Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lamentations 4.14
Bible en Swahili de l’est


Horreur du siège de Jérusalem

1 Jinsi dhahabu ilivyoacha kung’aa, Na dhahabu iliyo safi ilivyobadilika! Mawe ya patakatifu yametupwa Mwanzo wa kila njia.
Ezéchiel 7.19-7.22 Esaïe 1.21 Lamentations 2.19 2 Rois 25.9-25.10 Esaïe 14.12
2 Wana wa Sayuni wenye thamani, Walinganao na dhahabu safi, Jinsi wanavyodhaniwa kuwa vyombo vya udongo, Kazi ya mikono ya mfinyanzi!
Jérémie 19.11 Esaïe 30.14 Zacharie 9.13 Lamentations 5.12 Romains 9.21-9.23
3 Hata mbwa-mwitu hutoa matiti, Huwanyonyesha watoto wao; Binti ya watu wangu amekuwa mkali, Mfano wa mbuni jangwani.
Ezéchiel 5.10 Esaïe 49.15 Lamentations 4.10 Luc 23.28-23.29 Lévitique 26.29
4 Ulimi wa mtoto anyonyaye Wagandamana na kaakaa lake kwa kiu; Watoto wachanga waomba chakula, Wala hakuna hata mmoja awamegeaye.
Psaumes 22.15 Lamentations 2.11-2.12 Psaumes 137.6 Deutéronome 32.24 Lamentations 1.11
5 Wale waliokula vitu vya anasa Wameachwa peke yao njiani; Wale waliokuzwa kuvaa nguo nyekundu Wakumbatia jaa.
Amos 6.3-6.7 Luc 7.25 2 Samuel 1.24 Luc 15.16 Luc 16.19
6 Maana uovu wa binti ya watu wangu ni mkubwa Kuliko dhambi ya Sodoma, Uliopinduliwa kama katika dakika moja, Wala mikono haikuwekwa juu yake.
Genèse 19.25 Luc 10.12 Lamentations 4.9 Matthieu 11.23-11.24 Daniel 9.12
7 Wakuu wake walikuwa safi kuliko theluji, Walikuwa weupe kuliko maziwa; Miili yao, walikuwa wekundu kuliko marijani, Na umbo lao kama yakuti samawi.
Psaumes 51.7 Cantique 5.10 Juges 16.17 Amos 2.11-2.12 Juges 13.5
8 Nyuso zao ni nyeusi kuliko makaa; Hawajulikani katika njia kuu; Ngozi yao yagandamana na mifupa yao Imekauka, imekuwa kama mti.
Lamentations 5.10 Psaumes 102.3-102.5 Job 30.30 Job 19.20 Psaumes 119.83
9 Heri wale waliouawa kwa upanga Kuliko wao waliouawa kwa njaa; Maana hao husinyaa, wakichomwa Kwa kukosa matunda ya mashamba.
Lévitique 26.39 Ezéchiel 24.23 Jérémie 16.4 Ezéchiel 33.10
10 Mikono ya wanawake wenye huruma Imewatokosa watoto wao wenyewe; Walikuwa ndio chakula chao Katika uharibifu wa binti ya watu wangu.
Lamentations 2.20 Esaïe 49.15 Jérémie 19.9 Ezéchiel 5.10 Lamentations 4.3
11 Bwana ameitimiza kani yake, Ameimimina hasira yake kali; Naye amewasha moto katika Sayuni Ulioiteketeza misingi yake.
Jérémie 7.20 Ezéchiel 22.31 Lamentations 2.17 Jérémie 17.27 Jérémie 9.9-9.11
12 Wafalme wa dunia hawakusadiki, Wala wote wakaao duniani, Ya kwamba mtesi na adui wangeingia Katika malango ya Yerusalemu.
Deutéronome 29.24-29.28 1 Rois 9.8-9.9 Psaumes 48.4-48.6 Jérémie 21.13
13 Ni kwa sababu ya dhambi za manabii wake Na maovu ya makuhani wake, Walioimwaga damu ya wenye haki Katikati yake.
Jérémie 5.31 Jérémie 6.13 Jérémie 26.8-26.9 Lamentations 2.14 Ezéchiel 22.26-22.28
14 Hutanga-tanga njiani kama vipofu, Wametiwa unajisi kwa damu; Hata ikawa watu wasiweze Kuyagusa mavazi yao.
Jérémie 2.34 Deutéronome 28.28-28.29 Esaïe 56.10 Esaïe 1.15 Nombres 19.16
15 Watu waliwapigia kelele, Ondokeni, Uchafu, Ondokeni, ondokeni, msiguse; Walipokimbia na kutanga-tanga, watu walisema kati ya mataifa, Hawatakaa hapa tena.
Lévitique 13.45-13.46
16 Hasira ya Bwana imewatenga, Yeye hatawaangalia tena; Hawakujali nafsi za wale makuhani, Hawakuwaheshimu wazee wao.
Lamentations 5.12 Esaïe 9.14-9.16 2 Chroniques 36.17 Deutéronome 32.26 Psaumes 106.44
17 Macho yetu yamechoka Kwa kuutazamia bure msaada wetu; Katika kungoja kwetu tumengojea taifa Lisiloweza kutuokoa.
Ezéchiel 29.16 Ezéchiel 29.6-29.7 Esaïe 20.5 2 Rois 24.7 Jérémie 8.20
18 Wanatuvizia hatua zetu, Hata hatuwezi kwenda katika njia zetu; Mwisho wetu umekaribia, siku zetu zimetimia; Maana mwisho wetu umefika.
Amos 8.2 Ezéchiel 7.2-7.12 Jérémie 16.16 Lamentations 3.52 Ezéchiel 12.22-12.23
19 Waliotufuatia ni wepesi Kuliko tai za mbinguni; Hao walitufuatia milimani, Nao walituotea jangwani.
Esaïe 5.26-5.28 Habakuk 1.8 Jérémie 4.13 Esaïe 30.16-30.17 Deutéronome 28.49
20 Pumzi ya mianzi ya pua zetu, masihi wa BWANA, Alikamatwa katika marima yao;Ambaye kwa habari zake tulisema,Chini ya kivuli chake tukakaa kati ya mataifa.
2 Samuel 19.21 Jérémie 39.5 Genèse 2.7 Ezéchiel 12.13 2 Samuel 1.14
21 Furahi, ushangilie, Ee binti Edomu, Ukaaye katika nchi ya Usi; Hata kwako kikombe kitapita, Utalewa, na kujifanya uchi.
Job 1.1 Amos 1.11 Psaumes 137.7 Ezéchiel 25.6 Ezéchiel 35.11-35.15
22 Uovu wako umetimia, Ee binti Sayuni; Hatakuhamisha tena; Atapatiliza uovu wako, Ee binti Edomu; Atazivumbua dhambi zako.
Esaïe 40.2 Psaumes 137.7 Jérémie 32.40 Lamentations 4.6 Esaïe 60.18

Cette Bible est dans le domaine public.