Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 13
Bible en Swahili de l’est


L’Éternel, seul vrai soutien d’Israël

1 Efraimu aliponena, palikuwa na tetemeko; alijitukuza katika Israeli; Lakini alipokosa katika Baali, alikufa.
Osée 11.2 1 Rois 12.25 2 Corinthiens 5.14 2 Rois 17.16-17.18 Nombres 10.22
2 Na sasa wanazidi kufanya dhambi, nao wamejifanyizia sanamu kwa fedha yao, naam, sanamu kwa kadiri ya akili zao; zote pia ni kazi ya mafundi; nao huzitaja hivi, Wanaume watoao dhabihu na wazibusu ndama.
Esaïe 44.17-44.20 Osée 2.8 Jérémie 10.4 1 Rois 19.18 Esaïe 46.6
3 Kwa sababu hiyo watakuwa kama wingu la asubuhi, na kama umande utowekao upesi, kama makapi yaliyopeperushwa na tufani sakafuni, na kama moshi utokao katika bomba.
Osée 6.4 Psaumes 1.4 Psaumes 68.2 Esaïe 17.13 Daniel 2.35
4 Lakini mimi ni Bwana, Mungu wako tangu nchi ya Misri; wala hutamjua mungu mwingine ila mimi; wala zaidi ya mimi hakuna Mwokozi.
Osée 12.9 Esaïe 45.21-45.22 Esaïe 43.10-43.13 Psaumes 81.9-81.10 Exode 20.2-20.3
5 Mimi nalikujua katika jangwa, katika nchi yenye kiu nyingi.
Deutéronome 2.7 Deutéronome 8.15 Deutéronome 32.10 Psaumes 1.6 Jérémie 2.6
6 Kwa kadiri ya malisho yao, kwa kadiri iyo hiyo walishiba; walishiba na moyo wao ukatukuka; ndiyo sababu wamenisahau mimi.
Deutéronome 32.13-32.15 Osée 10.1 Jérémie 2.31-2.32 Psaumes 10.4 Deutéronome 8.12-8.14
7 Basi nimekuwa kama simba kwao; kama chui nitavizia njiani;
Osée 5.14 Jérémie 5.6 Lamentations 3.10 Esaïe 42.13 Amos 1.2
8 nitakutana nao kama dubu aliyenyang’anywa watoto wake; nami nitararua nyama ya mioyo yao; na huko nitawala kama simba; huyo mnyama mkali atawararua.
2 Samuel 17.8 Jérémie 12.9 Psaumes 80.13 Psaumes 50.22 Proverbes 17.12
9 Haya ndiyo maangamizo yako, Ee Israeli, ya kuwa wewe u kinyume changu mimi, kinyume cha msaada wako.
Jérémie 2.17 Jérémie 2.19 Deutéronome 33.26 Tite 3.3-3.7 Esaïe 3.9
10 Yuko wapi sasa mfalme wako, apate kukuokoa katika miji yako yote? Na hao waamuzi wako, uliowanena hivi, Nipe mfalme na wakuu?
Osée 8.4 1 Samuel 8.5-8.6 Osée 10.3 Jérémie 8.19 Psaumes 74.12
11 Nimekupa mfalme katika hasira yangu, nikamwondoa katika ghadhabu yangu.
1 Samuel 10.19 1 Samuel 31.1-31.7 Proverbes 28.2 2 Rois 17.1-17.4 1 Samuel 16.1
12 Uovu wa Efraimu umefungwa kwa kukazwa; dhambi yake imewekwa akiba.
Deutéronome 32.34-32.35 Job 14.17 Romains 2.5 Job 21.19
13 Utungu wa mwanamke mwenye mimba utampata; yeye ni mwana asiye na akili; maana wakati umewadia, ambao haimpasi kukawia mahali wapenyapo watoto.
Esaïe 13.8 Esaïe 37.3 Michée 4.9-4.10 Esaïe 26.17 2 Rois 19.3
14 Nitawakomboa na nguvu za kaburi; nitawaokoa na mauti; ewe mauti, ya wapi mapigo yako? Ewe kaburi, ku wapi kuharibu kwako? Kujuta kutafichwa na macho yangu.
Esaïe 25.8 Apocalypse 21.4 Psaumes 49.15 Esaïe 26.19 Psaumes 16.10
15 Ajapokuwa yeye ni mwenye kuzaa sana kati ya ndugu zake, upepo wa mashariki utakuja, hiyo pumzi ya Bwana itokayo upande wa nyikani, na kijito chake cha maji kitakauka, na chemchemi yake itakaushwa; yeye atateka nyara hazina ya vyombo vyote vipendezavyo.
Ezéchiel 19.12 Ezéchiel 17.10 Jérémie 4.11 Genèse 41.52 Genèse 49.22
16 Samaria atachukua hatia yake; kwa maana amemwasi Mungu wake; wataanguka kwa upanga; watoto wao wachanga watavunjwa vipande vipande, na wanawake wao wenye mimba watatambuliwa.
2 Rois 15.16 2 Rois 8.12 Esaïe 13.16 Amos 1.13 Michée 6.16

Cette Bible est dans le domaine public.