Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lamentations 4.2
Bible en Swahili de l’est


Horreur du siège de Jérusalem

1 Jinsi dhahabu ilivyoacha kung’aa, Na dhahabu iliyo safi ilivyobadilika! Mawe ya patakatifu yametupwa Mwanzo wa kila njia.
Ezéchiel 7.19-7.22 Esaïe 1.21 Lamentations 2.19 Luc 21.5-21.6 Jérémie 52.13
2 Wana wa Sayuni wenye thamani, Walinganao na dhahabu safi, Jinsi wanavyodhaniwa kuwa vyombo vya udongo, Kazi ya mikono ya mfinyanzi!
Jérémie 19.11 Esaïe 30.14 Lamentations 2.21 2 Corinthiens 4.7 Jérémie 22.28
3 Hata mbwa-mwitu hutoa matiti, Huwanyonyesha watoto wao; Binti ya watu wangu amekuwa mkali, Mfano wa mbuni jangwani.
Esaïe 49.15 Ezéchiel 5.10 Deutéronome 28.52-28.57 Romains 1.31 Jérémie 19.9
4 Ulimi wa mtoto anyonyaye Wagandamana na kaakaa lake kwa kiu; Watoto wachanga waomba chakula, Wala hakuna hata mmoja awamegeaye.
Psaumes 22.15 Lamentations 2.11-2.12 Deutéronome 32.24 Lamentations 1.11 Matthieu 7.9-7.11
5 Wale waliokula vitu vya anasa Wameachwa peke yao njiani; Wale waliokuzwa kuvaa nguo nyekundu Wakumbatia jaa.
Amos 6.3-6.7 Luc 15.16 Luc 16.19 1 Timothée 5.6 Luc 7.25
6 Maana uovu wa binti ya watu wangu ni mkubwa Kuliko dhambi ya Sodoma, Uliopinduliwa kama katika dakika moja, Wala mikono haikuwekwa juu yake.
Genèse 19.25 Luc 10.12 Ezéchiel 16.48-16.50 Esaïe 1.9-1.10 Luc 12.47
7 Wakuu wake walikuwa safi kuliko theluji, Walikuwa weupe kuliko maziwa; Miili yao, walikuwa wekundu kuliko marijani, Na umbo lao kama yakuti samawi.
Psaumes 51.7 Cantique 5.10 Juges 13.7 Nombres 6.2-6.21 1 Samuel 16.12
8 Nyuso zao ni nyeusi kuliko makaa; Hawajulikani katika njia kuu; Ngozi yao yagandamana na mifupa yao Imekauka, imekuwa kama mti.
Psaumes 102.3-102.5 Job 30.30 Lamentations 5.10 Job 19.20 Psaumes 119.83
9 Heri wale waliouawa kwa upanga Kuliko wao waliouawa kwa njaa; Maana hao husinyaa, wakichomwa Kwa kukosa matunda ya mashamba.
Ezéchiel 24.23 Lévitique 26.39 Jérémie 16.4 Ezéchiel 33.10
10 Mikono ya wanawake wenye huruma Imewatokosa watoto wao wenyewe; Walikuwa ndio chakula chao Katika uharibifu wa binti ya watu wangu.
Lamentations 2.20 Esaïe 49.15 Jérémie 19.9 2 Rois 6.26-6.29 Lamentations 3.48
11 Bwana ameitimiza kani yake, Ameimimina hasira yake kali; Naye amewasha moto katika Sayuni Ulioiteketeza misingi yake.
Ezéchiel 22.31 Jérémie 7.20 Jérémie 17.27 Lamentations 2.17 Deutéronome 32.21-32.25
12 Wafalme wa dunia hawakusadiki, Wala wote wakaao duniani, Ya kwamba mtesi na adui wangeingia Katika malango ya Yerusalemu.
1 Rois 9.8-9.9 Psaumes 48.4-48.6 Jérémie 21.13 Deutéronome 29.24-29.28
13 Ni kwa sababu ya dhambi za manabii wake Na maovu ya makuhani wake, Walioimwaga damu ya wenye haki Katikati yake.
Jérémie 5.31 Jérémie 6.13 Matthieu 23.31 Jérémie 26.8-26.9 Lamentations 2.14
14 Hutanga-tanga njiani kama vipofu, Wametiwa unajisi kwa damu; Hata ikawa watu wasiweze Kuyagusa mavazi yao.
Jérémie 2.34 Esaïe 56.10 Esaïe 1.15 Nombres 19.16 Deutéronome 28.28-28.29
15 Watu waliwapigia kelele, Ondokeni, Uchafu, Ondokeni, ondokeni, msiguse; Walipokimbia na kutanga-tanga, watu walisema kati ya mataifa, Hawatakaa hapa tena.
Lévitique 13.45-13.46
16 Hasira ya Bwana imewatenga, Yeye hatawaangalia tena; Hawakujali nafsi za wale makuhani, Hawakuwaheshimu wazee wao.
Esaïe 9.14-9.16 Lamentations 5.12 2 Rois 25.18-25.21 Lévitique 26.33-26.39 Genèse 49.7
17 Macho yetu yamechoka Kwa kuutazamia bure msaada wetu; Katika kungoja kwetu tumengojea taifa Lisiloweza kutuokoa.
Ezéchiel 29.16 Ezéchiel 29.6-29.7 Esaïe 20.5 2 Rois 24.7 Jérémie 37.7-37.10
18 Wanatuvizia hatua zetu, Hata hatuwezi kwenda katika njia zetu; Mwisho wetu umekaribia, siku zetu zimetimia; Maana mwisho wetu umefika.
Amos 8.2 Ezéchiel 7.2-7.12 Lamentations 3.52 Jérémie 16.16 Jérémie 52.7-52.9
19 Waliotufuatia ni wepesi Kuliko tai za mbinguni; Hao walitufuatia milimani, Nao walituotea jangwani.
Esaïe 5.26-5.28 Habakuk 1.8 Jérémie 4.13 Deutéronome 28.49 Esaïe 30.16-30.17
20 Pumzi ya mianzi ya pua zetu, masihi wa BWANA, Alikamatwa katika marima yao;Ambaye kwa habari zake tulisema,Chini ya kivuli chake tukakaa kati ya mataifa.
Genèse 2.7 Ezéchiel 12.13 2 Samuel 19.21 Jérémie 39.5 Lamentations 2.9
21 Furahi, ushangilie, Ee binti Edomu, Ukaaye katika nchi ya Usi; Hata kwako kikombe kitapita, Utalewa, na kujifanya uchi.
Psaumes 137.7 Job 1.1 Amos 1.11 Jérémie 25.15-25.29 Esaïe 34.1-34.17
22 Uovu wako umetimia, Ee binti Sayuni; Hatakuhamisha tena; Atapatiliza uovu wako, Ee binti Edomu; Atazivumbua dhambi zako.
Esaïe 40.2 Psaumes 137.7 Jérémie 33.8 Malachie 1.4 Lamentations 4.21

Cette Bible est dans le domaine public.