matthieu 5.27-5.28
21 Nawe usitoe kizazi chako cho chote na kuwapisha kwa Moleki, wala usilinajisi jina la Mungu wako; mimi ndimi Bwana.
Lévitique 19.12 Lévitique 20.2-20.5 Lévitique 21.6 Deutéronome 18.10 Malachie 1.12
22 Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo.
Lévitique 20.13 Romains 1.26-1.27 1 Timothée 1.10 1 Corinthiens 6.9 Juges 19.22
23 Wala usilale na mnyama ye yote, ili kujitia unajisi kwake; wala mwanamke asisimame mbele ya mnyama ili kulala naye; ni uchafuko.
Exode 22.19 Lévitique 20.15-20.16 Lévitique 20.12 Deutéronome 27.21
24 Msijitie unajisi katika mambo hayo hata mojawapo; kwa maana hizo taifa nitakazozitoa mbele zenu zimekuwa najisi kwa mambo hayo yote;
Deutéronome 18.12 Lévitique 18.30 Deutéronome 12.31 Marc 7.10-7.23 Lévitique 20.22-20.23
25 na hiyo nchi imekuwa najisi; kwa ajili ya hayo naipatiliza uovu wake juu yake, na hiyo nchi yatapika wenyeji wake na kuwatoa.
Lévitique 18.28 Jérémie 2.7 Jérémie 9.9 Jérémie 14.10 Nombres 35.33-35.34
26 Kwa hiyo mtazishika amri zangu na hukumu zangu, wala msifanye machukizo hayo mojawapo; yeye aliye mzalia, wala mgeni aketiye kati yenu;
Lévitique 18.5 Psaumes 105.44-105.45 Lévitique 17.8 Deutéronome 4.1-4.2 Jean 15.14
27 (kwa kuwa hao watu wa nchi wameyafanya machukizo haya yote, hao waliotangulia mbele zenu, na hiyo nchi imekuwa najisi;)
Ezéchiel 22.11 Deutéronome 27.15 Deutéronome 23.18 Osée 9.10 1 Rois 14.24
28 ili kwamba hiyo nchi isiwatapike na ninyi pia, hapo mtakapoitia unajisi, kama ilivyoitapika hiyo taifa iliyotangulia mbele yenu.
Ezéchiel 36.13 Lévitique 18.25 Apocalypse 3.16 Romains 8.22 Ezéchiel 36.17
29 Kwani mtu awaye yote atakayefanya machukizo hayo mojawapo, nafsi hizo zitakazoyafanya zitakatiliwa mbali na watu wao.
Lévitique 17.10 Exode 12.15 Lévitique 20.6
30 Kwa ajili ya hayo yashikeni mausia yangu, ili kwamba msifanye kabisa desturi hizi zichukizazo mojawapo, zilizotangulia kufanywa mbele zenu, wala msijitie unajisi katika mambo hayo; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Lévitique 20.23 Lévitique 18.2-18.4 Deutéronome 11.1 Lévitique 18.26-18.27 Deutéronome 18.9-18.12

Cette Bible est dans le domaine public.