Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 4.17
Bible en Swahili de l’est


Siège de Jérusalem

1 Wewe nawe, mwanadamu, jipatie tofali uliweke mbele yako, kisha, chora juu yake mfano wa mji, yaani, Yerusalemu;
Jérémie 25.15-25.38 Osée 12.10 Jérémie 18.2-18.12 Jérémie 19.1-19.15 Ezéchiel 12.3-12.16
2 ukauhusuru, ukajenge ngome juu yake, na kufanya boma juu yake; ukaweke makambi juu yake, na kuweka magogo ya kuubomoa yauzunguke pande zote.
Ezéchiel 21.22 Luc 19.42-19.44 Jérémie 6.6 Jérémie 39.1-39.2 Jérémie 52.4
3 Kisha ukajipatie bamba la chuma, ukalisimamishe liwe ukuta wa chuma kati ya wewe na mji huo; ukaelekeze uso wako juu yake, nao utahusuriwa, nawe utauhusuru. Hili litakuwa ishara kwa nyumba ya Israeli.
Ezéchiel 12.6 Esaïe 8.18 Esaïe 20.3 Ezéchiel 12.11 Ezéchiel 24.24-24.27
4 Tena lala chini kwa ubavu wako wa kushoto, ukaweke huo uovu wa nyumba ya Israeli juu yake; kwa kadiri ya hesabu ya siku utakazolala juu yake, kwa kadiri hiyo utauchukua uovu wao.
Lévitique 16.22 Lévitique 10.17 Nombres 18.1 Esaïe 53.11-53.12 Ezéchiel 4.8
5 Maana nimekuagizia miaka ya uovu wao iwe kwako hesabu ya siku, yaani, siku mia tatu na tisini; ndivyo utakavyouchukua uovu wa nyumba ya Israeli.
Esaïe 53.6 Nombres 14.34
6 Tena utakapozitimiza hizo, utalala kwa ubavu wako wa kuume, nawe utauchukua uovu wa nyumba ya Yuda; siku arobaini, siku moja kwa mwaka mmoja, nimekuagizia.
Nombres 14.34 Daniel 12.11-12.12 Daniel 9.24-9.26 Apocalypse 11.2-11.3 Apocalypse 12.14
7 Nawe utauelekeza uso wako, uelekee mazingiwa ya Yerusalemu, na mkono wako utakuwa haukuvikwa nguo, nawe utatoa unabii juu yake.
Esaïe 52.10 Ezéchiel 4.3 Ezéchiel 6.2 Ezéchiel 21.2
8 Na tazama, nitakutia pingu, wala hutageuka toka upande mmoja hata upande wa pili, hata utakapozitimiza siku za mazingiwa yako.
Ezéchiel 3.25
9 Pia ujipatie ngano, na shayiri, na kunde, na dengu, na mtama, na kusemethi, ukavitie vyote katika chombo kimoja, ukajifanyie mkate kwa vitu hivyo; kwa kadiri ya hesabu ya siku utakazolala ubavuni mwako; yaani, siku mia tatu na tisini utaula.
Esaïe 28.25 Ezéchiel 4.13 Ezéchiel 4.16
10 Na chakula chako utakachokula kitapimwa, shekeli ishirini kwa siku moja; utakila kwa wakati wake.
Esaïe 3.1 Deutéronome 28.51-28.68 Lévitique 26.26 Ezéchiel 4.16 Ezéchiel 14.13
11 Nawe utakunywa maji kwa kuyapima, sehemu ya sita ya hini; utayanywa kwa wakati wake.
Ezéchiel 4.16 Jean 3.34 Esaïe 5.13
12 Nawe utakila kama mkate wa shayiri, nawe utakioka mbele ya macho yao juu ya mashonde yatokayo katika mwanadamu.
Esaïe 36.12 Genèse 18.6
13 Bwana akasema, Hivyo ndivyo wana wa Israeli watakavyokula chakula chao, hali kimetiwa unajisi, kati ya mataifa nitakakowafukuza.
Daniel 1.8 Osée 9.3-9.4
14 Ndipo nikasema, Ee Bwana MUNGU, tazama, roho yangu haikutiwa unajisi; maana tangu ujana wangu hata sasa sijala nyamafu, wala iliyoraruliwa na hayawani; wala nyama ichukizayo haikuingia kinywani mwangu.
Ezéchiel 9.8 Actes 10.14 Ezéchiel 20.49 Jérémie 1.6 Esaïe 65.4
15 Ndipo akaniambia, Tazama, nimekupa mashonde ya ng’ombe badala ya mashonde ya mwanadamu, nawe utakipika chakula chako juu ya hayo.
16 Tena akaniambia, Mwanadamu, tazama, nitalivunja tegemeo la chakula katika Yerusalemu; nao watakula mkate kwa kuupima, na kwa kuutunza sana; nao watakunywa maji kwa kuyapima, na kwa kushangaa;
Lévitique 26.26 Ezéchiel 5.16 Ezéchiel 14.13 Esaïe 3.1 Ezéchiel 4.10-4.11
17 wapate kupungukiwa na mkate na maji, na kustaajabiana, na kukonda kwa sababu ya uovu wao.
Ezéchiel 24.23 Lévitique 26.39 Ezéchiel 33.10

Cette Bible est dans le domaine public.