Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 13.7
Bible en Swahili de l’est


L’Éternel, seul vrai soutien d’Israël

1 Efraimu aliponena, palikuwa na tetemeko; alijitukuza katika Israeli; Lakini alipokosa katika Baali, alikufa.
Osée 11.2 Juges 8.1 Romains 5.12 Nombres 13.8 1 Rois 18.18-18.19
2 Na sasa wanazidi kufanya dhambi, nao wamejifanyizia sanamu kwa fedha yao, naam, sanamu kwa kadiri ya akili zao; zote pia ni kazi ya mafundi; nao huzitaja hivi, Wanaume watoao dhabihu na wazibusu ndama.
Esaïe 46.6 Esaïe 44.17-44.20 Osée 2.8 Jérémie 10.4 1 Rois 19.18
3 Kwa sababu hiyo watakuwa kama wingu la asubuhi, na kama umande utowekao upesi, kama makapi yaliyopeperushwa na tufani sakafuni, na kama moshi utokao katika bomba.
Osée 6.4 Psaumes 68.2 Psaumes 1.4 Esaïe 17.13 Daniel 2.35
4 Lakini mimi ni Bwana, Mungu wako tangu nchi ya Misri; wala hutamjua mungu mwingine ila mimi; wala zaidi ya mimi hakuna Mwokozi.
Osée 12.9 Esaïe 45.21-45.22 Esaïe 43.10-43.13 Esaïe 44.6-44.8 Psaumes 81.9-81.10
5 Mimi nalikujua katika jangwa, katika nchi yenye kiu nyingi.
Deutéronome 2.7 Deutéronome 8.15 Deutéronome 32.10 Psaumes 63.1 Psaumes 31.7
6 Kwa kadiri ya malisho yao, kwa kadiri iyo hiyo walishiba; walishiba na moyo wao ukatukuka; ndiyo sababu wamenisahau mimi.
Deutéronome 32.13-32.15 Esaïe 17.10 Osée 8.4 Osée 10.1 Jérémie 2.31-2.32
7 Basi nimekuwa kama simba kwao; kama chui nitavizia njiani;
Osée 5.14 Jérémie 5.6 Lamentations 3.10 Amos 3.8 Esaïe 42.13
8 nitakutana nao kama dubu aliyenyang’anywa watoto wake; nami nitararua nyama ya mioyo yao; na huko nitawala kama simba; huyo mnyama mkali atawararua.
2 Samuel 17.8 Esaïe 5.29 Jérémie 12.9 Psaumes 80.13 Psaumes 50.22
9 Haya ndiyo maangamizo yako, Ee Israeli, ya kuwa wewe u kinyume changu mimi, kinyume cha msaada wako.
Jérémie 2.17 Jérémie 2.19 Deutéronome 33.26 Jérémie 5.25 Psaumes 121.1-121.2
10 Yuko wapi sasa mfalme wako, apate kukuokoa katika miji yako yote? Na hao waamuzi wako, uliowanena hivi, Nipe mfalme na wakuu?
Osée 8.4 1 Samuel 8.5-8.6 Osée 10.3 Psaumes 47.6-47.7 Esaïe 43.15
11 Nimekupa mfalme katika hasira yangu, nikamwondoa katika ghadhabu yangu.
1 Samuel 10.19 1 Rois 12.15-12.16 1 Samuel 8.7-8.9 Osée 10.7 1 Samuel 31.1-31.7
12 Uovu wa Efraimu umefungwa kwa kukazwa; dhambi yake imewekwa akiba.
Job 14.17 Deutéronome 32.34-32.35 Romains 2.5 Job 21.19
13 Utungu wa mwanamke mwenye mimba utampata; yeye ni mwana asiye na akili; maana wakati umewadia, ambao haimpasi kukawia mahali wapenyapo watoto.
Esaïe 13.8 Michée 4.9-4.10 Esaïe 37.3 Psaumes 48.6 Proverbes 22.3
14 Nitawakomboa na nguvu za kaburi; nitawaokoa na mauti; ewe mauti, ya wapi mapigo yako? Ewe kaburi, ku wapi kuharibu kwako? Kujuta kutafichwa na macho yangu.
Esaïe 25.8 Apocalypse 21.4 Esaïe 26.19 Psaumes 49.15 Psaumes 30.3
15 Ajapokuwa yeye ni mwenye kuzaa sana kati ya ndugu zake, upepo wa mashariki utakuja, hiyo pumzi ya Bwana itokayo upande wa nyikani, na kijito chake cha maji kitakauka, na chemchemi yake itakaushwa; yeye atateka nyara hazina ya vyombo vyote vipendezavyo.
Ezéchiel 19.12 Ezéchiel 17.10 Genèse 41.52 Genèse 49.22 Jérémie 4.11
16 Samaria atachukua hatia yake; kwa maana amemwasi Mungu wake; wataanguka kwa upanga; watoto wao wachanga watavunjwa vipande vipande, na wanawake wao wenye mimba watatambuliwa.
2 Rois 15.16 2 Rois 8.12 Esaïe 13.16 Amos 1.13 Osée 10.2

Cette Bible est dans le domaine public.